Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji ambavyo havijafikiwa na huduma ya umeme katika Kata za Businde, Bugara na Kibale?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kyerwa tuna Vitongoji 670, Vitongoji ambavyo vina umeme ni vitongoji 170, vitongoji 500 vyote havina umeme sawa sawa na asilimia zaidi ya 75.

Je, nini mkakati wa Serikali wa kupelekea vitongoji vingine ambavyo havina umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la Pili; Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa Mikoa ambayo tunapata adha kutokana na umeme unaokatika mara kwa mara. Je, nini mkakati wa Serikali wa haraka kuunganisha Mkoa wa Kagera na gridi ya Taifa? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali wa kupeleka umeme katika maeneo ya vitongoji ni katika maeneo matatu. Kwanza ndiyo hii ambayo tunaifanya saa hizi ya REA III Round II, ambayo inafikisha umeme katika vijiji lakini katika vitongoji pia. Kama tulivyosema kwenye jibu la misingi Vitongoji 33 vitapata umeme.

Mheshimwa Spika, kuna mkakati wa pili ambao unafanyika wa umeme jazilizi (densification) na Mkoa wa Kagera kwenye eneo lake la Kyerwa densification katika two B na C zimo na kuanzia Januari tutaongeza wigo wa kupeleka kwenye maeneo hayo.

Mheshimwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta pesa sasa nyingi zaidi kwa ajili ya kumaliza vitongoji vyote nchini takribani kama elfu 30 na zaidi ambavyo havijapata umeme, inahitajika karibia Trilioni Sita na Bilioni Mia Tano kuweza kukamilisha eneo hili lote na jitihada za Serikali kutafuta hizo pesa zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, mwezi huu, Mheshimiwa Rais amezindua kituo cha kupooza umeme cha pale Nyakanazi ambacho ndiyo sasa kimeingiza Gridi ya Taifa katika Mkoa wa Kigoma na katika Wilaya mbili za Mkoa wa Kagera ambapo ni Ngara na Biharamulo. Jitahada za kuhakikisha kwamba Mkoa mzima wa Kagera unapata umeme kutoka katika chanzo hicho unaendelea na tayari mradi wa kuanza kupeleka umeme kutoka Benako kwenda Kyaka umeshatangazwa na Mkandarasi anatafutwa ili sasa Mkoa wa Kagera na wenyewe uweze kuingia katika Gridi ya Taifa hivi karibuni.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji ambavyo havijafikiwa na huduma ya umeme katika Kata za Businde, Bugara na Kibale?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Hai maeneo mengi yamekuwa na miundombinu ya umeme ambayo ni chakavu sana, jambo ambalo ni hatari. Katika Kata ya Uroki, Masama Kusini, Machame na maeneo mengi yamekuwa na miundombinu ambayo kwa kweli ni chakavu sana. Tuliwasilisha maombi maalum ya kupewa vifaa kwa ajili ya kufanya marekebisho.

Je, ni lini Serikali itatuletea vifaa hivi ili kutuondoa kwenye hatari ya miundombinu ambayo imekuwa chakavu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kurasimisha na kurekebisha miundombinu yake ya umeme inayowapelekea wananchi nishati hiyo. Katika Mwaka huu wa Fedha, Serikali imetenga jumla ya Shilingi Bilioni 500 kwa ajili ya kurekebisha Gridi ya Taifa katika maeneo ya umeme mkubwa pia imetenga Bilioni 300 kwa ajili ya kurekebisha miundombinu ya umeme kwenye maeneo madogo madogo ambayo tunaziita ni project mapato.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba na yeye atapata mgao huo kwa ajili ya kurekebisha miundombinu yake chakavu ili huduma hii iweze kuendelea kupatikana katika eneo lake la Hai. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji ambavyo havijafikiwa na huduma ya umeme katika Kata za Businde, Bugara na Kibale?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Mkoa wa Rukwa, Wilaya ya Sumbawanga Mjini, Kata ya Malangali, TANESCO waliweka kipooza umeme kwenye Kata hiyo.

Je, ni lini sasa Serikali itawalipa wananchi wa kule fidia? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ninaomba nikimaliza maswali nikapate eneo maalum, eneo ni eneo gani na fidia ni fidia gani ili niweze kulishughulikia na kujua kwa nini halijafanyiwa kazi kama changamoto hiyo bado ipo.