Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: - Je, ni lini marekebisho ya sheria yataletwa Bungeni ili mwanamke anayejifungua mtoto njiti aongezewe likizo ya uzazi?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsanta, nashukuru kwa majibu mazuri, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Kutokana na upungufu wa vifaa vya makuzi kwa watoto njiti kwenye hospitali zetu; njia kubwa inayotumika kulelea watoto ni kwa kukubambatiwa na mama zao yaani kangaroo style.

Je, Serikali haioni kuchelewesha marekebisho ya sheria kunaendelea kuhatarisha afya na uhai wa watoto hao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, watoto njiti wana haki ya kuishi na kulelewa katika mazingira mazuri kama watoto wengine.

Je, Serikali haina timeframe ya kufanyia marekebisho ili kuhakikisha kwamba uhai wa watoto hao unalindwa?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Judith Kapinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imekwishakuanza kuchukua hatua mbalimbali za kufanya maboresho katika sekta ya afya ikiwemo pamoja na ununuzi wa vifaa ambavyo vinawasaidia watoto hawa kuweza kukua.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, katika eneo hilo hilo, maboresho yamekuwa yanafanyika na Serikali imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali ipo moja ya taasisi katika taasisi nyingi ambazo zinafanya na Serikali, Doris Mollel Foundation pamoja na Vodacom wamekuwa wakifanya kazi hii kwa kushirikiana na Serikali na maeneo mengi tumeona wamefanya kazi kubwa ya kuwasaidia.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusu haki ya watoto, tayari Serikali kwa kuona umuhimu wa watoto lakini pia generation tayari ilikwishatunga sheria ya mwaka 2009 sheria ya mtoto ambao inatoa haki, moja ya haki ya msingi ambayo iko kwenye Katiba, haki ya kuishi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika kufanya hivyo Serikali imeendelea kuboresha katika sekta ya afya na kuweza kuhakikisha kwamba katika mazingira haya hata mabadiliko ambayo yanatakiwa kufanyika kwa upande wa Serikali tunayachukua haraka sana na kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, niseme tu katika hatua ya awali, tulikwishakuwinda Dar es Salaam, na tukakutana na taasisi mbalimbali/Asasi za Kiraia ambazo zilikuwa na ajenda hii hii na nilikuwa mgeni rasmi katika shughuli hiyo ya kuweza kuona namna gani tunaweza tukachukua best practice katika nchi yetu kuweza kuona tunawasaidia mama hawa wanaojifungua watoto njiti na kupunguza vifo. Ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: - Je, ni lini marekebisho ya sheria yataletwa Bungeni ili mwanamke anayejifungua mtoto njiti aongezewe likizo ya uzazi?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa watoto njiti hao wana haki kabisa kama alivyosema mwenye kutujibia maswali kutoka Serikalini.

Ni kwa nini sasa basi Serikali hailipi gharama ya mtoto huyo wakati ambapo yuko hospitali na inalazimu wazazi kulipa mpaka milioni tano ikiwemo Muhimbili Hospital? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, niseme kwanza moja kwa mwaka huu kwenye bajeti zimetengwa bajeti ya kujenga vituo vya watoto njiti 100, lakini katika module yetu ya kawaida pamoja kwamba hakuna sheria ambayo imetunga kwamba unampa mama huyu likizo, lakini kuna utaratibu wa ndani umekuwa ukifanyika wakati wote ambapo mama akitokea namna hiyo madaktari wanaandika na anapewa huduma.

Mheshimiwa Spika, lakini kwenye suala lako la kusema kwamba Serikali kwa nini hawalipii, kwenye mfuko wa bima kweli kulikuwa na changamoto hiyo kwamba anatokea mtoto njiti, lakini anatakiwa afanyiwe hivyo, lakini inaandikwa na sasa hivi tumeshaondoa hiyo na watoto njiti wanalipiwa na watoto chini ya miaka mitano huwa wanalipiwa bure kama sio bima. Kwenye mfuko wa bima ndio kulikuwa na shida na hiyo shida imeshamalizwa sasa hivi, watoto njiti wanahudumiwa kama kawaida.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: - Je, ni lini marekebisho ya sheria yataletwa Bungeni ili mwanamke anayejifungua mtoto njiti aongezewe likizo ya uzazi?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, mtoto njiti akizaliwa pale Muhimbili Hospital, anatakiwa alelewe mpaka afika ule umri ambao sasa mimba ingekuwa term na mtoto azaliwe na wengi wanakuwa na complication, lakini suala alilojibu Naibu Waziri mimi mwenyewe nilishafikisha kwake maombi ya kufadhili mtoto njiti ambaye alipitishwa kwangu na anaijua hiyo kesi ilifika mpaka shilingi milioni tano, ni watoto wa kawaida pamoja na hata wale waliokuwa kwenye insurance kama alivyoeleza yeye. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli alishanifikishia, mara nyingi kuna wenzetu kulikuwa na shida kweli Muhimbili, watoto wakipata matatizo si watoto tu hata wazee na watu wengine imekuwa kwamba wanakuwa-charged hasa hao watoto chini ya miaka mitano. Lakini tulipiga simu kwa sababu ni suala kisheria na halikuwa exempted na sasa tumeweka mfumo ambao hayo mambo hayajitokezi tena. Ahsante.