Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi waliohamishiwa Halmashauri mpya Nzera?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naomba kumshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Halmashauri ya Wilaya ya Geita ni moja ya Halmashauri mpya ambazo zilianzishwa miaka michache iliyopita. Ambazo watumishi wake wengi bado wanaishi kwenye Halmashauri za zamani. Kwa kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Ardhi na NHC, imekuwa ikijenga nyumba na kukopesha watumishi na Halmashauri hiyo ina viwanja tayari vimepimwa. Ni kwa nini TAMISEMI, wasiingie mkataba na Wizara ya Ardhi, kujenga nyumba na kuirahisishia Halmashauri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Miji mingi Tanzania imekuwa ikikua lakini kwa ujenzi holela. Kwa nini Serikali kwa sababu ni sharti moja la Miji hiyo kupanda hadhi na kuwa Manispaa au Miji mikubwa isiingie utaratibu na Wizara ya Ardhi kuipima Miji yote ili kuzuia ujenzi holela ambao unaendelea? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, Mheshimiwa Constantine Kanyasu, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, kwanza kuhusu suala la Ofisi ya Rais – TAMISEMI, kuingia makubaliana na Wizara ya Ujenzi kwa ajili ya kuitumia NHC kujenga nyumba za watumishi, Serikali imekuwa ikifanya hivyo katika Halmashauri mbalimbali. NHC wamejenga nyumba na watumishi wameuziwa au wanapangishwa na wanaendelea huduma katika maeneo hayo. Kwa hiyo, tumepokea wazo la Mheshimiwa Kanyasu tutafanya utaratibu huo ili kuona uwezekano wa kujenga nyumba hizo katika Halmashauri ya Geita Vijijini lakini pia Geita Mjini baada ya kuongea na Wizara ya Ujenzi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusiana na upimaji wa Miji, Serikali ilishaweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba Mamlaka za Serikali za Mitaa zinatekeleza jukumu lao la kupima ardhi katika maeneo yao. Kwa hiyo, suala hili ni suala la msingi na jukumu la msingi la Halmashauri kazi zinaendelea, ni kweli kwamba kasi ya upimaji imekuwa ndogo na ujenzi holela umeendelea kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, naomba nichukue fursa hii kuwaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri zote kote nchini, kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao wa kupima maeneo ya ardhi katika Miji ili kuzuia ujenzi holela. (Makofi)

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi waliohamishiwa Halmashauri mpya Nzera?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imekamilisha jengo la utawala na wamehamia katika makao mapya yaliyoko Dongobeshi, lakini kuna changamoto kubwa ya nyumba za watumishi.

Je, Serikali itawejengea lini nyumba za watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu limekamilika lakini kuna changamoto ya nyumba za watumishi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeweka mpango baada ya kukamilisha jengo la watumishi sasa tutakwenda kufanya utaratibu wa kujenga nyumba za watumishi ili watumishi waishi karibu na Makao Makuu ya Halmashauri na kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi waliohamishiwa Halmashauri mpya Nzera?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Halmashauri ya Mji ya Bunda ni mpya tayari imejenga jengo la ofisi ya Halmashauri, lakini kuna changamoto kubwa sana ya nyumba za watumishi wakiwemo Walimu, Madaktari na watumishi wa halmashauri. Ni lini sasa Serikali itajenga na hasa ukisema utegemee Halmashauri ya Bunda mapato yake ni madogo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Halmashauri ya Mji wa Bunda, imejengewa jengo la halmashauri kwa maana ya jengo la utawala, lakini changamoto ya nyumba za watumishi ipo na Serikali inatambua changamoto hiyo. Nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wananchi wa Bunge Mjini kwamba wewe pamoja na Mheshimiwa Mbunge Maboto mnashirikiana vizuri kuhakikisha nyumba za watumishi zinajengwa pale na Serikali itaendelea kufanya utaratibu kuona uwezekano wa kujenga nyumba za watumishi pale.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi waliohamishiwa Halmashauri mpya Nzera?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa nyumba za walimu katika shule za msingi na sekondari Mkoa wa Simiyu.

Je, ni lini Serikali itajenga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kwamba Mkoa wa Simiyu lakini pia Mikoa yote kote nchini bado kuna changamoto ya upungufu wa nyumba za watumishi wa sekta ya afya, sekta ya elimu pia sekta na idara nyingine. Mpango wa Serikali tumeendelea kujenga nyumba za watumishi lakini safari ni hatua tunakwenda kwa awamu. Tumeendelea kujenga, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri hizo, Serikali imeelekeza kuhakikisha wanaanza kutenga fedha kwa ajili ya kujenga nyumba hizo, pia Serikali Kuu itaendelea kujenga kwa awamu. Ahsante. (Makofi)