Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kufanya mapitio ya upimaji wa vijiji nchini kwa kuwa migogoro mingi imesababishwa na upimaji usio shirikishi wa mwaka 1970?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwa kweli vijiji hivi kama majibu ya msingi yanavyosema; ni kweli upimaji huu ulifanywa lakini walio wengi wanaolalamika ni kwamba upimaji haukuwa shirikishi. Kwa mfano, kuna mgogoro wa Mkutano na Kikunyungu, Kipelele, Nangumbu au Ngongowele na Ngunja. Wanachozungumza pale ni kwamba yale mawe wakati wanabeba kuna mahali walichoka wakayatunza mahali. Matokeo yake hawakurudi pale, kwa hiyo, yule aliyekuja kuchukua a-coordinate majira ya nukta akachukulia pale. Kwa hiyo, hicho ndiyo chanzo cha migogo mingi kwenye hivi vijiji ambavyo nimevitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna mgogoro kati ya Wilaya ya Kilwa na Wilaya ya Liwale kwenye Vijiji vya Nanjilinji na Milui. Mgogoro wake scenario yake inafanana na hiyo hiyo, kwamba wakati wanapima wakazi wa wilaya hizi mbili zote hawakushirikishwa. Sasa Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kufuatana nami baada ya Bunge hili twende Liwale akatatue migogoro hii?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya changamoto iliyotokea ni kweli yako baadhi ya maeneo ambayo yana changamoto hizo. Nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge tutapanga ziara twende tukakutane na wananchi wake ili kumaliza kero katika maeneo yake. Ahsante.