Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitumie fursa hii kuishukuru sana Serikali kwa ajili ya kuingiza Wilaya ya Manyoni katika mpango wa kujenga Chuo cha VETA mwaka huu, lakini ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa tuna vijana wengi wanamaliza kidato cha nne hawaendelei kidato cha tano na vijana wengi wanamaliza kidato cha tano na sita hawaendelei vyuoni; je, nini mpango wa Serikali kuifanya elimu ya ufundi kuwa basic education yaani elimu ya msingi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa sasa hivi tuna uhitaji mkubwa sana wa elimu ya ufundi hasa hasa kwa ajili ya uzalishaji viwandani; nini mpango wa Serikali na Wizara kutoa mikopo kwa vijana ambao wanaenda kusoma elimu ya ufundi? Ahsante sana.

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Chaya, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Serikali inakusudia kama nilivyosema kujenga vyuo vya ufundi katika Wilaya zote hapa nchini na sasa hivi zimebaki wilaya hizo 62. Kwa hiyo, ujenzi utaendelea na kuhakikisha kwamba vyote vinafanya kazi kwa ajili ya wanafunzi kuweza kusoma humo.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwa sababu sasa hivi tunapitia mitaala na kazi mojawapo kubwa ya kupitia mitaala ni kuongeza elimu ya ujuzi, ujuzi ikiwa ni pamoja na ufundi, tunaamini tutakapokamilisha kazi hii rasimu zitakamilika mwisho wa mwaka huu maamuzi mwakani, tunaamini kwamba tutakuja na mkakati ambao utaongeza mafunzo ya ufundi na ujuzi katika shule zetu kuanzia darasa la kwanza kwenda mpaka elimu ya kidato cha sita.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la pili kuhusu mikopo. Kwa sasa hivi kwa kweli Serikali haitoi mikopo kwa ajili ya kwenda kwenye vyuo vya VETA, lakini tumefanya mazungumzo na Benki ya NMB kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaweza tukatoa mikopo kwa wale ambao wana miamala inayopitia kwenye benki hiyo kwa ajili ya kusaidia wanafunzi kusoma kwenye vyuo vyote ikiwa ni pamoja na vyuo vya ufundi.

Kwa hiyo, tunaamini kwamba itasaidia kupunguza adha ya wanafunzi kutopata mkopo lakini tutaendelea kutafuta mikakati mizuri zaidi kuhakikisha kwamba tunatoa fursa ya mikopo.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 2

MHE. BENEYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi. Wilaya ya Mbinga hatuna Chuo cha VETA na tulipata ahadi ya Serikali kwamba awamu hii tutaingia kwenye mpango wa kujengewa Chuo cha VETA, tayari tuna eneo. Ni lini sasa chou hiki kinaenda kuanza kujengwa?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kapinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema Wilaya zote ambazo hazina Vyuo vya VETA tunaanza kujenga VETA mwaka huu tumekubaliana kwenye hizo bilioni 100 ambazo tumezipata kutoka Hazina tutaanza ujenzi mwaka huu na mwakani tutapata bilioni 100 nyingine na kumalizia ujenzi. Kwa hiyo, tutafanya hivyo pamoja na Wilaya ya Mbinga na ujenzi utaanza siku za karibuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, wito wangu kwa Wabunge wote ni kwamba kuhakikisha tunapata maeneo mapema, tunapata hati miliki ili tuweze kujenga kwa sababu hatuwezi kwenda kujenga chou mahali ambapo hatumiliki ardhi chini ya utaratibu wa VETA. (Makofi)