Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Wilayani Kalambo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kutenga na kuanza kujenga vyuo vya ufundi ni jambo jema, lakini ipo haja ya kuhakikisha kwamba vyuo hivi vinaanza kufanya kazi. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba vyuo vinapomalizika kujengwa na vifaa vya kufundishia vijana vinakuwa vinapatikana?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa sababu wananchi wa Kalambo wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu ujenzi wa chuo, je, ujenzi huu utaanza lini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulikamilisha au tunakamilisha ujenzi wa vyuo 25 katika wilaya 25 pamoja na vile vya mikoa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeweza kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa pamoja na samani ili vyuo hivi viweze kuanza kufanya kazi mapema iwezekanavyo. Tunatarajia kama mambo yote yatakwenda sawasawa kunako Januari vyuo vile ambavyo vitakuwa vimekamilika au tunavyokamilisha hivi sasa vitaanza kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, kwa upande wa kule Kalambo, tayari Serikali tupo katika mchakato wa kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa chuo hicho. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi, ndani ya quarter hii ya pili tutahakikisha tunapata fedha hizi ili ujenzi wa Kalambo uweze kuanza mara moja. Nakushukuru sana.