Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa utaratibu wa biashara mpya kutakiwa kulipa kodi ya mapato kabla ya biashara kuanza?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Kama Serikali ilivyosema kwamba imetoa utaratibu mzuri wa kwamba mtu anayeanzisha biashara awe ana miezi Sita kabla ya kuanza kulipa kodi, lakini sasa katika uhalisia (in practice) mazingira hayapo hivi. Mpaka sasa bado watu wanatakiwa. Kwa sababu mtu anapoanzisha biashara inabidi kwanza apate leseni ya biashara ili apate leseni ya biashara inabidi aende akapate TIN na ili apate TIN inabidi apate TAX Clearance, sasa ili apate hiyo TAX Clearance anapewa makadirio ya kodi na analazimika alipe robo ya kwanza ya yale makadirio ya kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa analipa kabla hata ya hiyo miezi Sita ambayo amepewa kama muda ambao hatakiwi kulipa kodi. Sasa naomba kujua kwa sababu ni mwongozo na ni utaratibu ambao umetolewa na Serikali lakini kiuhalisia haupo hivyo.

Je, Serikali inatoa majibu gani kuhusiana na changamoto hii? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Zainab Athman Katimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hili tulichukue tulifanyie uchunguzi, lakini nitoe maelekezo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania kufuata Sheria, Utaratibu na Kanuni zilizowekwa na Serikali. Ahsante. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa utaratibu wa biashara mpya kutakiwa kulipa kodi ya mapato kabla ya biashara kuanza?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nyakati tofauti Serikali imekuwa ikisisitiza kutokufungia akaunti wafanyabiashara, lakini tumeendelea kupokea malalamiko wafanyabiashara wanafungiwa akaunti. Hata kama kuna changamoto za kikodi lakini kumekuwa na tatizo hilo.

Je, ni ipi kauli ya Serikali kwa TRA kuacha utaratibu wa kufungia akaunti wafanyabiashara hata kunapotokea changamoto za kikodi? Ahsante.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba kauli ya Serikali katika jambo hili ni ile kutaka mamlaka ya mapato kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na Serikali katika majukumu yao ya kila siku. Suala la kufunga akaunti bila vielelezo hili hakuna. Ahsante.