Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuzungumza na taasisi za kifedha ili mikopo kwa watu wenye ulemavu itolewe kwa mtu mmoja mmoja badala ya vikundi?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kufuatia majibu mazuri ya Serikali lakini bado changamoto inayoyakuta makundi haya ni pale unapokwenda kwenye taasisi za kifedha na kushindwa kufungua akaunti ya mtu mmoja. (Makofi)

Sasa ni lini Serikali itafanya makubaliano na mabenki ili makundi haya yaweze kunufaika na mikopo hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kufuatia hali ya watu wenye ulemavu na mazingira magumu ya biashara, je, Serikali haioni haja ya kuongezea muda marejesho makundi haya ikawa tofauti na makundi ya kinamama na vijana?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janeth kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza naomba tulichukue kama ushauri na nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji huo kwamba tutaona namna bora ya kuwasaidi watu wetu katika kuona utaratibu wa kupata mikopo kupitia taasisi hizo kama alivyoshauri.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, la kuhusiana na muda wa marejesho ni kweli tumekwishakuliona hilo Ofisi ya Waziri Mkuu kwamba watu wenye ulemavu ni kweli kwamba wanachangamoto. Unaweza ukakuta mtu wa kawaida ni tofauti na mtu mwenye ulemavu kwa sababu kuna wakati anahitaji kuwa na msaidizi ambaye yeye amekopa sawa, kama ni milioni 10 na mtu ambaye ni mzima naye ana milioni 10 lakini akienda kununua bidhaa atajikuta anahitaji kwenda na mtu wa kumsaidia kuona hizo bidhaa au kumsaidia kwenye usafiri.

Mheshimiwa Spika, pili hata atakapopata hitaji la chakula atahitaji amnunulie tena chakula msaidizi wake, na tatu hata anapokuwa anafanya biashara yake kwenye yale mazingira kama ni ana ulemavu wa kutokuona, atalazimika awe na mtu pale. Kwa hiyo, gharama inakuwa kubwa tofauti na hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tumeliona hilo na tunaona sasa namna gani ambavyo tunaweza tukaona utaratibu wa kubadilisha kanuni ili kuweza kuwanufaisha zaidi watu wenye ulemavu kwa sababu kama unavyofahamu hujafa hujauumbika sisi wote ni watarajiwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, ahsante.