Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaifanya elimu ya sekondari kuwa ya lazima?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, kwa kuwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameonesha nia na dhamira ya dhati ya kumlinda mtoto wa kike, kwa kuweka elimu bila malipo kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha sita. Kwa nini sasa Wizara isitoe waraka wa kulinda watoto hawa dhidi ya mimba za utotoni na ndoa za utotoni ili kuwahimiza kuwa shuleni wakati tunasubiri mabadiliko makubwa ya sera?

Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali isitoe kauli dhidi ya watoto walioko mtaani wanaokosa kwenda shuleni ambao wamejiingiza kwenye makundi ya vilevi na uhalifu kama panya road? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Husna Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba sasa Serikali tunafanya mapitio ya Sera pamoja na Sheria yetu ya Elimu. Nimeeleza hapa kwamba rasimu hiyo itakuwa tayari mwezi wa Desemba, 2022. Hata hivyo, uandaaji wa miongozo anayozungumza Mheshimiwa Mbunge pamoja na nyaraka mbalimbali zinategemea vilevile mwongozo kutoka kwenye sera hii. Kwa hiyo namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, kwa vile Desemba sio mbali tutakamilisha rasimu hii na huenda hayo yote anayoyazungumza yakawemo kwenye sera pamoja na sheria yetu.

Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili mwaka jana, 2021, Serikali ilishatoa Waraka Na.2 wa Elimu wa mwaka 2021 ambao unahusu namna gani wanafunzi walioacha shule kwa sababu mbalimbali ikiwemo na hii ya ujauzito wanaweza kurudi shuleni. Kwa hiyo tutoe wito tu na rai kwa wadau pamoja na mamlaka mbalimbali zinazosimamia elimu kuhakikisha kwamba tunakwenda kutekeleza maagizo haya ya Serikali. Nakushukuru sana.