Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi – Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, mimi nishukuru tu kwamba majibu ni mazuri, lakini siyo majibu ya swali la msingi.

Swali la msingi linauliza ni lini barabara hii inaanza kujengwa?

Kwa hiyo swali langu mimi la kwanza la nyongeza ni lini barabara hii inaanza kujengwa? Na swali la pili ni lini barabara hii inaanza kujengwa? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante na napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Stanslaus Nyongo, Mbunge wa Maswa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la msingi ni lini Serikali itajenga barabara kutoka Sibiti hadi Salama, Sayaka, Kisamba nimejibu kwamba ili uanze kuijenga barabara lazima ifanyiwe upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, na katika hiyo barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge kuna eneo ambalo tumesema kilometa 71 ipo kwenye mpango wa EPC na tayari taratibu zimeshaanza.

Kwa hiyo, ni kwa maandalizi ya kuijenga na vipande ambavyo vimebaki kutoka Mwandoya Junction ambapo ni Goboko kwenda Kisesa hadi Itilima mkandarasi ameshapatikana kwa ajili ya kuanza kuifanyia usanifu, hayo yote ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami na baada ya kuikamilisha ndipo sasa barabara hiyo tutajua gharama za ujenzi na tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi – Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nami naomba niulize swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami inayotokea Duto kuelekea Nyashimo kupitia Shigala, Malili?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Duto - Nyashimo itajengwa tu pale ambapo fedha na bajeti itaruhusu kwa sababu tayari ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi – Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ni lini barabara ya Mnivata kwenda Masasi itajengwa ni kwa nini haijengwi wakati pesa bado ipo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote ambao barabara hii inapita Mnivata - Newala hadi Masasi yenye urefu wa kilometa 160 kwamba tayari taratibu zote zimeshakamilika kwa maana ya maandalizi ya zabuni na barabara itakuwa na loti mbili na katika ujenzi huu pia Daraja la Mwiti limeunganishwa na tayari tunachosubiri ni wenzetu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika watupe no objection kwa sababu ndiyo wanaoijenga hii barabara. Kwa hiyo, muda si mrefu barabara hii itatangazwa kwa ajili ya kuijenga yote kilometa 160. Ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi – Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi amekuwa akiniahidi sana kila mara kwamba pesa ya upembuzi yakinifu itakapopatikana barabara ya kutoka Kahama - Nyang’hwale itawekwa ndani ya mpango.

Je, ni lini pesa hiyo itapatikana na kuwekwa ndani ya mpango hiyo barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Nassor Mbunge wa Nyang’hwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tuweze kuangalia kitabu cha bajeti ili tuone. Naamini kwamba hii barabara itakuwa imetengewa fedha kwa ajili ya mpango kwa mwaka huu. Na kama kutakuwa haijatengwa basi tuangalie Wizara nini cha kufanya ili kuiwekea kwenye mpango wa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara hii. (Makofi)

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi – Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwakuwa Serikali imetangaza zabuni ya ujenzi wa barabara ya Morogoro, Njombe boda walau kwa kilometa 100 route one na route two. Je ni lini kazi hii itaanza? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ipo kwenye hatua za manunuzi. Najua Mheshimiwa Mbunge anaifuatilia; ipo kwenye hatua za manunuzi kwa ajili ya kuanza kuijenga hiyo barabara kwa hivyo ipo kwenye hatua mbalimbali za manunuzi ili iweze kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi – Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, barabara ya Kolandoto Munze Mwingunge yenye kilometa 63 imekuwepo kwenye mpango wa utekelezaji kwa maana ya ujenzi katika kiwango cha lami kwa mwaka 2021/2022. Mwaka 2021/2022 haikuweza kutekelezwa. Je, nini mpango wa Serikali kwa mwaka 2022/2023 kuhakikisha kwamba unatekelezwa? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Butondo Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kolandoto hadi Lalago kama alivyotaja hizo kilometa 62 imepewa Bajeti kwa ajili ya kuanza kujenga kwa kiwango hiki; kwa hiyo tusubiri tutakapoanza utekelezaji wa bajeti. Ahsante.