Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali iliamua kujiondoa kwenye mpango wa uendeshaji wa Serikali kwa uwazi wakati silaha kubwa ya kupambana na rushwa ni uwazi?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza swali langu halijajibiwa. Naomba niulize maswali maeili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna mikataba mbalimbali ambayo tunaridhia katika nchi yetu, nini kilitokea mpaka tukajitoa katika OGP?

Mheshimiwa Naiibu Spika, swali langu la pili, kama alivyosema kwamba kuna vyombo mbalimbali ambavyo tunavitumia kama alivyoainisha. Sasa ni nini kinatufanya tusiridhie katika mikataba hiyo wakati sisi nchi yetu si kisiwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Tendega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, kwamba kwanini tulijitoa; tulikuwa tayari tupo na Mkataba wa Umoja wa Mataifa yaani UPRM, (Universal Periodical Review Mechanism) ambayo inafanyiwa review kila baada ya miaka minne, ambayo ni ya umoja wa mataifa. Wakati huo huo tulikuwa kwenye OGP ambayo ni CSO private sector.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tayari nchi yetu ipo katika mikataba ya Umoja wa Mataifa kama vile UPRM. Nikienda kwenye swali lake la pili, why tusiridhie. Kama nilivyojibu kwenye swali la kwanza lakini kwenye majibu yangu ya msingi, tayari tuna mechanism zetu za ndani ya nchi, kama vile Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, tuna taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. Tuna mechanism nyingi ambazo zinaangalia uwazi na utawala bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeweka wazi mbele taasisi zetu na mifumo yetu yote hii itafanya kazi kwa uwazi na uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.