Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Tunduru?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tunaishukuru Serikali kwa kuwa na azma nzuri ya ujenzi wa Vyuo vya VETA katika Wilaya zote 63. Swali dogo tu la nyongeza, je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa vyuo hivyo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoanza kueleza katika swali la mwanzo kwamba vyuo hivi tutajenga vyote kwa pamoja na tunachosubiri sasa ni upatikanaji wa fedha ambazo ndizo tumeshafanya maombi kwa Wizara ya Fedha na Mipango; na mara tu tutakapopata fedha hizi ujenzi huu utaanza kwenye vyuo vyote 63 katika Wilaya zote 63 kwa pamoja. Nakushukuru sana.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Tunduru?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante; katika hesabu ya Halmashauri 63, je, na Mbogwe imo kwenye hesabu hiyo Mheshimiwa Waziri? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nicodemas Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Mbogwe ni Wilaya, sina uhakika sana kwa sababu kuna Wilaya ambazo zina majimbo mawili. Kwa hiyo, hapa kwenye majimbo mawili ina maana tunapokwenda kujenga ni Wilayani, sasa kama Mbogwe ni Wilaya ambayo inajitegemea itakuwa imo, lakini kama Mbogwe ni jimbo miongoni mwa Wilaya ina maana tutakapokwenda kujenga ni Wilayani ambako na Mbogwe ita-share chuo hicho ambacho kitajengwa katika Wilaya hiyo ambayo Mbogwe ipo kwenye Wilaya husika.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Tunduru?

Supplementary Question 3

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, kwanza naomba niishukuru Serikali kwa kujenga Chuo cha VETA pale Uvinza.

Sasa nauliza; ni lini chuo kile kitafanya kazi ili watoto wa pale waweze kuanza kuingia chuoni? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Nashon, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna vyuo vyetu 25 vya Wilaya ambavyo tulianza ujenzi wake toka mwaka 2021 na ujenzi ule uko kwenye hatua za mwisho. Hivi sasa tunatengeneza samani au tunasambaza samani pamoja na vifaa vya kufundishia. Ni matarajio yetu katika mwaka ujao, 2023 vyuo hivi 25 vya Wilaya pamoja na vile vinne vya mikoa vitaanza kutoa mafunzo rasmi. Nakushukuru.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Tunduru?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi; elimu ya ufundi ni nyenzo muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yoyote.

Je, Serikali haioni sasa kwamba ni muhimu kubadilisha utaratibu, badala ya kujenga hivi vyuo kiwilaya ijenge kijimbo kwa sababu, kuna Wilaya nyingine ambazo zina majimbo mawili?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kada hii ya ufundi ni muhimu, naomba tuchukue ushauri wa Mheshimiwa Mbunge, hivi sasa tumeanza katika ngazi ya kanda, mikoa pamoja na ngazi ya Wilaya. Tuangalie baadaye namna gani tunaweza tukafika katika ngazi ya jimbo kama Mheshimiwa Mbunge anavyoshauri.

Kwa hiyo, tunaubeba ushauri wako tunakwenda kuufanyia kazi na tufanye tathmini ya kina. Nakushukuru sana.