Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

Kuwawezesha Wananchi Kupata Umeme wa Bei Nafuu MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Licha ya Serikali kupeleka umeme vijijini kwa kasi kupitia mradi wa REA, bado kuna changamoto za kuunganisha umeme kwa wananchi. (a) Je, Serikali ina mpango gani kuwawezesha wananchi kupata umeme kwa bei nafuu? (b) Nguzo za umeme zinasimikwa kwenye njia kuu tu; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha nguzo hizi zinapelekwa kwenye vitongoji?

Supplementary Question 1

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la umeme hasa kwenye uunganishaji limekuwa ni tatizo kubwa hasa kwenye maeneo ya mita. Wananchi wengi na wateja wengi wamekuwa wakilalamika kwamba mita ambazo wanafungiwa zinaharibika baada ya muda mfupi. Ningependa kujua kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba je, analifahamu hili na kama analifahamu, hatua gani zitachukuliwa, ili kuhakikisha kwamba, utaratibu huu mbovu unasitishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Jimbo la Kalenga limekuwa lina changamoto kubwa katika masuala haya ya umeme na nina vijiji kadhaa ambavyo mpaka dakika hii viko gizani na vinahitaji umeme. Kijiji cha Lupalama katika Kata ya Nzii, Kijiji cha Kipera, Kijiji cha Itagutwa, Kijiji cha Magunga na Lyamgungwe; ningependa kusikia commitment ya Mheshimiwa Waziri, je, ana utaratibu gani na mpango gani kuhakikisha kwamba, vijiji hivi vinapata umeme? Na kama je, yuko tayari kuungana na mimi kwenda moja kwa moja Kalenga ili kuweza kuwapa hamasa wananchi wangu? Nashukuru.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, wakati REA wanapofunga umeme ni mara nyingi sana imekuwa ikitokea kwamba zile mita inaonekana kama hazina nguvu, tatizo siyo kwamba mita ni mbovu, tatizo tu ni kwamba umeme unaokuja ni wa low voltage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge ni vizuri tukawaeleza baada ya REA kuunganisha umeme sasa, umeme tunaotumia ni wa low voltage ambao ni kilovolt 30 na mwingine 11 zaidi ni 132. Kuanzia Julai mwaka huu kuna mradi sasa wa kuongeza nguvu za umeme ambao ni kilovolt 400 utapita kwenye maeneo ambayo tuliyataja. Kilovolt 400 zitakapoingia na kuanza matatizo ya kukatika kwa umeme kwenye tatizo la mita yatakoma mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vijiji alivyotaja Mheshimiwa Mgimwa, vijiji vitano vya Lupalama, Lupelo, Magunga na vingine ni kweli kabisa havijapata umeme na tulishavitembelea, kwa sasa tumezungumza na Mheshimiwa Mgimwa, kati ya vijiji vitakavyoanza kupatiwa umeme kwenye Jimbo lake tutaanza na hivi vijiji vitano ambavyo Mheshimiwa Mgimwa amevitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ameomba sana tupate fursa ya kutembelea kule mimi pamoja na Mheshimiwa Waziri tumekuwa tukitembelea sana maeneo ya Morogoro, hata hivyo, bado tumhakikishie baada ya Bunge lako Tukufu kuisha mimi na Mheshimiwa Mbunge bado tutakwenda kutembelea zaidi, hata akisema mara tano bado tutakwenda kuhakikisha wananchi wanapata umeme.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

Kuwawezesha Wananchi Kupata Umeme wa Bei Nafuu MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Licha ya Serikali kupeleka umeme vijijini kwa kasi kupitia mradi wa REA, bado kuna changamoto za kuunganisha umeme kwa wananchi. (a) Je, Serikali ina mpango gani kuwawezesha wananchi kupata umeme kwa bei nafuu? (b) Nguzo za umeme zinasimikwa kwenye njia kuu tu; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha nguzo hizi zinapelekwa kwenye vitongoji?

Supplementary Question 2

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu linaelekea kwa Naibu Waziri. Katika mikoa ya Mtwara na Lindi tuna tatizo kubwa sana la usambazaji wa umeme kwa kuwa haikuwahi kupata Phase I ya REA wala fedha za MCC. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akalithibitishia Bunge hili kwamba, katika awamu hii ya tatu ya REA vijiji vyote vitapewa umuhimu wa kupewa umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, ni kweli kabisa Mtwara na Lindi yamekuwa ni maeneo ambayo kwa miaka mingi hayapati umeme, lakini baada ya ugunduzi wa gesi miaka miwili iliyopita, kati ya maeneo ambayo tuliyapa vipaumbele kuyapatia umeme wa gharama nafuu ni pamoja na Mtwara na Lindi. Hii ni kwa sababu tulianza sasa kutumia umeme wa gesi kwa mikoa yote hiyo miwili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie tu kwa mikoa hii miwili tuliwatengea kisima ambacho kwa ujumla wake kinapata megawatt 18 za umeme wa gesi. Kwa hiyo, watu wa Mtwara na Lindi wanaweza kupata umeme na tena wa gharama nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo kwenye REA Awamu ya Tatu inayokuja kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, tutahakikisha kwamba vijiji vyote vya Mtwara na Lindi ambavyo vimebaki kutopata umeme kwenye REA Awamu ya Kwanza kwa sababu haikuwepo na Awamu ya Pili ambayo imekwenda kwa kiwango kidogo sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahakikisha vijiji vyote vya Mtwara na Lindi ambavyo vimeingia kwenye mpango huu wa REA Awamu ya Tatu vitapata umeme wa uhakika.