Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: - Je ni lini serikali itajenga Chuo cha Ualimu Masasi baada ya Chuo cha Ualimu Ndwika kuwa shule ya Sekondari ya Wasichana?

Supplementary Question 1

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili nyongeza. Swali la kwanza; ni lini basi Serikali itaona umuhimu katika hivyo vyuo ambavyo imepanga kujenga basi kijengwe pale Masasi kwa sababu tayari kilikuwepo na Serikali ilifanya maamuzi ya kukibadilisha chuo na kuwa shule ya sekondari ili pia ihudumie wananchi wa Masasi na wilaya za jirani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, ni lini Serikali pia itaona haja ya kufungua matawi vyuo vya elimu ya juu Wilayani Masasi ili kuweza kusaidia watu wa Masasi, lakini pia na watumishi mbalimbali kuweza kujiendeleza kielimu? Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwambe, Mbunge wa Masasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika majibu yangu ya msingi kwamba Serikali inamiliki vyuo 35 na katika vyuo hivi tuna mahitaji ya wanafunzi zaidi ya 25,000 lakini wanafunzi waliopo kwa sasa ni 22,000. Tafsiri yake hapa ni kwamba, hata hivi vyuo vilivyopo bado vina upungufu mkubwa wa kupata wanafunzi. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kufanya tathmini ya jambo hili kulingana na mahitaji, kama nilivyozungumza kwenye majibu yangu ya msingi, iwapo kama tutaona kwamba kuna uhitaji wa kujenga chuo, basi Masasi tutaipa kipaumbele katika ujenzi huo.

Mheshimiwa Spika, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika Mkoa wa Mtwara, bado tuna vyuo vitatu vya ualimu, tuna Chuo pale Mtwara Mjini, tuna vyuo viwili kimoja cha ufundi na kile cha kawaida. Vilevile katika Wilaya ya Newala tuna chuo pale Kitangale ambavyo wanafunzi hawa wote wanaweza wakatumia vyuo hivi kuweza kupata elimu yao katika maeneo hayo. Kwa hiyo, kama mahitaji yatatokea basi tutaweza kwenda kujenga katika eneo hili Masasi.

Mheshimiwa Spika, katika eneo lake la pili, kuhusiana na masuala ya matawi ya Vyuo Vikuu, naomba nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, hivi sasa Serikali inakwenda kujenga katika maeneo mbalimbali matawi ya Vyuo Vikuu. Naomba tu nitoe taarifa kwenye Bunge lako Tukufu, pale Mtwara tuna matawi ya Chuo Kikuu Huri ana Chuo Kikuu cha Stella Marius, lakini vilevile tuna tawi la Chuo cha TIAA. Vyuo hivi vyote vinaweza vikatumiwa na wenzetu wa Masasi kwa ajili ya kupata mafunzo yao pale. Vilevile Chuo Kikuu chetu cha Dar es Salaam kiko mbioni kufungua tawi katika Mkoa wa Lindi ambapo ni jirani kabisa na Wilaya ya Masasi. Nakushukuru.