Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itabadili utaratibu kuwataka wavuvi wanaotumia ring net kutoruhusiwa kuvua mchana na kuvua chini ya mita 50?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, huoni kwamba kuvua samaki usiku wakiwa wamelala unaweza ukavua samaki hata wale ambao hawajalengwa? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, ni lini Serikali itabadilisha au itafanya marekebisho ya kanuni ya mwaka 2020, kipengele cha 66(b)(b), 66(f)(f), 66(g)(g) na kipengele 128(1) ambacho kina faini ambayo haitekelezeki kwa wavuvi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naomba nitoe ufafanuzi katika suala hili la kuvua samaki usiku. Kuvua samaki usiku kuna uwezekano wa samaki wale wadogo kuwa karibu zaidi ya kina 50 kuliko wale samaki wakubwa, lakini pia uvuvi wa kutumia ring net unasababisha kuchukua mazalia ya samaki pamoja na mayai ambayo yanaweza yakaondoa uvuvi endelevu katika mazalia ya samaki na hivyo kufanya maeneo haya yasiwe endelevu kiuchumi na kiuvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye suala la lini Serikali itabadili kanuni; mchakato wa kanuni hizi unaendelea, hivyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Bunge, muda ukifika zitakuja kwenye kamati husika na kanuni hizi zitafanyiwa marekebisho, ahsante.

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itabadili utaratibu kuwataka wavuvi wanaotumia ring net kutoruhusiwa kuvua mchana na kuvua chini ya mita 50?

Supplementary Question 2

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali imefikia wapi katika kuwasaidia wavuvi ili waweze kupata vifaa vya kisasa na waweze kuvua uvuvi wenye tija?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na zana bora za uvuvi, na kwa mwaka huu wa fedha tayari wavuvi wameshapata taarifa na wameshaanza kufanya maombi na zana hizi watakazopewa zitakuwa hazina riba, watapewa mikopo ambayo haina riba ili kufanya uvuvi uwe ni uvuvi endelevu na wa kisasa, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itabadili utaratibu kuwataka wavuvi wanaotumia ring net kutoruhusiwa kuvua mchana na kuvua chini ya mita 50?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Mheshimiwa Waziri kuhusiana na uvuvi wa mita 50 yanaenda kinyume kabisa na uhalisia katika maeneo yote ya ukanda wa pwani. Wavuvi wetu wa Mtwara, Lindi, Pwani, Kilwa, Tanga ni wavuvi wa kawaida ambao hawana uwezo wa kuvua kina cha mita 50 ambayo ni bahari kuu. Katika mabadiliko ya kanuni yanayokuja, Serikali iko tayari kuondoa kikwazo hiki cha uvuvi wa mita 50?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tulipokee wazo lake na tutalifikisha kwa wataalamu, watalichakata na majibu yatatoka katika Bunge lako tukufu.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itabadili utaratibu kuwataka wavuvi wanaotumia ring net kutoruhusiwa kuvua mchana na kuvua chini ya mita 50?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kanuni hizi ambazo zinaandaliwa, Ziwa Tanganyika tuna-share zaidi ya nchi moja, lakini nchi nyingine kwenye ziwa hilo hilo wanavua mchana. Hamuoni kama zuwio hilo linawapa umasikini wavuvi wa nchi yetu na mbadilishe ili waendelee kunufaika na Taifa letu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba Waheshimiwa Wabunge watambue kwamba rasilimali za uvuvi ni rasilimali za muhimu sana ambazo zinahitaji kuwa na uvuvi endelevu. Kwanza Serikali inafanya kuyalinda maeneo haya, kuyasimamia vizuri, lakini pia kuyahifadhi ili kuwepo na uvuvi endelevu. Hivyo tunavyoelekeza namna ya kutumia uvuvi wa kisasa na ni uvuvi endelevu kwa kuyafanya mazalia ya samaki yaendelee kuwa endelevu wananchi wanapaswa kufuata taratibu na sheria zilizopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hii ina lengo la kuhakikisha kwamba, tunalinda maeneo haya ili tuwe na uvuvi endelevu, tunapoyamaliza haya mazalia ya samaki tutahakikisha uvuvi usiwepo kabisa hapa nchini. Kwa hiyo, tunaendelea kuwaomba wananchi waendelee kufuata sheria zilizopo ili kufanya uvuvi uwe uvuvi endelevu.