Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya eneo la Nsemulwa na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa muda huu wa maswali madogo mawili ya nyongeza. Ninaishukuru sana Serikali kwa fedha hizo zilizotolewa, na hivi karibuni tulipata milioni 300, nasema ahsante kwa Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa maana ya Mwamkulu fedha zilizotolewa zina uwezo wa kujenga OPD. Ni lini Serikali itatuongeza fedha ili tuweze kumalizia majengo mengine?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kituo cha Afya cha Ilembo kilibahatika kupata fedha shilingi milioni 400, lakini fedha zile hazikulenga vifaa tiba. Ni lini Serikali itatusaidia fedha ili tuweze kununua vifaa tiba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nipokee shukrani nyingi za Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi wa Manispaa ya Mpanda ambazo amezielekeza kwa Serikali yetu inayochapa kazi, chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan. Na ni kweli, hakuna jimbo ambalo halijapata vituo vya afya na zahanati. Kazi inaendelea na tunaona wananchi wetu wananufaika na miradi hii ya afya.

Mheshimiwa Spika, Kituo hiki cha Afya cha Mwamkulu kimepewa milioni 250, na maelekezo ni kujenga majengo matatu. Jengo la OPD, maabara pamoja na kichomea taka. Kwa hiyo milioni 250 si ya kujenga OPD peke yake, na hiyo ni standard kwa milioni 250 zilizotolewa nchini kote. Awamu ya pili tutapeleka fedha tena kwa ajili ya kikamilisha majengo yaliyobaki yakiwemo wodi, majengo ya upasuaji na majengo mengine muhimu.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la vifaa, Serikali imeweka utarartibu, kuanza baada ya kukamilisha miundombinu hiyo, kwa awamu tutapeleka fedha kwa ajili ya kununua vifaa tiba ili kuwezesha vituo vyetu kufanya kazi vizuri zaidi. Ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya eneo la Nsemulwa na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mwaka 2017/2018 Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuwa anazindua Siku ya Ushiriki wa Afya Duniani katika Jimbo la Ushetu katika Halmashauri ya Ushetu, Kata ya Ulowa, aliwaaahidi wananchi kuwajengea kituo cha afya, lakini hadi leo ni miaka mitano kituo hicho hakijaanza kujengwa.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Kituo Cha Afya kwa wananchi wa Ulowa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Cherehani, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ahadi zote za viongozi wetu wa Kitaifa ni kipaumbele katika utekelezaji, kikiwepo Kituo cha Afya katika Kata ya Ulowa. Kwa hiyo, ninaomba nimhakikishie kwamba Serikali imechukua mahitaji na ahadi hii, na tunatafuta fedha, wakati wowote kupitia fedha za tozo tutaleta pale milioni 250 ili Kituo cha Afya cha Ulowa kianze kujengwa. Ahsante.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya eneo la Nsemulwa na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 3

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ninaomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pale Moshi Mjini, kwa sababu ilishapitishwa kwenye bajeti na wengine wameshapata?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Priscus Tarimo Mbunge, wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka huu wa fedha Serikali imetenga shilingi bilioni 14 kwa ajili ya hospitali za halmashauri 28 katika hamashauri ambazo hazina kabisa hospitali za halmashauri ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Moshi. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba ndani ya mwaka huu wa fedha lengo la Serikali ni kuleta fedha hiyo, milioni 500, ili kazi ya ujenzi iweze kuanza. Ahsante.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya eneo la Nsemulwa na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 4

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba imeanza ujenzi wa Kituo cha Afya kwa mapato ya ndani, na jengo la la wagonjwa wa nje (OPD) limekamilika. Sasa ni nini mpango wa Serikali kuisaidia halmashauri hiyo kukamilisha majengo yaliyobaki? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godwin Kunambi, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa ujenzi wa vituo vya afya unahusisha nguvu za wananchi katika michango yao na kujenga vituo hivyo. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kwanza kuwapongeza sana wananchi wa Jimbo hili la Mlimba, ambako Mheshimiwa Kunambi ndiye Mbunge, kwa kazi nzuri na kubwa ambayo wameifanya ya kujenga kituo cha afya. Nimhakikishie, kwa awamu tutatafuta fedha ili kuhakikisha kwamba tunakamilisha miundombinu ambayo inabaki.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.