Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya utafiti wa chanzo cha watoto wachanga kugeuka njano baada ya kuzaliwa na Mama kuishiwa nguvu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Ninamshukuru kwanza majibu ya Mheshimiwa Waziri lakini changamoto kubwa kuna baadhi ya Vijiji, Kata hakuna hospitali wala vipimo, sasa sijui anawasaidiaje wazazi ambao wanazaa watoto wachanga ambao wapo katika vijiji ambavyo hakuna hata hospitali yenye vipimo kama hivyo?

Swali langu la pili, kuna watoto ambao wanazaliwa na sickle cell wamekuwa wakipata mateso makubwa sana, damu kupungua mwilini, lakini sasa hivi tunaona kwamba hatupatiwi dawa bure katika hospitali zetu. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wanawasaidia watoto wanaozaliwa na sickle cell?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo.

Moja ni suala la kwamba kuna watoto ambao vituo haviko kule, ndiyo maana kuna juhudi kubwa ambayo Rais wetu anafanya kwenye masuala ya kujenga vituo vya afya kila mahali katika nchi yetu na ndiyo maana pia tunasisitiza kila mama mjamzito aweze kujifungulia kwenye zahanati au kituo cha afya ili utambuzi uweze kufanyika na kumpa mtoto tiba stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili linalohusu suala la selimundu maana yake sickle cell ni kweli kuna tatizo hilo katika nchi, lakini imeshachukuliwa hatua sasa na dawa ya kuweza kuwasaidia hawa watoto imeshawekwa package yake kwa ajili ya kununuliwa na MSD na kusambaza kwenye vituo vyetu na kuweka utaratibu maalum, kwa kushirikiana vilevile na Serikali ya Marekani tayari vilevile imetengenezwa program maalum ambayo inashughulikia watoto wenye matatizo hayo. Ahsante sana.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya utafiti wa chanzo cha watoto wachanga kugeuka njano baada ya kuzaliwa na Mama kuishiwa nguvu?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, tafiti zimefanyika Kitaifa, Je, ni maeneo gani ambayo yanaonyesha baada ya kufanya tafiti kwamba zoezi hili liko kwa wingi nchini? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi tunachoweza kumwambia Mheshimiwa Mbunge ni kwamba katika kila watoto 20 mmoja anakutwa na tatizo hilo, maeneo yote ya nchi wamekuwa wapatikana watoto kama hao kwa sababu matatizo mengine yanatokana na maambukizi au wakati mwingine inaweza kuwa mama ana damu aina fulani na mtoto ana damu aina fulani ambayo wakati mwingine ikichanganyikana inasababisha tatizo hilo. Wakati mwingine inatokana kwamba wakati mtoto yuko tumboni kwa mama anakuwa na damu nyingi, chembechembe nyekundu nyingi za damu, kwa sababu tumboni kwa mama anatumia hewa oxygen ambayo ni ile ya mama, kwa hiyo ni lazima awe na chembe chembe nyingi za damu.

Kwa hiyo, akitoka nje akizaliwa baada ya saa 24 zile chembechembe nyekundu zinaanza kuondoka kwa maana ya kupasuka zinapoanza kuondoka sasa inasababisha hilo tatizo lakini ni la kawaida kwa sababu anapofika sehemu yenye oxygen nyingi basi chembe chembe zile nyekundu hazihitajiki inabidi ziondoke. Hivyo ni kwamba, kila mahali hilo tatizo linaonekana, jambo la msingi ni kujua katika kila watoto 20 mmoja anaonekana ana hilo tatizo.(Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya utafiti wa chanzo cha watoto wachanga kugeuka njano baada ya kuzaliwa na Mama kuishiwa nguvu?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti mbalimbali na majarida mbalimbali yanaonyesha bado vifo vinavyotokana na uzazi vinazidi kuongezeka. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba inapunguza vifo hivyo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba vifo vinavyotokana na wazazi vipo lakini vinapungua kwa kila wakati. Suala zima la mkakati wa kuendelea kupunguza zaidi ndiyo maana umeona Rais wetu ameelekeza tutumie shilingi bilioni 23 kujenga wodi maalum kwa ajili ya watoto njiti, kwa sababu vifo vya watoto wachanga vinachangiwa asilimia 48 na watoto njiti wanaozaliwa.

Vilevile kwenye suala la akinamama ukiona tunasogeza vituo sana, kumekuwepo na tozo kwa ajili ya kuchangisha kuhakikisha tunajenga vituo kule sehemu ambazo hakuna vituo vya afya ni kuhakikisha wale akinamama ambao wanashindwa kujifungua, basi vituo vinavyoweza kufanya huduma ya dharura na kuokoa maisha ya akinamama vinapatikana hivyo ukiona hela nyingi zinaelekezwa kwenye vituo vya afya, zahanati lakini kwenye kuboresha huduma za afya dawa, ndiyo hatua ambazo zinatumika kuhakikisha tunapunguza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie kwenye nchi yetu vifo vya akinamama na watoto vinaendelea kupungua. Ahsante.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya utafiti wa chanzo cha watoto wachanga kugeuka njano baada ya kuzaliwa na Mama kuishiwa nguvu?

Supplementary Question 4

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ninashukuru sana kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutujengea jengo kubwa sana la zaidi ya bilioni 11 pale Mkoani Mbeya hospitali ya Meta.

Mheshimiwa Rais alizindua jengo hilo pindi alipofika mkoa wa Mbeya, hali imekuwa mbaya sana wanawake bado wanatumia jengo la zamani kujifungulia. Ni lini Serikali italeta vifaa hata angalau vitanda 100 ili wakinamama wanusurike kulala wanne wanne kwenye wodi ya zamani? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Rais wetu alikwenda akafungua jengo kubwa sana la akinamama pale Mbeya Meta, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Mkoa wa Mbeya ni kati ya Mikoa yenye hali nzuri sana ya afya ukilinganisha na sehemu zingine. Kwa maana ya kwamba ukiangalia hospitali ya Mkoa kuna ujenzi mkubwa sana unafanyika wa zaidi ya bilioni 21 na unaujua, pia ukienda kwenye hospitali ya Rufaa pale umeona jengo lililojengwa. Rais wetu alipoondoka alielekeza kwamba shilingi bilioni 2.1 zielekezwe pale kwa ajili ya kuhakikisha jengo hilo linawekwa vifaa na tayari vifaa vimenunuliwa kwa hiyo ndani ya miezi miwili zitakuwa zimefikishwa pale na kufanyia kazi. (Makofi)