Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, pamoja na yote hayo utaona kwamba Hospitali ya Temeke sasa hivi ni hospitali ya Kimkoa. Kwa nini, sasa basi isiwe muhimu kituo hiki cha afya cha Malawi kipandishwe nakuwa Hospitali ya Temeke kwa sababu ile ya Temeke ni ya Kimkoa sasa hivi?

Swali la pili; Je, ni lini sasa Serikali itatutengea fedha ili tuweze kujenga mochwari katika kituo hiki cha Malawi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dorothy Kilave Mbunge wa Jimbo la Temeke kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Dorothy Kilave kwa namna ambavyo anawasemea kwa dhati kabisa wananchi wa Jimbo la Temeke, nimhakikishie kwamba katika utaratibu ambao Serikali inaendelea kuufanya kila Halmashauri lazima iwe na hospitali ya Halmashauri, ni kweli kwamba hospitali ya Temeke ni Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa hiyo taratibu zitafanyika kufanya tathmini ya kituo cha afya cha Malawi kama eneo linatosheleza ili miuondombinu iongezwe ili baadaye iweze kupandishwa hadhi kuwa hospitali ya Halmashauri ya Temeke.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na jengo la mochwari tumeelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ianze kutenga fedha kwenye mapato ya ndani, ili ijenge jengo la kuhifadhia maiti na huduma hiyo iweze kuwa bora kwa wananchi wa Temeke.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe ina tatizo kubwa sana la mashine ya X-Ray ni lini Serikali itapeleka mashine yakisasa ya X-Ray kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe? Nashukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Mkundi Mbunge wa Jimbo la Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vifaa tiba zikiwemo X-Ray za kisasa ni moja ya vipaumbele ambavyo Serikali imeviweka na tunakwenda kwa awamu. Ninafahamu kwamba Hospitali ya Ukerewe ina X-Ray ya zamani ambayo imekuwa inaharabika mara kwa mara na Mheshimiwa Mbunge amekuwa mara kwa mara akikumbusha na kuomba Serikali iweze kupeleka X-Ray hiyo.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba tunaendelea kutafuta fedha na ni kipaumbele tukipata fedha tutahakikisha tunapeleka X-Ray katika kituo cha afya hicho.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali lini itakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ubungo iliyopo Kata ya Kimara ili iweze kupokea wagonjwa wa aina zote badala ya kupokea wagonjwa wa OPD ilivyo sasa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipeleka fedha takribani shilingi bilioni moja na milioni mia tano kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo na kazi ile inaendelea, nimefanya ziara pale zaidi ya mara tatu na huduma za awali zimeanza kutolewa.

Mheshimiwa Spika, hospitali ile itakamilishwa kwa fedha za awamu ya pili ambazo zitakwenda kukamilisha miundombinu ambayo imebaki.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 4

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera haina Mtaalam wa Mifupa na wagonjwa wanalazimika kupewa rufaa kwenda Bugando na hivyo kuwa na gharama kubwa.

Je, ni lini Serikali itapeleka Mtaalam huyo kuwasaidia wananchi?(Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hospitali zetu zote za Rufaa za Mikoa zimewekea mpango mkakati kwanza kwa kuhakikisha Wataalamu na Madaktari Bingwa wa yale magonjwa ambayo ni kipaumbele sana ikiwemo matatizo ya mifupa wanakuwepo. Kwa hivyo, tunapokea hoja ya Mheshimiwa Mbunge ili tuifanyie kazi kama Serikali tupate Daktari kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 5

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, assante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wetu wa Tabora na hasa Tabora Manispaa, bado wagonjwa wengi wa rufaa wanakwenda Bugando kwa sababu ya kuwa na upungufu mkubwa wa Madaktari Bingwa katika hospitali yetu ya rufaa ya Kitete, sijui Serikali ina mpango gani wa kutuletea Madaktari Bingwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetangulia kujibu swali la Mheshimiwa Rwamlaza, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha hospitali zetu za Rufaa za Mikoa zinakuwa na Madaktari Bingwa. Kwa hivyo, nimhakikishiwa Mheshimiwa Mbunge kwamba Hospitali ya Mkoa wa Tabora nayo ni kipaumbele na tutahakikisha tunapata wataalam hao kwa ajili ya huduma katika hospitali ile.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 6

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kituo cha afya cha Kata ya Malolo ni zaidi ya kilomita 150 mpaka hospitali ya Wilaya na kile kituo kimejengwa kwa nguvu ya wananchi na Waziri Mkuu amekichangia sana.

Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba ili kituo hiki cha afya kianze kufanya kazi katika ubora wake?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) : Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo Mbunge wa Jimbo la Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza ninawapongeza wananchi wa Kata ya Malolo kwa kujenga kituo cha afya kwa nguvu zao na Serikali imeendelea kuhamasisha wananchi kujenga vituo hivi kwa nguvu zao, Serikali ichangie nguvu za wananchi.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba katika mipango ya kuhakikisha vituo hivi vinapata vifaa tiba, tumeanza na Hospitali za Halmashauri lakini tutakwenda kwenye vituo vyetu vya afya ili vitoe huduma na kituo hicho pia kitapewa kipaumbele.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 7

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kituo cha afya cha Maskati Mkoani Morogoro kina Mhudumu mmoja wa afya. Je, ni lini Serikali itapeleka Wahudumu wa Afya katika kituo hicho?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwamba katika vituo vyetu vyote tunafahamu nchini kote kuna upungufu wa watumishi, ndiyo maana wiki iliyopita Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi, alitoa tangazo kwamba tutakwenda kuendelea kuajiri watumishi wa kada ambalimbali ikiwepo wa afya, nikuhakikishie kwamba tutatoa kipaumbele katika kituo cha afya ambacho kinahitaji mhudumu wa afya.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa na Wataalam wa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Malawi ambayo ipo Kata ya Buza Temeke?

Supplementary Question 8

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante Mheshimiwa Spika, wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais Mkoani Mara mwezi wa Pili mwaka huu, alielekeza kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda iweze kujengwa. Je, ni lini Serikali itajenga hospitali hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kajege Mbunge wa Jimbo la Mwibara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni maelekezo ya kuyafanyia kazi mapema iwezekanavyo na tayari Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumeshaanza kuweka taratibu ili tuanze ujenzi wa hospitali katika Jimbo la Mwibara. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba suala hilo tayari linafanyiwa kazi.