Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Rukwa?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini bado nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; wakati huwa tunasubiri madaktari waliokwenda kusoma lakini pia bado ile hospitali ni chakavu, na miundombinu yake imechoka; na wakati huo tuna eneo ambalo lilipimea na limefanyiwa usanifu.

Je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Rukwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili wakati huwa tuna changamoto za madaktari inalazimika wagonjwa kuwasafirisha kuwapeleka rufaa ya Mbeya.

Je, ni lini Serikali itaongeza magari kwenye hospitali ya Rufaa Mkoa wa Rukwa ikiwemo na ambulance? ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge Bupe Mwakang’ata kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza la kwamba wameshatenga eneo na kwamba ni lini Serikali itaanza ujenzi kwenye eneo jipya ambalo hospitali ya mkoa inataka kujengwa. Kwenye bajeti kwa mwaka huu imetengwa Bilioni tatu kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali hiyo, pamoja na Shilingi milioni mia tisa kwa ajili ya kufanya ukarabati kwenye eneo lile ambalo sasa hivi bado majengo yake ni chakavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kwamba sasa hivi wagonjwa wanapekekwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, kwa maana ya rufaa wanapokuwa wanashida. Umeona idadi ya madaktari bingwa waliopo kwenye hospitali yako ya Mkoa. Maana yake ni nini, wanaopeleka rufaa Mbeya ni wale ambao wanahitaji kutibia kwenye hospitali ya level ya Kanda. Lakini tanategemea kwa idadi hii ya madaktari tulionao ambao sasa hivi katika hao watano waliopo shuleni watatu watamaliza mwezi ya kumi mwakani. Maana yake ni kwamba tutaongeza idadi ya madaktari bingwa na hata rufaa nayo itapungua, ili ifikie kwamba wale wanaohitajika kanda ndio waende lakini wa level ya mkoa ibadi pale pale mkoani. Ahsante.