Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani na Mifupa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 1

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu hayo ya Serikali. Swali la kwanza; kwa kuwa magonjwa yasiyoambukiza ni tatizo kubwa katika Mkoa wa Lindi. Je, ni lini sasa watapeleka specialist hao wa internal medicine? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, ni lini Waziri atakwenda Mkoa wa Lindi pale Hospitali ya Sokoine kwenda kuona hali halisi ya ukosefu wa Madaktari hao na kadhia wanayopata wananchi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ni lini Serikali sasa itapeleka Daktari huyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tukae naye pamoja tuwasiliane na Afisa Utumishi na Wizara ya Utumishi tuone ni lini watakamilisha mchakato huo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, ameniuliza kwamba ni lini tutakwenda Lindi ili kwenda kuona matatizo yanayoendelea pale. Namuahidi Mheshimiwa Mbunge mara tu tukimaliza Bunge, tutashirikiana na yeye na Mbunge mwingine wa Mkoa wa Lindi twende huko. Ahsante.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani na Mifupa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Hospitali ya Mkoa wa Katavi inao upungufu mkubwa sana wa Madaktari Bingwa akiwemo Physician na Daktari Bingwa wa Watoto, pia Mkoa mzima Daktari Bingwa wa magonjwa ya wanawake yupo mmoja tu.

Je, ni lini Serikali itapeleka Madaktari Bingwa katika Mkoa wa Katavi?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge, kwanza hospitali yao ni mpya inayojengwa sasa, lakini ni kweli kwamba siyo tu kwa Mkoa wa Katavi bali upungufu wa Madaktari Bingwa uko karibu nchi nzima, ndiyo maana unaona kuna mkakati unaofanywa kuongeza Madaktari Bingwa. Nitashirikiana na Mheshimiwa Mbunge tuangalie la kufanya. Kwa sababu najua kuna Daktari wa Watoto aliyekuwepo pale alipelekwa Songwe, sasa tutaona ni nini kinafanyika ili kurekebisha hayo yaliyotokea. Ahsante.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani na Mifupa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Natambua kwamba kila hospitali ya Wilaya inayo shida ya kupata Madaktari Bingwa na upatikanaji wake kidogo unakuwa ni mgumu. Pia kuna Halmashauri zinakuwa na uwezo wa kusomesha Madaktari Bingwa, mojawapo ikiwa ni hospitali yangu. Sheria ya Utumishi inasema tukimsomesha at least afanye Miezi 36 ndiyo aweze kuhama. Sasa kwa sisi ambao tumepeleka Madaktari wakapata huo Ubingwa, halafu wakarudi ndani ya wiki moja wakahamishwa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anasemaje kuhusu hilo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwenye hili suala la Madaktari Bingwa siyo tu kwa hospitali za Wilaya hata za Mikoa kuna baadhi ya Mikoa ukimpeleka Daktari Bingwa ana-resign anakwenda sehemu nyingine. Tulichokubaliana ni kwamba kama ni Wilaya au Mkoa ametokea pale Daktari kwenda kusomea Ubingwa, anapewa mkataba maalum wa kufanya kazi na Halmashauri au Mkoa huo kwa muda wa Miaka mitano bila kuhama. Kwa hiyo, hilo likianza kutekelezwa na tumeanza kutekeleza huo mkakati ili kuzuia wasihame tena, hivyo, nafikiri hiyo itasaidia sana. Mheshimiwa Musukuma hebu uje kwangu tuone kilichotokea kwenye eneo lako ili tuone kwa yule mliyemsomesha kama tunaweza kufanya lolote. (Makofi)

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani na Mifupa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 4

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, tatizo lililopo katika Hospitali ya Mkoa wa Lindi Sokoine ni sawa kabisa na tatizo lililopo katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara Ligula, kukosekana kwa Daktari wa magonjwa ya ndani pamoja na mifupa. Je, Serikali ina kauli gani kutuletea, ingawa tunajua tunayo hospitali ya Rufaa lakini hii ni kuhusu ya Mkoa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nimemwelewa Mheshimiwa kwa sababu sijaiangalia vizuri kama ya Mtwara lakini kwa kweli wana bahati moja kwamba, wana hospitali ya Mkoa ambayo ina baadhi ya specialists lakini haijafika hata kilometa moja kutoka Hospitali ya Mkoa kuna Hospitali ya Kanda, ambayo nayo ina Mabingwa. Kwa hiyo, mimi na wewe tutakuja tuangalie specifically tatizo ni nini ili tushirikiane na Mheshimiwa Waziri tuone tunafanya nini.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani na Mifupa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 5

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, tatizo lililopo katika Hospitali ya Mkoa wa Lindi Sokoine ni sawa kabisa na tatizo lililopo katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara Ligula, kukosekana kwa Daktari wa magonjwa ya ndani pamoja na mifupa. Je, Serikali ina kauli gani kutuletea, ingawa tunajua tunayo hospitali ya Rufaa lakini hii ni kuhusu ya Mkoa?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Nimesimama ili kuwatoa hofu Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali kwa sasa ina mpango maalum wa kusomesha Madaktari Bingwa na Madaktari Bingwa Bobezi ambapo katika Mwaka huu wa Fedha wa 2022/2023 tutasomesha Madaktari Bingwa na Bobezi 139. Madaktari Bingwa na Wabobezi 136 tutawasomesha nje ya nchi. Tumeamua kuwasomesha kwa utaratibu wa set badala ya kupeleka Daktari Bingwa Mmoja wa magonjwa ya ndani inabidi awe na Muuguzi Bingwa wa masuala ya usingizi, kuwepo na mtoa huduma Bingwa wa radiology, kwa hiyo ndiyo jambo ambalo tunaenda nalo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, tuna Madaktari Bingwa 457 tunawasomesha katika pair moja moja. Kwa hiyo, niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge, kwanza tutafanya assessment, tunafahamu kuna baadhi ya hospitali za Rufaa za Mikoa zinazo idadi kubwa ya Madaktari Bingwa kuliko hospitali za pembezoni. Mheshimiwa Waziri wa Utumishi, ameshanipa kibali kama wamezidi niwahamishe ili kuwapeleka ambako kuna shida wakati tukiendelea kusubiri hawa ambao tunawasomesha.

Mheshimiwa Spika, tunatambua ni changamoto kubwa lakini ndani ya miaka miwili itakuwa ni historia chini ya mpango wa Samia Suluhu Health Super Specialization Program. Ahsante sana.