Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI atauliza: - Je, ni lini Serikali itafunga Mtambo wa Mashine ya Oxygen katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa ili kuhudumia wagonjwa wa dharura?

Supplementary Question 1

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya kupimia saratani ya matiti katika hospitali ya rufaa Mkoa wa Iringa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nafikiri Mheshimiwa Mbunge hilo ni hitaji la msingi kwa sababu mashine hiyo iko kwenye Hospitali ya Kanda ya Mbeya, lakini ni vizuri ikapatikana kwenye hospitali ya Mkoa wa Iringa. Basi mimi na wewe tuje tukae tushirikiane na wenzetu ili tuone ni namna gani tunaweza tukaweka utaratibu wa mashine hiyo kupatikana kwa sababu fedha zipo.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI atauliza: - Je, ni lini Serikali itafunga Mtambo wa Mashine ya Oxygen katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa ili kuhudumia wagonjwa wa dharura?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Halmashauri ya Ushetu imekamilika ujenzi wake, lakini wananchi bado wanatembea zaidi ya kilometa 80 kwenda kupata matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama.

Je, ni lini Serikali italeta vifaa tiba katika hospitali hiyo ili wananchi hawa waanze kupata matibu karibu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza priority ambayo Mheshimiwa Waziri wa Afya ameelekeza sasa hivi ni kuhakikisha hospitali zote zile ambazo zimeshajengwa vituo vya afya, zahanati na hospitali za Wilaya na majenzi yote, kuhakikisha sasa vifaa tiba vinaenda kununuliwa. Kama ambavyo nilisema jana sasa hivi shida siyo fedha kwa sababu Rais wetu kama nilivyosema tayari alishapeleka shilingi bilioni 333.8 na tayari kila mwezi kuna utaratibu wa kupeleka shilingi bilioni 15 MSD. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kwanza nitumie fursa hii kwa kushirikiana na wenzangu wa TAMISEMI kwamba RMO asimamie kwanza OPD kwenye hiyo hospitali ianze, kwa sababu inawezekana kuanza OPD mapema na kujipanga kwa ajili ya kuanza wakati tunangojea vifaa vya kuhakikisha hospitali hii inaenda kufanya kazi kama full flagged kama hospitali ya Wilaya. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI atauliza: - Je, ni lini Serikali itafunga Mtambo wa Mashine ya Oxygen katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa ili kuhudumia wagonjwa wa dharura?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Wilaya ya Tanganyika imekamilika kila kitu, tatizo lililopo ni ukosefu wa vifaa tiba ambavyo vinapelekea huduma ya upasuaji kukosekana katika hospitali hiyo.

Je, ni lini itakamilisha kuleta vifaa tiba ambavyo vimebaki katika hospitali hiyo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza hospitali hiyo tuliitembelea na nilitegemea Mheshimiwa Mbunge kwanza angeshukuru kwa Digital X-Ray ambayo tayari tuliikabidhi pale siku ile, yeye hakuwepo lakini Mkuu wa Wilaya alipokea kwa niaba yake.

SPIKA: Ngoja Mheshimiwa Naibu Waziri subiri kidogo, Waheshimiwa Wabunge nilishatoa maelekezo hapa kwa hiyo usimuweke Mbunge mazingira kwamba yeye hatambui huo mchango uliotolewa, anatambua mchango ni kwa sababu maswali lazima yawe mafupi, kwa hivyo anaenda moja kwa moja kwenye swali na wewe nenda moja kwa moja kwenye jibu la swali alilouliza. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni ukweli anachokisema Mbunge kulikuwa na vifaa vya Shilingi Milioni 507 vilitakiwa zipelekwe vimepelekwa vifaa vya Shilingi Milioni
203 vitaenda kumaliziwa mwaka huu kuhakikisha vimepelekwa vilivyobakia.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI atauliza: - Je, ni lini Serikali itafunga Mtambo wa Mashine ya Oxygen katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa ili kuhudumia wagonjwa wa dharura?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Je, ni lini zile mashine ulizokuja kukagua mwaka jana ukaniahidi baada mwezi utaleta Wataalam wa dialysis zitaanza kufanya kazi katika Hospitali ya Mkoa ya Iringa? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nalipokea swali lake na kwa sababu tulienda wawili tukalitembelea eneo, naomba tukutane tukae pamoja tuhakikishe hiyo kazi inaanza mara moja.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI atauliza: - Je, ni lini Serikali itafunga Mtambo wa Mashine ya Oxygen katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa ili kuhudumia wagonjwa wa dharura?

Supplementary Question 5

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, asante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itakamilisha taratibu za manunuzi ya mashine ya CT-Scan ambapo na tunategemea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi itapata mojawapo?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli anachosema Mheshimiwa Mbunge na tayari CT-Scan yao iko kwenye manunuzi kabla ya mwezi Juni itakuwa imefika ST-Scan ya hospitali ambayo Mheshimiwa Mbunge anaisema.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI atauliza: - Je, ni lini Serikali itafunga Mtambo wa Mashine ya Oxygen katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa ili kuhudumia wagonjwa wa dharura?

Supplementary Question 6

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na tatizo la MSD kutokuleta dawa kwa wakati katika Mkoa wa Kigoma, hata wakileta wanaleta chini ya asilimia 50.

Je, nini kauli ya Serikali katika kutatua changamoto hii? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli anachosema Mheshimiwa Mbunge na kama nilivyosema jana na nimerudia leo kwamba shida siyo fedha ni pale MSD Idara ya Manunuzi kumekuwa na tatizo ambalo Wabunge mmekuwa mkielezea.

Mheshimiwa Spika, siyo Kigoma tu nilikwenda Mkoa wa Lindi waliomba madawa 102 lakini ziko item 55 wakapewa Tano, kwa hiyo kuna tatizo kwenye eneo la manunuzi na ndilo ambalo mmekuwa mkizungumzia.

Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana na wenzetu tutaenda kulishughulikia. (Makofi)