Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini Mtambo wa matangazo ya TBC Taifa na TBC FM utafungwa katika Mji wa Itigi ili Wananchi wapate matangazo hayo muhimu?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi hii, lakini nisikitike swali nimeulizia Itigi lakini wamejibiwa watu wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeuliza usikivu wa Itigi kwa sababu maalum, sisi Itigi hatusikii kabisa redio, ni kwa sababu redio Mwangaza waliweka mnara wao pale mtambo, kwa hivyo redio nyengine hazisikiki kabisa ikiwemo TBC, na swali hili ni mara ya 3 nauliza ndani ya Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niulize Mheshimiwa Waziri aniambie Manyoni ni sehemu ya Itigi, Manyoni wanasikia TBC, Itigi hatusikii kabisa, sasa huo mtambo mtakaoufunga mwakani huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi kweli mnatuahirishia miaka yote hii, Mheshimiwa Nape yupo hapa ulipokuwa Waziri wa Habari ulijibu swali hili ukatuambia mtatusaidia kutufungia mtambo pale sasa leo tunajibiwa tu watafunga na Manyoni na Ngara na wapi, hebu naomba comitment ya Serikali, sisi Itigi hatusikii kabisa redio, wananchi wetu hawana pesa ya kununua tv, hata Mheshimiwa Rais akihutumia hawamsikii kupitia viredio vyao.

Sasa ni lini mtatufungia kamtambo hako? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare Mbunge wa Manyoni Magharibi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya matangazo ya TBC, changamoto ni mbili ya kwanza ni uhafifu wa usikivu na pili inawezekana usikivu haupo kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa changamoto ya Manyoni kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi, nimesema kwamba katika mwaka wa fedha ujao kuna Wilaya 14 ambapo Manyoni ikiwa moja ya Wilaya ambazo zinakwenda kutatuliwa changamoto za usikuvu wa mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile nafahamu kabisa kwamba changamoto hii imekuwa ya muda mrefu lakini ni lazima pia tutume wataalamu wetu wakajiridhishe na ukubwa wa tatizo ili tujue tatizo ni kwamba hakuna mawasiliano au mawasiliano ni hafifu, ili tuweze kuchukuwa hatua stahiki ili kuhakikisha kwamba Itigi inapata mawasiliano ya TBC. Nakushukuru. (Makofi)