Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantatu Mbarak Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu katika vyombo vya usafiri ikiwemo mabasi ya mwendokasi?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake. Hata hivyo, pamoja na majibu hayo mazuri pia napenda kumuuliza maswali mawili ya nyongeza.

(i) Je, ni maeneo gani mahsusi ambayo Serikali imeyazingatia katika utumiaji watu wenye ulemavu katika mabasi hayo?

(ii) Kwa kuwa mmesema mmezingatia; je, ni kwa nini hakuna utaratibu maalum ambao umezingatia watu wenye ulemavu wakati wanapofika vituoni na wanapotaka kutumia usafiri huo kwa kupanda mabasi hayo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza tukiri kwamba hapo awali miundombinu mingi ambayo ilikuwa ikijengwa ilikuwa haizingatii sana mahitaji ya watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kwenye hospitali, shule na majengo mengi. Hata hivyo, sasa imekuwa ni utaratibu wa Serikali kwamba miundombinu yote inayojengwa, iwe majengo iwe wapi lazima izingatie watu wote wenye mahitaji maalum.

Mheshimiwa Spika, kwenye masuala la usafiri; na tumetoa mfano wa mwendokasi; Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba hata ujenzi wa barabara na hasa kwenye vituo mtu yeyote mwenye mahitaji maalum, na hasa watu wenye ulemavu, yale mabasi yamejengwa na yametengenezwa kiasi kwamba yapo kwenye usawa. Kwamba anatoka anaingia, na hata kama ana Wheelchairs ana uwezo wa kuingia kwenye mabasi hayo katika vituo vyote. Lakini pia kwenye mabasi kumekuwa na nafasi na kumekuwa na viti maalum vya watu wenye mahitaji hayo; kwa maana ya watu wenye ulemavu wazee na hata wajawazito; na hata rangi ya viti imekuwa ni tofauti. Pia kumekuwa na utaratibu wa watu kuingia kwa foleni

Mheshimiwa Spika, pengine nitumie nafasi hii kusema kwamba, kunapokuwa na watu wenye ulemavu wanaposafiri wanatakiwa wawe na mstari wao na wawe wa kwanza kuingia, na viti vyao visikaliwe na watu wengine. Sasa, suala hili tunataka pia liende kwenye mabasi mengine ya umma, kwa mfano daladala na hata yanayokwenda mikoani. Ahsante. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu katika vyombo vya usafiri ikiwemo mabasi ya mwendokasi?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Kwakuwa Serikali sasa inaandaa kanuni za ujenzi, kwa maana ya Billing regulation, nini commitment ya Serikali kuhakikisha majengo yote yanayojengwa kwenye nchi yetu yanazingatia mahitaji wa watu wenye ulemavu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Kama nilivyosema kwenye maelezo yangu ya awali, kwa sasa majengo na ujenzi wowote unajengwa wa Serikali lazima uzingatie watu wenye mahitaji maalum. Na kwa suala la hizo regulation nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba lipo na linaendelea kufanyiwa kazi. Lakini hadi sasa hivi hakuna ujenzi wowote unaojengwa bila kuzingatia hayo mahitaji maalum. Ahsante (Makofi)