Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Busega?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kutoa pesa za ujenzi wa VETA ya Mkoa wa Simiyu na mpaka sasa ujenzi unaendelea. Kwa kuwa sSera ya Serikali ni ujenzi wa VETA kila Wilaya; ni lini sasa Serikali itajenga VETA katika Wilaya ya Simiyu ambayo haina VETA?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni azma ya Serikali kujenga vyuo hivi katika Wilaya ambazo hazina vyuo na hivi sasa tuko katika mkakati au mchakato wa kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa VETA hizi. Mara tu pesa zitakapopatikana tutahakikisha kwamba, tunaanza ujenzi mara moja. Nakushukuru sana.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Busega?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Rorya ni moja ya Wilaya ambazo na sisi tumeanza mchakato wa muda mrefu sana kwa ajili ya maombi ya kupata Chuo cha VETA, na Mheshimiwa Waziri unakumbuka nimekuwa nikikusumbua sana kwa muda mrefu ili angalau na sisi tuweze kupata chuo cha VETA. Nilitaka nijue sasa kwenye mpango wa bajeti ya mwaka huu katika vyuo vya VETA 63 kama na sisi Wilaya ya Rorya tumo katika vyuo hivyo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya zilizobaki ambazo hazina Vyuo vya VETA ni Wilaya 63, tafsiri yake Wilaya ya Rorya nayo imo katika ile orodha. Tafsiri yake tunataka tujenge katika Wilaya zote ambazo hazina vyuo kwa awamu. Kwa hiyo, katika awamu ya kwanza tutaanza kwa Wilaya zote ambazo hazina kwa pamoja katika mwaka huu wa fedha na mwaka unaofuata ina maana tutakuwa na jukumu la kumalizia kazi ile ambayo tutakuwa tumeianza katika mwaka huu wa fedha. Nakushukuru sana.

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Busega?

Supplementary Question 3

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Singida imeshatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa VETA na uhitaji ni mkubwa sana kwa wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa ajili ya chuo hiki.

Naomba commitment ya Mheshimiwa Waziri; je, Halmashauri ya Wilaya ya Singida nayo imo katika kupata chuo hiki? Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ramadhani, Mbunge wa Singida, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Singida ninachofahamu kuna Chuo cha VETA cha Mkoa wa Singida ambacho kipo katika Wilaya ya Singida. Kwa hiyo, maadam tuna chuo cha VETA cha Mkoa ambacho kipo katika Wilaya ya Singida, hatuwezi tena kwenda kujenga chuo kingine katika Wilaya hiyo hiyo. Kwa hiyo, kile Chuo cha VETA cha Mkoa wa Singida ndicho ambacho kitatumika kama chuo cha Wilaya ya Singida. Nakushukuru sana.