Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali langu la kwanza, Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba ina vijiji 62; na katika mpango wa Land Tenure Support Programme, vijiji 30 tu vilifanyiwa kazi: Je, ni lini Serikali inakwenda kukamilisha kazi hii ya vijiji 32 vilivyobaki?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari mara baada ya Bunge hili kuambatana nami kwenda kufanya ziara ndani ya Jimbo langu? Ahsante.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Kunambi maswali yake mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza naomba kukiri mbele ya Bunge lako kwamba kweli ule mkakati ulipofanyika mara ya kwanza, yaani ile programme ya LSTP ulipita katika vijiji 32 ndani ya Halmashauri ya Mlimba ambayo ina vijiji 62. Nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakapokuwa tumeshatenga fedha, basi tutakwenda kwa ajili ya kumalizia vijiji hivyo vilivyobakia kwa sababu programme hii ili kuwa ni kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, la pili nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge kwisha tutakwenda pamoja katika Halmashauri yake ili Kwenda kujadili siyo tu matatizo haya ya mipango ya matumizi bora ya ardhi, lakini pia na kutatua kero nyingine zinazoendelea katika maeneo ya matumizi ya ardhi. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 2

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Ni ukweli usiopingika kwamba migogoro ya ardhi imekuwa ikileta changamoto kubwa ikiwemo maafa na pia udumavu wa uchumi wa Taifa letu: Je, Serikali haioni sasa ni wakati umefika wa kuipanga ardhi kuitambua kwamba hii ni ardhi ya kilimo, hii ni ardhi ya mifugo na matumizi mengine kwa Taifa letu? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Kunti Majala, swali lake la nyongeza juu ya utaratibu wa kutambua ardhi za Tanzania. Naomba kwanza nimrudishe Mheshimiwa Mbunge katika Sheria zetu zinazoongoza usimamizi yaani Sheria Na. 4 na Sheria Na. 5 ambazo zinatambua uwepo wa mgawanyo huu ambao yeye ameusema.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hilo, pia Wizara imeendelea kufanya semina mbalimbali na elimu mbalimbali kwa wananchi ili kuweza kuwatambulisha. Pia ziko hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wanakuwa na ufahamu juu ya mgawanyiko wa maeneo ya ardhi ikiwemo kufanya hatua kubwa za kuelewesha Umma wetu kwa jumla yake. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa ni ukweli pamekuwa na migogoro mingi sana kwenye Jimbo la Kibamba kuhusiana na kutokamilika kwa urasimishaji, sasa je, Serikali ina mkakati gani kumaliza kabisa migogoro hii inayohusiana na urasilimishaji kwenye Jimbo la Kimbamba?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mtemvu kwamba kama ambavyo nimeeleza katika swali la msingi kutoka kwa Mbunge Kunambi, hatua hizo ambazo zimechukuliwa kule Mlimba ndiyo ambazo pia zinaendelea kuchukuliwa katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na kama nilivyoeleza; kuendelea kutoa elimu na kuendelea kuhakikisha Halmashauri zetu zinaendelea kusimamia mipango ya matumizi bora ya ardhi ikiwemo mipango iliyowekwa na kushirikisha wananchi katika kuweka taratibu za ardhi katika maeneo yao.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 4

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini Wizara yake itaridhia upanuzi wa Mji wa Moshi kufikia kilometa za mraba 142 ukizingatia sasa hivi tuna kilometa za mraba 58 na maombi yako ofisini kwao; na hata damp tumenunua Moshi Vijijini na makaburi yanajaa, tutahitajika tena kununua pia?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Priscus Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli maombi ya Mheshimiwa Priscus yalifika katika Ofisi zetu, lakini kama inavyofahamika mwenye mamlaka ya kuongeza maeneo ya kiutawala ni Mheshimiwa Rais. Hivyo, maombi yake tuliyapeleka katika ngazi husika na majibu yatakapokuwa yametolewa tutamjulisha Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 5

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa jicho lako kuniona. Naomba katika Halmashauri yangu ya Mkalama, Kata ya Matongo Kijiji cha Mnung’una yuko mwananchi mmoja ambaye amechukua ardhi ya wananchi karibu ekari 400; na hata baada ya matumizi bora ya ardhi ameendelea kukaidi: Naomba nimwulize Mheshimiwa Naibu Waziri kama yuko tayari kufuatana nami ili kwenda kuondoa tatizo hili ambalo ni kubwa sana kwa wananchi wangu wa Matongo?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Francis kwamba niko tayari kuongozana naye kwenda kuzungumza juu ya mgogoro huu ambao unakabili vijiji vyake katika eneo hilo la Kata ya Matongo.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatatua migogoro ya wakulima na wafugaji katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi unaohusu wananchi wa Kata ya Malula na Majengo walioko katika eneo linalozunguka uwanja wa KIA?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Pallangyo, Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutakapokuwa tumemaliza Bunge hili, nitaomba kuongozana pia na Mheshimiwa Pallangyo ili twende tukazungumze na wananchi wale tuweze kujua undani wa tatizo lenyewe na baada ya hapo tuweze kutafuta suluhu ya pamoja katika kuleta maendeleo katika maeneo yetu ya Arumeru. (Makofi)