Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Swali la kwanza; kwa kuwa tunaelekea robo ya pili ya mwaka wa fedha sasa na jiografia ya Mlima Magara ni ngumu sana utekelezaji wake wakati wa mvua; je, Serikali imefikia hatua gani katika mchakato wa hiyo kilometa moja?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Barabara ya Magara – Mbulu ina jiografia ngumu kuliko sehemu yoyote nchini na hizo kilometa 44 zilizobaki zimefanyiwa usanifu tayari kwa miaka mitatu. Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mpango wake wa lami wa kilometa 44 katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kuanzia Novemba mwaka huu barabara hii itakuwa imeanza kujengwa kwa kiwango cha zege kwa sababu taratibu zote za zabuni zimeshakamilika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuanza kujenga barabara yote, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kilichokuwa kimefanyika ulikuwa ni usanifu wa awali na atakubaliana nami kwamba wakati Makamu wa Rais anafungua Daraja la Magara mwezi Machi mwaka huu aliagiza barabara ile ikamilike na Juni mwaka huu ndiyo usanifu wa kina umekamilika. Kwa hiyo Serikali inaendelea kutafuta fedha ili ijenge kilometa hizi 44 kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa kumekuwa na ucheleweshwaji mkubwa wa utoaji wa tax exemption kwa wakandarasi, sasa ni lini Wizara ya Ujenzi watakaa chini na Wizara ya Fedha ili waweke mfumo mzuri utakaorahisisha wakandarasi hawa kupewa tax exemption mapema ili waweze kujenga barabara mapema ikiwemo Barabara ya Bulyanhulu mpaka Kahama? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na maboresho mengi ya kuhakikisha kwamba malipo ya wakandarasi yanalipwa haraka na sasa hivi TRA hata mikoani wana uwezo wa kuchakata na kuharakisha malipo ya hawa wakandarasi. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea kuboresha ili kuona namna bora zaidi ya kukamilisha malipo haya ya wakandarasi kwa muda. Ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nauliza Serikali, je, ni lini itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Bigwa – Kisaki ya kilometa 78?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Bigwa – Kisaki (kilometa 78) ilishapata kibali na taratibu za kukamilisha zabuni hizo ilitangazwa, lakini itatangazwa tena kwa ajili ya kupata mkandarasi. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa kibali kilishatolewa, kwa hiyo ni taratibu tu za manunuzi ambazo zinaendelea ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya kutoka Nangurukuru mpaka Liwale inayopitia katika Majimbo ya Kilwa Kusini, Kilwa Kaskazini pamoja na Jimbo la Liwale?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Nangurukuru – Liwale ipo kwenye mpango kuijenga kwa kiwango cha lami na tayari usanifu ulishakamilika. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo kwa kuwa usanifu umeshakamilika, Serikali ipewe nafasi na fedha ikipatikana barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Dongobesh – Dareda, ni lini itajengwa kwa kwiango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K.
MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii imeshapata kibali kuanza kujengwa kwa awamu kwa kiwango cha lami kuanzia Dareda kwa kilometa zisizopungua nane. Ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Tunaishukuru Serikali kwa kuendelea na ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kidatu na hasa tunaishukuru Wizara ya Ujenzi na TANROADS kwa usimamizi wa barabara hii. Je, Serikali ina mpango gani wa uwekaji wa taa za barabarani katika Barabara hii ya Ifakara – Kidatu kama Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyoelekeza kwa zile barabara zinazopita katika vijiji?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru na kumpongeza kwa kutambua jitihada za Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inaendelea kujengwa sasa hivi kwa kasi tofauti na ilivyokuwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa barabara zote zinazojengwa na hasa kwa kiwango cha lami, pale ambapo kuna miji mikubwa na midogo taa za barabarani zinatakiwa ziwekwe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utaratibu huo upo na itakapokamilika basi awamu itakayofuata itakuwa ni kuweka taa za barabarani. Ahsante.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 7

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza; ni lini Serikali itaanza upembuzi yakinifu wa Barabara kutoka Mfumbi – Matamba – Kitulo (kilometa 51) ili iweze kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu ni ahadi ya Serikali na ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni kama barabara ya uchumi ambako tunajua kunalimwa viazi vingi sana na mazao ya mbao. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ina mpango wa kuanza kuifanyia usanifu barabara hii ili kupata thamani ama gharama ya hiyo barabara na baadaye Serikali itafute fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Supplementary Question 8

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Imekuwepo Barabara ya Makondeko – Kwembe – Kisokwa ambayo imekuwa ndani ya bajeti katika kipindi cha miaka miwili mfululizo, 2021/2022 na 2022/2023. Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mtemvu na atakubaliana nami kwamba tumefika kwenye jimbo lake. Barabara hii ni kati ya zile barabara ambazo zinapunguza msongamano katika Jiji la Dar es Salaam na ipo katika mpango wa kuanza kuijenga kwa awamu hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante.