Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Bungu Wilayani Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kama alivyosema, kituo hiki ni kikongwe, hakuna ufinyu wa eneo. Kwa kuwa kutoka kituo hiki mpaka kituo kingine cha hadhi kama hii ni kilomita 50: Serikali haioni sasa ni vizuri kwa dharura ikawaonea huruma watu wa Bungu, angalau kuwajengea jengo la upasuaji au jengo la mama na mtoto ili kuwasaidia wananchi hasa akina mama na watoto? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wakati tukiwa tunasubiri hizo fedha na taratibu nyingine zote zikamilike, wananchi hawa wanateseka: Ni lini Serikali itapeleka gari la uhakika la wagonjwa ili kuwasaidia wananchi wa Bungu, kutoka Bungu kwenda mpaka Korogwe Mjini kilomita 50 kupata matibabu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo hiki cha Afya cha Bungu kiko katika eneo lenye ukubwa wa ekari mbili, lakini standards zetu za vituo vya afya ni angalau ekari kumi na Serikali imefanya tathmini kwa aina ya uchakavu mkubwa wa kituo kile cha afya, haitakuwa na tija kuweka fedha za kukarabati kituo kile. Ni vema kujenga kituo cha afya ambacho kitaendana na ramani za kisasa. Bahati nzuri kituo hicho kinajenga ndani ya Kijiji kile kile cha Bungu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimtoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo cha afya kitajenga katika kijiji kile na Halmashauri itaanza kutenga fedha katika mwaka ujao wa fedha mpaka kitakapokamilika.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kununua magari ya wagonjwa. Niwahakikishie Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe pia itapelekewa gari la wagonjwa ndani ya mwezi ujao. Ahsante.