Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati wa kukarabati barabara zilizo katika hali mbaya Wilayani Kyela kwani bajeti ya TARURA haitoshi?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii. Swali la kwanza; kwa kuwa Kyela ni sehemu ambayo ina mvua nyingi sana na huwa inakumbwa na mafuriko kwa kipindi kila mwaka. Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta fedha ambazo zimekosekana kwa muda mrefu kwa maendeleo ya barabara Wilayani Kyela?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa inajulikana barabara haziwezi kudumu kwenye mafuriko hasa hizi za changarawe na udongo. Je, Serikali imewahi kufanya utafiti wa kutafuta namna nyingine ya ujenzi wa barabara kwa mfano, kutumia enzymes katika kitengo chake cha utafiti hapo TARURA?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Jimbo la Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge, Serikali itaendelea kupeleka fedha kwa ajili ya barabara na nimwondoe shaka tu. Bahati nzuri Serikali sasa hivi imeongeza bajeti yake na sisi tumekuwa tukitekeleza vya kutosha. Kwa hiyo, hilo aondoe shaka kabisa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu tafiti katika maeneo ambayo barabara hazidumu kutokana na mvua nyingi kama ilivyo Kyela, utafiti huo umefanyika na moja ya mipango yetu ni kuja na majibu ambayo yatasaidia barabara za maeneo hayo ziweze kupitika muda wote. Kwa hiyo, Serikali ipo kazini na inafanya hii kazi kwa umakini kabisa ili kuwasaidia wananchi wake.