Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya Taifa na vyeti vya kuzaliwa wananchi wa Kata za Ololosokwan, Soitsambu na Enguserosambu Ngorongoro?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, nashukuru pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwenye Kata nilizotaja za Oldonyosambu, Ololosokwan, Solosambu pamoja na Soitsambu ni kwamba kuna wananchi wengi ambao fomu zao zimezuiliwa kwenye Ofisi ya Uhamiaji.

Je, ni lini Serikali itamaliza uhakiki kwa haraka ili wananchi wapate Vitambulisho vya Taifa pamoja na vyeti vya kuzaliwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuna wananchi wengi Wilaya ya Ngorongoro hasa Kata ya Orgosorok Loliondo; wengi wao wazazi wao walizaliwa Tanganyika wamefanya kazi walikuwa watumishi na wengine wamestaafu lakini bado wanasumbuliwa hata kupata vitambulisho vya Taifa pamoja na vitambulisho vya kuzaliwa.

Je, Waziri yuko tayari kuongozana nami kwa ajili ya kutatua matatizo ya wananchi hao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Emmanuel Shangai, Mbunge wa Ngorongoro kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikianza na ombi lake la kutaka tuambatane pamoja kwenye jimbo lake kutatua changamoto hizi mbili; nimhakikishie Mheshimiwa Lekisho Shangai tutafanya hivyo. Naamini tutakapokuwa tumekwenda kwenye hiyo ziara jimboni kwake tutaweza kujua na kupata undani wa changamoto alizozungumza ili tuweze hatua stahiki ili wananchi hawa wanaostahiki haki yao ya msingi ya kupata vitambulisho waweze kupata; ikiwemo wale ambao amezungumza mara ya kwanza ambao fomu zao Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba zimezuiwa uhamiaji. Vile vile hata wale ambao amesema ni raia lakini bado wameshindwa kutambuliwa

Mheshimiwa Spikam, changamoto zote hizi mbili tutazishughulikia mimi na yeye kwa pamoja.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya Taifa na vyeti vya kuzaliwa wananchi wa Kata za Ololosokwan, Soitsambu na Enguserosambu Ngorongoro?

Supplementary Question 2

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa vitambulisho vya Taifa, kwa mfano NIDA, ni kazi kubwa kuvipata au ni janga kubwa kwa wananchi kuweza kuvipata.

Je! Mheshimiwa Waziri ataliambia Taifa au atawaambia wananchi watu ili kuweza kuvipata kwa wepesi waweze kupita njia gani ikiwa ni haki yao? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fakharia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna changamoto kidogo ya upatikanaji wa vitambulisho na changamoto hii inatokana na ukweli kwamba, tulikuwa na changamoto ya kimikataba kati ya mkandarasi ambaye alikuwa anapaswa kutoa huduma hiyo. Changamoto nyingine ilitokana na upungufu wa kadi ghafi ambazo ndizo zinatumika kuzalisha vitambulisho.

Mheshimiwa Spika, ikiwemo na changamoto ya tatu vilevile ambayo ni changamoto ya upatikanaji wa kadi ghafi zenyewe katika soko la dunia zilizosababishwa na athari za UVIKO-19. Kwa hiyo changamoto hizo ndizo zilizosababisha tukajikuta kwamba hatuna kadi za kutosha za kuzalisha vitambulisho hivi.

Mheshimiwa Spika lakini nataka nimkikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Serikali imefanya jitihada kuhakikisha changamoto zote hizi tatu zinatatuliwa. Nimani yangu kwamba changamoto za upatikanaji vitambulisho zitapungua hatua kwa hatua. Hata hivyo, nitoe wito kwa wananchi ama Waheshimiwa Wabunge kuwajulisha wananchi katika maeneo ambayo wanayasimamia na kuyaongoza, kwamba upatikanaji wa namba ya utambulisho bila kuwa na kadi unawezesha vilevile kuwafanya waweze kupata huduma mbalimbali za kijamii. Hivyo, kwa wale ambao bado wanasuburi kupata kadi zao waendelee kutumia namba za utambulisho wakati Serikali inaendelea na jitihada za kuhakikisha kwamba watanzania wote waliosajiliwa na kutambuliwa wanapata vitambulisho vya Taifa.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya Taifa na vyeti vya kuzaliwa wananchi wa Kata za Ololosokwan, Soitsambu na Enguserosambu Ngorongoro?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ndani ya Jimbo la Momba wapo baadhi ya wananchi wengi kadhaa ambao wamekosa kunufaika na Mfuko wa TASAF na zoezi la kuandikishwa kwenye mbolea kwa sababu wamekosa vitambulisha vya Taifa.

Je, ni lini Serikali itachukuwa jambo hili kwa haraka na kwa dharula ili wananchi hawa waweze kupata haki yao ya msingi kwenye mahitaji hayo? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe Mbunge wa Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na wananchi kukosa huduma mbalimbali, nilieleza katika swali la nyongeza la Mheshimiwa Fakharia kwamba namba za utambulisho zinaweza kutumika katika kupata huduma mbalimbali. Lakini kama kuna changamoto katika maeneo mahususi ambayo ameyagusia Mheshimiwa Mbunge, kwa mfano eneo hili la TASAF na sensa kama nilivyosikia sawa sawa.

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, na mbolea.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, na mbolea! Basi nilichukuwe pamoja na kukaa na Mawaziri wa sekta husika hili tuweze kulifanyia kazi kama Serikali. Lakini suluhisho la kudumu ni kuhakikisha kwamba watanzania wote wanapata vitambulisho vyao, na ndicho kipaumbele cha Serikali na tunachukuwa jitihada ili kuhakikisha hili linatekelezeka. Na kwa bahati njema katika bajeti hii ya mwaka huu wa fedha tumetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 42.5 kwa ajili ya ununuzi wa kadi ghafi milioni nane laki tano.

Mheshimiwa Spika, upatikanaji wa kadi ghafi hizo utasaidia sana kuepukana na changamoto mbalimbali ikiwemo changamoto ambazo Mheshimiwa Mbunge amezungumza.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya Taifa na vyeti vya kuzaliwa wananchi wa Kata za Ololosokwan, Soitsambu na Enguserosambu Ngorongoro?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tulipokuwa tunafanya elimu ya sensa katika Mkoa wetu wa Iringa kuna baadhi ya vijiji wana vijiji kabisa hawajui kabisa kama wanapataje namba za utambulisho, na kuna baadhi wana namba za utambulisho muda mrefu sana hawajapatiwa NIDA.

Je, ni lini sasa waliopata namba watapata na wale ambao hawajasajiliwa watapata angalau elimu wajue wanasajiliwaje?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna haja ya kuongeza jitihada za kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na huduma hii ya vitambulisho na katika kufanya hivyo kuna njia kadhaa. Njia moja ni kuhakikisha kwamba huduma hizi zinasogea karibu na wananchi. Katika kufanya jitihada hizo, Serikali imefanya kazi kubwa sana kuhakikisha inaimarisha Ofisi za NIDA katika ngazi za chini kwa maana ya Wilayani ili Maafisa hawa wa NIDA waweze kuwa karibu na wananchi na waweze kutoa huduma ikiwemo hii huduma ya Elimu kwa Umma.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza hilo, katika bajeti ya mwaka huu tunatarajia kuongeza ujenzi wa vituo zaidi 31 katika wilaya 31 nchini. Lengo ni kuhakikisha kwamba Wilaya zote katika nchi hii zinapata huduma ya NIDA ili kuwa karibu na wananchi waweze kupata huduma mbalimbali ikiwemo elimu itakayowezesha kuwasaidia kujua haki zao za msingi katika kupata kadi na vitambulisho vya NIDA kwa ujumla wake.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya Taifa na vyeti vya kuzaliwa wananchi wa Kata za Ololosokwan, Soitsambu na Enguserosambu Ngorongoro?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Kwenye taasisi nyingi za Serikali na zisizo za Serikali kuna mkanganyiko mkubwa kwamba wananchi wengi wenye namba za NIDA hawapati huduma. Naomba kauli ya Serikali leo kuhusiana na wananchi wenye Namba za NIDA ambao hawana vitambulisho na wanakosa huduma hasa kwenye mikopo. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Njau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kauli ya Serikali ni kwamba huduma za Serikali popote zilipo zinatakiwa zitolewe kwa kutambua uhalali wa namba za vitambulisho. Kwa sababu hatuwezi kumhukumu mwananchi kutokupata huduma kwa kosa ambalo siyo lake. Kama amechukua hatua zote za kisheria kuweza kujisajili, amepatiwa namba ya kitambulisho na kadi hatujampa kwa kosa ambalo siyo lake, lazima huduma yake ya msingi apate.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kauli ya Serikali ni kwamba taasisi zote zinazohusika za Serikali, kama kuna changamoto basi tutakaa tuzungumze ndani tuone, inawezekana pengine kuna baadhi ya Taasisi kulingana na masuala ya kisheria au masuala ya kimiundombinu zinashindwa kutekeleza hayo. Tutalichukua kama Serikali kwa pamoja tuzungumze tuone tunalitatua vipi maeneo ambayo bado kuna tatizo katika kukibali ama kuzipokea namba hizo za utambulisho wa wananchi. (Makofi)