Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuboresha minara ya mawasiliano ya simu katika Kata za Makurunge na Fukayosi?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kunipa nafasi hii, lakini nitumie nafasi hii kwanza kuipongeza Serikali, nimepitia taarifa yao ya miradi ya Tanzania ya Kidigitali, nimeona Kata za Gwata, Bokomnemela na Dutumi zimewekwa kwenye orodha ya Kata 763; nawashukuru sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa swali la nyongeza; je, ni lini wakandarasi hawa ambao wameshapatikana watafika kwenye kata hizo na kuanza utekelezaji wa mradi husika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni kwa kiwango gani huduma ya 3G inawasaidia Watanzania? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tumejibu katika swali la msingi, tender ya upatikanaji wa mawasiliano katika miradi ya World Bank ambayo ilitangazwa tarehe 24 itafunguliwa tarehe 2 Desemba. Na baada ya kufunguliwa, mchakato wa upatikanaji wa vibali na hatimaye kuanza kwa hatua za ujenzi utakapokamilika ujenzi wa mawasiliano katika hizo kata utaanza mara moja.

Mheshimiwa Spika, katika kipande cha pili cha swali la Mheshimiwa Mwakamo, ni kwamba huduma ya 3G itawafikia lini Watanzania?

Mheshimiwa Spika, labda nitoe tu takwimu za harakaharaka; katika teknolojia ya 2G mpaka sasa kwa population coverage mpaka sasa Tanzania tumefikia asilimia 96; lakini kwa 3G tumeshafikia asilimia 72; 4G tumeshafikia asilimia 55. Internet penetration mpaka sasa kwa nchi yetu ni asilimia 50. ahsante sana.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuboresha minara ya mawasiliano ya simu katika Kata za Makurunge na Fukayosi?

Supplementary Question 2

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa ya swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa katika orodha aliyotoa Mheshimiwa Waziri ya usambazaji wa minara vijijini kata zangu za Kaengesa, Mfinga, Izimba na Milepa hazimo; je, Serikali mna mpango gani wa kupeleka minara katika kata hizo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo uliagiza Wizara yetu tulete orodha hapa Bungeni, orodha hiyo ina segments mbalimbali; ina borders and special zone, phase six, miradi 763, vijiji ambavyo vimeshafanyiwa tathmini 2,116. Kama ukiangalia kwenye kata 763 haupo, basi tunaamini kabisa katika vijiji 2,116 unaweza ukawemo. Na kama utakuwa haupo basi tunaamini kwamba katika hatua za kuendelea kufanya tathmini tutaviingiza vijiji hivyo ili vipate mawasiliano, ahsante.