Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, kuna wahanga wangapi wa vitendo vya ukatili nchini kuanzia mwaka 2019 hadi 2022?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ninamshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa idadi kubwa ya waathirika wa ukatili ni wanawake na watoto.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzuia idadi kubwa ya takwimu tunazoletewa hapa ili kupunguza ukatili huo? (Makofi)

Swali la pili, pamoja na kuwa Serikali imetoa taarifa kuwa wanaume 3,077 ndiyo waliofanyiwa ukatili wa kulawitiwa, sina shaka idadi kubwa itakuwa ni watoto wa kiume.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwalinda watoto wa kiume ili kusudi wasifanyiwe ukatili? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la takwimu linaweza kuonekana kwamba ni nyingi kwa sababu ya jitihada ambazo Serikali imechukua kupitia Jeshi la Polisi la kuanzisha Dawati la Kijinsia, ambapo hapo zamani watu wengi ilikuwa wanapata shida au wanaona aibu kuripoti matukio kama haya kwenye counter ya polisi. Kupitia uendeshwaji wa dawati hili watu wengi zaidi wamekuwa wakijitokeza na kutoa taarifa na hivyo basi kufanya sasa yale matukio ambayo hayatolewi taarifa zamani sasa yanaweza kutambulika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la mikakati ya kuwalinda. Suala la kuwalinda watoto wetu si jukumu la Serikali peke yake, hili ni suala la kila mmoja wetu tukianzia wazazi. Kwa hiyo, niseme wakati Serikali inafanya kila jitihada kuhakikisha kwamba inaweka mazingira mazuri ya ulinzi ikiwemo kuhakikisha kwamba inachukua hatua kali kwa wale wote ambao wanahusika na vitendo vya kuzalilisha Watoto wetu naomba sana wazazi na wenyewe wachukue majukumu yao ipasavyo, kwa maana ya kuangalia kuhakikisha wanafuatilia nyendo za watoto wao na kuhakikisha kwamba wanawalinda na kuwasimamia. (Makofi)

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, kuna wahanga wangapi wa vitendo vya ukatili nchini kuanzia mwaka 2019 hadi 2022?

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.

Kwa kuwa vitendo vya ukatili vimezidi kuongezeka kila siku tunasikia matukio mbalimbali, na kwa kuwa adhabu mbalimbali zinatolewa lakini vitendo vinazidi kuongezeka.

Je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka wa ku-review hizi adhabu ili ziwe kali zaidi watu wasiendelee kufanya hivi vitendo vya ukatili? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Malapo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ametoa wazo zuri nadhani ni jambo la kulichukua na kulitafakari na kulifanyia kazi. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: - Je, kuna wahanga wangapi wa vitendo vya ukatili nchini kuanzia mwaka 2019 hadi 2022?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kumekuwa na mauaji na vipigo vingi sana kisa wivu wa kimapenzi. Serikali inachukua jukumu gani la kuhakikisha wale wanaofanya vitendo hivyo wanachukuliwa hatua kali na za haraka ili mambo hayo yasiendelee kutokea katika jamii ya kitanzania. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli yametokea matukio ya mauaji yenye vyanzo mbalimbali ikiwemo chanzo ambacho amekizungumza Mheshimiwa Mbunge. Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba adhabu hizo hazijasaidia. Lakini labda nieleze kwa ufupi kwamba, ukiangalia katika kipindi cha mwezi Januari mpaka Februari tulishuhudia matukio mengi sana ya mauaji ya vyanzo mbalimbali kwenye jamii, ikiwemo vyanzo hivyo vya wivu wa mapenzi, ushirikina, ulevi uliokithiri, kugombania mali, urithi na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumechukua hatua ya kuunda Tume, Tume imefanya kazi yake vizuri imetuletea mapendekezo mengi, lakini katika mambo makubwa na ya msingi ambayo nimetaka nilizungumze hapa kwamba mbali ya kuchukua hatua jambo kubwa la msingi ni kuhakikisha kwamba tunadhibiti matukio kama haya yasijitokezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia taarifa ambayo tumepewa na Tume kuna hatua mbalimbali ambazo tumezichukua za kuhakikisha tunadhibiti. Moja katika hatua muhimu sana ambayo tumechukua ni kuhakikisha kwamba tunaimarisha mifumo katika ngazi za Kata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Jeshi la Polisi mtakumbuka hivi karibuni walihitimu askari zaidi ya zaidi ya 4,200 na zaidi, hao wote tumewapeleka kwenye kata kuhakikisha kwamba kwenye kata tuna askari wa kutosha ambao wana weledi wa kusimamia masuala ya usalama katika ngazi husika na kushirikiana na Kamati za Ulinzi za Kata pamoja na wadau mbalimbali ikiwemo wananchi kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, mbali ya kuchukua hatua lakini jitihada kubwa vilevile tunazielekeza katika kudhibiti matukio kama haya yasiweze kujitokeza.