Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Utekelezaji wa maagizo ya Serikali Kuu kwa Halmashauri imekuwa ni changamoto na mzigo mkubwa kwa Halmashauri hizo hususan Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambapo maagizo mengi hayamo kwenye Mpango wa Bajeti na hivyo utekelezaji unakuwa mgumu. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha maagizo hayo yanatengewa bajeti?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri Jafo mpaka sasa tunavyoongea baadhi ya shule za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ikiwemo Shule ya Sekondari Magindu, Shule ya Ruvu Station na Shule ya Dosa Aziz katika kutii agizo la Serikali Kuu la kujenga maabara katika shule zetu za sekondari inakabiliwa na madeni makubwa ya wazabuni pamoja na mafundi. Swali langu la kwanza, ninaomba kauli ya Serikali, je, itakuwa tayari ku-clear madeni hayo ili kutua mzigo Halmashauri zetu?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, ni lini sasa Serikali Kuu itaacha kubebesha mizigo Halmashauri kwa kutoa maagizo nje kabisa ya bajeti ya Halmashauri ya kuzitaka zitekeleza maagizo ya Serikali kuu ikiwemo hili agizo jipya la kila mtoto kukalia dawati pasipo kuwatengea fungu maalum. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa agizo la ujenzi wa maabara na agizo lile lilikuwa ni agizo la kimkakati. Kwa sababu shule nyingi sana katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa hizi shule za kata zilikuwa zina upungufu wa maabara. Sambamba na hiyo watoto walikuwa wakienda shuleni wanakosa fursa ya kupata masomo ya sayansi, kwa mtazamo ulio makini ndiyo maana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
16
alitoa agizo hilo. Lakini naomba niseme wazi kwamba agizo lile limeleta manufaa makubwa sana kwa watoto wetu wanaosoma shule za kata. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hili niwapongeze Watanzania wote kwa ujumla wamejitahidi katika kila eneo moja kufanya fursa, hata Halmashauri ya Kibaha najua walikuwa na mchakato wa kujenga takribani maabara nane, changamoto iliyokuwepo ni upatikanaji wa fedha ilikuwa ni changamoto kubwa kwa sababu Kibaha peke yake walichanga shilingi milioni 218. 6 lakini bahati mbaya upelekaji wa fedha haukuwa vizuri.
Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie suala la upelekaji wa fedha lilikuwa sio suala la sekta ya elimu peke yake, mnakumbuka hata miradi ya maji ilisimama ndiyo maana ajenda kubwa ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliposhika madaraka aliazimia kuhakikisha kwamba kodi inakusanywa ili mradi kulipa madeni ya wakandarasi wa aina mbalimbali. Hili naomba niseme pale kuna wakandarasi wanadai na niseme Serikali inalitambua hilo na juhudi ya Serikali itaendelea kukusanya kodi ili mradi kulipa madeni ya wakandarasi kwa kadri iwezekanavyo kuweza kutatua tatizo hilo.
Mheshimiwa Spika, suala lingine ni lini Serikali sasa itaacha kutoa maelekezo haya. Naomba niwaambie ndugu zangu, Serikali inapima nini kifanyike katika muda gani na hivi sasa mnakumbuka kuna maagizo mbalimbali yametoka lakini lengo lake kubwa ni kuisaidia jamii.
Kwa hiyo, naamini maagizo yote yaliyotolewa na Serikali ni maagizo na kuona ni uhitaji wa kiasi gani uweze kufanyika kwa ajili ya kutatua matatizo ya Watanzania. Lakini hili nililosikia kwamba kila mtoto achangie dawati, hili nadhani ngoja tutalifanyia kazi kwa sababu maagizo yetu ya Serikali kama watu watachangia ni wadau wenyewe katika maeneo husika wanajihamasisha kama tunavyoona hivi sasa, na juzi nishukuru nilikabidhi madawati hapa Dodoma. Watu/wadau waliamua kuchangia madawati lakini siamini kama kuna watu wanalazimishwa kuchangia madawati kwa sababu hizo ndiyo miongoni mwa kero tuliamua kuzitatua katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzana ili mradi mwananchi wa kawaida aweze ku-access elimu ya mtoto wake. Ahsante.

Name

Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Utekelezaji wa maagizo ya Serikali Kuu kwa Halmashauri imekuwa ni changamoto na mzigo mkubwa kwa Halmashauri hizo hususan Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha ambapo maagizo mengi hayamo kwenye Mpango wa Bajeti na hivyo utekelezaji unakuwa mgumu. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha maagizo hayo yanatengewa bajeti?

Supplementary Question 2

MHE. FREEMAN H. MBOWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
17
Maadam Mheshimiwa Waziri ameeleza kwamba maelekezo ambayo Serikali Kuu inatoa kwa Serikali za Mitaa yanasimamiwa ama yanasimamia msingi wa nia njema na kwa sababu tunakubaliana katika utawala wa nchi, nia njema haiwezi ikazidi utaratibu uliowekwa kwa sheria, kanuni na taratibu za kiutawala na kwa sababu kumekuwepo na tatizo kubwa sana la muingiliano wa maelekezo hususan kwenye zile Hamlashauri za Wilaya ama Manispaa ambazo zinaongozwa na vyama tofauti na Chama cha Mapinduzi.
Je, ili kuweka utawala wa sheria, unaoheshimu mifumo yetu ya kiutawala iliyowekwa na sheria, Waziri haoni kwamba ni muhimu na busara sana Serikali ikatoa tamko katika Bunge hili kwamba viongozi katika ngazi ya Wilaya kwa maana ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa waache kuingilia majukumu ya Halmashauri za Wilaya na Manispaa ili kuruhusu maamuzi ya vikao vya Madiwani na wengine kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu za sheria?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba tuweke kumbukumbu sawa sawa, lengo letu Serikali za Mitaa zimewekwa kwa mujibu wa Katiba Ibara 145 na utekelezaji wake unaelezewa katika Ibara 146; kwa hiyo, maana yake ni chombo halali ambacho kiko kwa mujibu wa sheria. Nimesema pale awali maelekezo hasa ya kutoka Serikali Kuu, maana yake kikubwa zaidi yanania njema kama Mheshimiwa Mbowe ulivyorejea hapa. Lakini anasema jinsi gani Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wasiingilie maamuzi, kinachofanyika ni kwamba Wakuu wa Mikoa na Wilaya sio wanaingilia, wanachokifanya ni nini? Kinachotakiwa hasa cha msingi ni kuona kama utaratibu unakiukwa pale Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya ana haki ya kuweza kuliingilia hilo jambo lisiharibike kwa ajili ya maslahi ya umma. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nina imani haiwezekani kikao halali cha baadhi ya Madiwani kimefanya ambayo hakuna utaratibu wowote uliokiukwa Mkuu wa Mkoa au Wilaya atakuwa ameingilia. Lakini kama kuna jambo linaenda kinyume na Mkuu wa Mkoa yupo, naye anaona jambo linaharibika kwa makusudi mbele yake ni lazima aingilie hapo ilimradi kuweka mambo sawasawa. Kwa sababu mwisho wa siku ni kwamba watu wanatarajia kwamba Serikali hiyo iliyowekwa kwa mujibu wa sheria basi itatimiza majukumu yake kama wananchi walivyoipa ridhaa itawaongoza katika kipindi hicho mambo yanayohitajika yaweze kufikiwa na yaweze kufahanikiwa. Kwa sababu sasa hivi Tanzania tunaongozwa kwa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020.
Mheshimiwa Spika, lengo kubwa ni kwamba kuanglia kama Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya aharibu utaratibu wa Baraza la Madiwani lakini wanahakikisha kwamba utekelezaji wa Ilani unakamilika kama ilivyokusudiwa na wananchi walioichagua Serikali hiyo.