Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa wananchi waliovamia Msitu wa Bondo uliopo Kata ya Mswaki, Kijiji cha Mswaki?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri tu lakini nina maswali madogo mawili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hili la Bondo katika Kata ya Mswaki ni eneo muhimu sana kwa ajili ya mvua, halikadhalika kwa ajili ya mazingira. Lakini eneo hili ni la Serikali na lina GN 341 toka 1960. Swali langu je, nini mpango madhubuti na endelevu wa Serikali wa kulinda maeneo haya ili yasiweze kuvamiwa na wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; moja ya ahadi ya wenzetu wa TFS juu ya eneo hili walikuwa wajenge Kituo cha Afya lakini naipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwamba tayari tumekuwa tukipata Milioni 500 Kituo cha Afya kwenye kijiji cha Mswaki kimejengwa. Je, nini kauli ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba wako tayari sasa kutujengea bwawa kwa ajili ya kitu kinaitwa CSR? Ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi ambavyo ametoa ushirikiano kwetu kuhakikisha kwamba eneo hii tunalirudisha Serikalini, wananchi ni kweli walikuwa wamevamia eneo hili lakini kwa kutambua umuhimu wa hifadhi basi tumeanza kuwatoa hawa wavamizi na kuweka vigingi ili maeneo haya yaweze kutambulika rasmi kama ni eneo la hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango madhubuti wa Serikali ni kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo ni mazuri na ya muhimu katika kuhifadhiwa vizuri tumeendelea kutoa elimu kwa wananchi, na kwa kutambua kwamba wananchi pia ni sehemu ya uhifadhi, hivyo tumekuwa tukishirikiana na wananchi kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo tunayatambua na ni ya muhimu tunayahifadhi vizuri kwa maslahi ya Taifa. Kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge Serikali inaendelea kuhakikisha kwamba wananchi wanatambua umuhimu wa uhifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala lingine ambalo amelisema la Kituo cha Afya, ni kweli Serikali iliwahi kuahidi kuwajengea Kituo cha Afya katika Wilaya ya Kilindi katika Kijiji cha Mswaki na kwa bahati nzuri Serikali imetimiza ahadi hiyo. Kwa kuwa, tumekuwa tukitoa CSR katika maeneo mbalimbali ambayo yanazunguka maeneo yaliyohifadhiwa Mheshimiwa Mbunge nimuombe tulichukue ombi lake tuende tukachakate na hatimay tutampa majibu yaliyo sahihi lakini tuwahakikishie wananchi wa Kilindi na Mswaki kwamba tutahakikisha wanapata CSR kama moja ya wajibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii. (Makofi)