Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je ni lini Serikali itakabidhi majengo yaliyokuwa ya Hospitali ya Muhimbili kwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ili kupunguza uhaba wa majengo katika Hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini majengo yale ni zaidi ya miaka 10 sasa yamekaa hayana matumizi yo yote. Swali la kwanza; je, MUHAS lini wanaanza huo upanuzi wao wa hayo maeneo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa nini wasiwaazime Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo yale majengo yakatumika kwa Hospitali ya Wilaya ili mradi majengo yale yapate kutumika, yasiendelee kuharibika? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo anawakilisha wananchi wa Bagamoyo. Ameuliza swali ni lini wataanza kufanya upanuzi na kuyatumia, nafikiri yanatumika wakati wote lakini nitakwenda tutembelee mimi na yeye na tuweze kuwasiliana na utawala wa MUHAS ili tuweke mkakati mzuri wa kuhakikisha wanashirikiana ofisi ya Mbunge na wananchi wa Bagamoyo na Chuo cha MUHAS.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ninachoweza kumwambia ndugu yangu ni kwamba, kikubwa kwa wananchi wa Bagamoyo, Chuo Kikuu kila Mbunge hapa angetamani Chuo Kikuu kiwepo ndani ya Jimbo lake. Chuo Kikuu kuwepo ndani ya Jimbo lako ni fursa kubwa sana. Kwa hiyo, kikubwa mimi na yeye tutakachokifanya ni kujenga uhusiano na Hospitali ya Wilaya na Chuo Kikuu cha MUHAS ili waweze kushirikiana na kufanya kazi pamoja na kufufua yale majengo ili hospitali ya Mheshimiwa iweze kupanuka, lakini manufaa ya watumishi yapatikane. Kwa upande wa hospitali ya wilaya lakini manufaa yanayotokana na Chuo Kikuu yapatikane kwa watu wa Bagamoyo. Tutakwenda kusisita umuhimu wa mahusiano. Ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je ni lini Serikali itakabidhi majengo yaliyokuwa ya Hospitali ya Muhimbili kwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ili kupunguza uhaba wa majengo katika Hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Singida Mjini hatuna Hospitali ya Wilaya na ipo ahadi ya Serikali ya kukabidhi majengo ya Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa Hospitali ya Wilaya. Sasa nataka kujua ni lini ahadi hii itatekelezwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge, swali lake, kama lifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza alivyo na taarifa na tulivyotembelea mimi na yeye kwenye hospitali yake ya mkoa juzi, tumeona majengo ambayo yanajengwa hospitali mpya ya Mkoa wa Singida. Siyo muda mrefu mpaka mwezi Julai majengo yale yanakwenda kukamilika na hospitali ya mkoa itaondolewa kwenye eneo iliyokuwepo halafu na kuwaachia wilaya hiyo iendelee kutumia hospitali iliyoko pale. (Makofi)

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je ni lini Serikali itakabidhi majengo yaliyokuwa ya Hospitali ya Muhimbili kwa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ili kupunguza uhaba wa majengo katika Hospitali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kuuliza Chuo cha MUHAS kimedahili wanafunzi wengi sana kiasi kwamba wanafundishwa somo hilo hilo kwa session mbili kwa siku. Je, Serikali inaonaje sasa ikachukua hatua ya haraka sana kuhakikisha kwamba haya majengo ambayo yanamilikiwa na Serikali yakatumika haraka ili wanafunzi wakayatumia ili kuweza kupunguza hiyo changamoto?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nahato, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niseme kwamba ndiyo maana nikamwambia Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza swali la msingi uwepo wa majengo yale kule Bagamoyo ni fursa kwake; na sababu mojawapo ni hilo analolisema Mheshimiwa Mbunge kwamba wanafunzi sasa wamerundikana pale Muhimbili na somo lilelile linaingia darasa hilo hilo mara mbili na wanafunzi wa session tofauti, lakini darasa lilelile.

Kwa hiyo, kimsingi tutakwenda kufanya haraka na tutakwenda kushauriana kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023, fedha ziweze kuwekwa kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu ili kuweza kukarabati majengo yaliyopo Bagamoyo na haya Mlonganzila iweze kutumika ili wanafunzi wa MUHAS waweze kufundishwa kwa wakati mmoja.