Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, kuna utafiti wowote ambao umefanyika ili kubaini dawa za ganzi/nusu kaputi zinazosababisha vifo kwa wanaojifungua kwa upasuaji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri. Niliomba kujua dawa ambazo zinasababisha akinamama kufa kutokana na ganzi; naomba sasa Serikali kupitia Wizara ya Afya ifanye utafiti ili tuweze kubaini ni dawa zipi ambazo zinasababisha wanawake wajawazito baada ya kujifungua wafariki? Kwa sababu hapa ametoa sababu nyingine, siyo zile dawa ambazo ilikuwa ni swali langu la msingi. Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, labda nimsaidie Mheshimiwa Mbunge kwamba leo mimi niliyesimama hapa huwa nikitumia flagyl nachubuka, lakini mimi kutumia flagyl na kuchubuka, haimaanishi flagyl inachubua watu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anatakiwa kujua kwamba vifo vya akina mama vimepungua kwa zaidi ya nusu kutokana na upasuaji unaofanyika na kutumia ganzi hizi hizi. Maana yake ni nini? Ganzi ambazo tunazozitumia leo hapa Bungeni, tuna Wabunge wengi wamefanyiwa operesheni na wametumia dawa hizi hizi na wako salama. Maana yake ni nini? Tumesema kuna sababu za vinasaba na kuna sababu nyingi ambazo zipo; sasa hizo haziwezi kufanya tukaleta taharuki kwenye nchi.

Mheshimiwa Spika, sisi madaktari huwa ni watu ambao tuna miiko na tunaapa na tuna maadili ya taaluma. Sasa ni muhimu sana unapouliza swali uhakikishe kwamba huvuki ile mipaka ya kitaaluma na miiko kwa sababu kimsingi labda kama angetaka nimweleze ninaposema DNA maana yake nini; ninaposema ganzi, maana yake ni nini? Kwa sababu kuna ganzi ukipigwa hapa kwenye mgongo inasababisha mtu kutokupumua. Kuna procedure za kufanya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nakuomba tuonane kama wanataaluma ili tuweze kusaidiana nawe uelewe jambo linafanyikaje?