Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa maeneo yote aliyoyataja hayana vituo vya Polisi: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kutupatia gari liendelee kuimarisha ulinzi eneo hilo huku tukiwa tunasubiri kujengwa kwa vituo hivyo? Hilo ni namba moja.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa eneo la Ngara liko mpakani na changamoto ya ulinzi na usalama ni kubwa, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuambatana nami tukaone changamoto hizo sambamba na kutatua mgogoro wa Rusumo Magereza na wananchi wa kijiji cha Magereza? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ruhoro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu kusaidia gari kwa ajili ya kuimarisha usalama na ulinzi wa raia na mali zao, kama ilivyojibiwa siku tatu zilizopita na Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi hapa, Wizara kweli itapata magari 78 mwishoni mwa mwezi huu ambapo tathmini itafanyika kuona Halmashauri yenye changamoto kubwa iweze kuzingatiwa ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Ngara na hasa ukizingatia iko mpakani.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuambatana naye, niko tayari kuongozana naye wakati wowote nafasi itakapopatikana hususan baada ya Bunge hili ili kuweza kuona changamoto zake na kuzifanyia kazi. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wilaya ya Maswa hasa katika Mji wa Maswa hatujawahi kujengewa Kituo cha Polisi toka tumepata uhuru mwaka 1961: -

Je, ni lini Serikali itajenga kituo chake katika Wilaya ya Maswa na nyumba za maaskari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Nyongo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba kweli ziko wilaya hasa Wilaya kongwe kama Maswa hazina vituo vya polisi kwa maana ya ngazi ya OCD. Wizara ina mpango wa kuzijengea vituo vya polisi vya ngazi ya wilaya, wilaya zote ambazo hazina vituo hivyo kwa kutegemea upatikanaji wa fedha. Nami nafahamu wilaya hii kwa sababu pia ina mapori kule na hifadhi, wanahitaji kituo hiki, hivyo tutaipa kipaumbele katika mpango huo. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi. Wananchi wa Kata Kakunyu, Wilaya ya Misenyi ambapo ni mpakani mwa nchi yetu na Uganda, wamejenga kituo cha polisi mpaka kuezeka.

Je, ni lini sasa Serikali itawaunga mkono kumalizia kituo hicho wapate huduma za kipolisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kyombo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema, wananchi wamejenga kituo, wanahitaji msaada wa kumalizia. Hatua watakayoanza ni kutathmini kiwango gani cha fedha kinatakiwa ili kukamilisha kituo hicho ili kuona kama tunaweza tukatumia sehemu ya fedha ya tuzo na tozo kwa ajili ya ku- support vituo hivi ambavyo viko mpakani. (Makofi)

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Jimbo la Kinondoni lina watu wengi sana na mahitaji ya usalama wa watu hao pamoja na mali zao ni mkubwa, hasa ikitiliwa maanani nyumba ziko karibu karibu sana: -

Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka kuruhusu vituo vidogo vya Polisi vinavyofungwa saa 12 vifanye kazi masaa 24 ili kuweza kusaidia usalama katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abbas kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua wingi wa watu kwa wananchi wa Kinondoni na umuhimu wa kuwa na vituo vidogo vya Polisi katika maeneo mbalimbali. Tutatathmini kwa sababu ili Kituo Kidogo cha Polisi kiweze kufanyakazi saa 24, vinahitaji rasilimaliwatu; na muundo wa kituo kile kuweza kuhifadhi silaha na mambo kama hayo. Kwa hiyo, tutatathmini kuona mahitaji, tutashauriana na Mheshimiwa Abbas kuona namna gani tuvifanye viweze kutoa huduma saa 24. (Makofi)

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa
Spika, ahsante sana kwa nafasi ya swali la nyongeza. Kwa kuwa Jiji la Tanga limetanuka na lina makazi mapya mengi, sasa ni lini Serikali itajenga vituo vya Polisi katika maeneo ya Kange Uzunguni, Kange Mbugani, Mwahako na Mwakidila? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanaisha Ulenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua ukubwa wa Jiji la Tanga na kwa kweli limepanuka sana na umuhimu wa kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo hayo ni mkubwa, kwa hiyo tutashauriana na uongozi wa Polisi wa Mkoa ili kuwajumuisha wadau akiwemo Mheshimiwa Ulenge na wengine wadau wema kuanza kujenga Vituo vya Polisi kwenye maeneo haya yaliyopanuka ili kuimarisha ulinzi kwenye maeneo hayo. (Makofi)

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 6

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tuna Kituo cha Polisi katika Wilaya yetu ya Kigoma DC, Kituo cha Polisi cha Mkuti, ukiangalia matukio mengi sana ya kihalifu yanafanyika katika eneo lile.

Je, ni lini Serikali itaweza kumalizia Kituo kile cha Polisi katika hali iliyopo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Makanika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nipo tayari kufuatana na Mheshimiwa Makanika baada ya Bunge hili ili kuona mahitaji ya kituo hicho kwa maana ya kufanya tathmini, kuona fedha zinazohitajika ziweze kutengwa katika bajeti zetu zinazofuata. (Makofi)

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 7

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, Mji wa Mlandizi unakua kwa kasi na pale Mlandizi kuna majengo kwenye Kituo cha Polisi yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi. Je, ni lini Serikali itaweka nguvu za Serikali kusaidia nguvu za wananchi kumaliza nyumba zile? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutaomba uongozi wa Polisi wa Mkoa ilipo Wilaya ya Mheshimiwa ili iweze kufanya tathmini kujua kiwango cha fedha zinazohitajika kwa ajili kukamilisha ili tuweze kuingiza kwenye mpango na hatimaye kiweze kumaliziwa. (Makofi)

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 8

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika Jimbo la Shinyanga mjini Kituo Kikuu cha Polisi kilikuwa na hali mbaya jambo ambalo uongozi wa Polisi waliamua kujenga kwa fedha zao za ndani, lakini kituo hicho kipya kilichojengwa bado hakijakamilika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza fedha katika kituo hicho ili kiweze kukamilika? Nashukuru. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salome Makamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu uchakavu wa Kituo cha Polisi Shinyanga Mjini kinachohitaji ukarabati, tutafanya tathmini ili kuona kiwango cha fedha zinazohitajika kuwezesha ukarabati huo kufanyika, tuingize kwenye mpango wa bajeti katika miaka inayofuata.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Nyamagana, Keza na Djululigwa vilivyojengwa na wananchi?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi katika Kata ya King’ori?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pallangyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tupo tayari kushirikiana na Mbunge na wadau wengine wa Kata ya King’ori kuona kiwango cha ujenzi kinachotakiwa kumaliziwa ili tuweze kutengea fedha kituo hicho kiweze kukamilishwa. (Makofi)