Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Mkoa wa Katavi ni moja kati ya mikoa iliyoanzishwa hivi karibuni ili kusogeza karibu na wananchi huduma muhimu za Serikali lakini mkoa huo hauna Hospitali ya Mkoa na Serikali ilishaamua kujenga hospitali hiyo na Serikali ya Mkoa ilishatenga eneo kwa ajili ya ujenzi. (a) Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza? (b) Jiografia ya Mkoa wa Katavi ni pembezoni mwa nchi; je, hiyo inaweza kuwa sababu ya kusuasua kwa mradi huo na kupita takribani miaka minne sasa toka Serikali ifanye uamuzi huo lakini hakuna hata dalili chanya kuelekea kukamilika kwa mradi huo?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Katavi kijiografia upo pembezoni lakini inapotokea shida ya barabara, shida ya huduma za afya inaufanya mkoa kuendelea kuwa pembezoni. Ninavyofahamu mimi, huduma ya afya kwa maana ya hospitali ni hitaji muhimu. Je, Serikali imejipangaje kulifanya jambo hili kwa haraka ili kunusuru nguvu kazi iliyoko kule kwa kuiepusha na maradhi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, fungu linalotengwa kwa ajili ya uendeshaji wa Hospitali ya Wilaya ni dogo, wananchi wote wa Wilaya ile ya Mpanda ambayo kwa sasa hivi ni mkoa, wanategemea Hospitali hiyo ya Wilaya. Je, Serikali inaisadiaje hospitali ile kwa maana ya kuiongezea bajeti?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ameuliza Serikali imejipanga vipi kuhakikisha jambo hili linafanyika kwa haraka?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kama nilivyosema awali, Serikali imetenga shilingi bilioni moja katika bajeti ya mwaka huu, tunachosubiri sasa hivi ni kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili mradi kazi hiyo ianze maana huo ndiyo mwanzo. Kazi yoyote haiwezi kufanyika lazima mshauri afanye kazi yake na kibali hicho kitakapotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali nadhani kazi hii itaanza rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato wa bajeti unaondelea sasa katika Ofisi ya Mkoa, kwa mwaka wa fedha 2016/2017 matarajio ni kwamba hospitali hii itatengewa shilingi bilioni 1.8 ili kuhakikisha watu wa Mkoa huu wa Katavi wanapata huduma ya afya. Umesema miundombinu ya barabara ina changamoto kubwa sana, endapo Hospitali ya Mkoa itakamilika tutawasaidia akina mama. Jambo hili ni la kipaumbele sana katika Serikali hii ya Awamu ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la hospitali yetu ya Mpanda ambayo kutokana na jiografia ilivyo inahudumia wananchi wengi wanaotoka maeneo mbalimbali. Pia inaonekana wazi hata dawa zikipelekwa pale hazitoshelezi na vifaa tiba vina changamoto kubwa. Namshukuru Mheshimiwa Waziri ameweza kupita katika maeneo mbalimbali, ni imani yangu tunakwenda kushughulikia jambo hili. Isipokuwa nawaagiza wataalamu wetu, mara nyingi wamekuwa na kigugumizi kikubwa sana cha kuandaa data za wagonjwa wanaotibiwa katika hospitali zao. Niwaagize zile data sheet za kusema hospitali inatibu wagonjwa wangapi zikusanywe vizuri. Mwisho wa siku ndiyo hizo data sheet ndiyo itakuwa taarifa elekezi ya jinsi gani Hospitali hii ya Mpanda iweze kusaidiwa ili mradi wananchi wapate huduma bora katika maeneo yao.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa niaba ya Waziri wa Nchi (TAMISEMI), napenda kujibu sehemu ya pili ya swali, je, Serikali inaisaidiaje Hospitali ya Wilaya ya Katavi katika kuongeza bajeti?
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema Naibu Waziri, afya ndiyo kipaumbele cha juu katika Serikali ya Awamu ya Tano, kwa hiyo, tutaongeza bajeti katika fedha zinazotoka moja kwa moja Serikalini. Hata hivyo, nimesimama kusisitiza jambo moja, ni lazima tuhakikishe mapato yanayopatikana kutokana na uchangiaji wa wananchi katika kupata huduma za afya yanatumika pia kwa ajili ya kuboresha huduma za afya. Tuwahimize Wanakatavi na wananchi wote wajiunge bima ya afya kwa sababu kadri wananchi wengi wanavyojiunga katika Mfuko wa Bima ya Afya au CHF, ndivyo mnavyopata fedha za kuweza kutatua changamoto za bajeti. Tumetoa mwongozo asilimia 60 ya fedha zinazopatikana kutokana na uchangiaji zirudishwe kwa ajili ya kuboresha huduma kama vile kununua dawa, vifaa na vifaa tiba. Kwa hiyo, bajeti haitatosha kwa sababu kasungura siku zote kitakuwa kadogo. Tutumie fedha za makusanyo za Bima ya Afya na CHF ili kuweza kutatua tatizo la bajeti ndogo.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Mkoa wa Katavi ni moja kati ya mikoa iliyoanzishwa hivi karibuni ili kusogeza karibu na wananchi huduma muhimu za Serikali lakini mkoa huo hauna Hospitali ya Mkoa na Serikali ilishaamua kujenga hospitali hiyo na Serikali ya Mkoa ilishatenga eneo kwa ajili ya ujenzi. (a) Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza? (b) Jiografia ya Mkoa wa Katavi ni pembezoni mwa nchi; je, hiyo inaweza kuwa sababu ya kusuasua kwa mradi huo na kupita takribani miaka minne sasa toka Serikali ifanye uamuzi huo lakini hakuna hata dalili chanya kuelekea kukamilika kwa mradi huo?

Supplementary Question 2

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Hospitali ya Kwangwa ya Mkoa wa Mara iliyopo Musoma Mjini imekuwa ni ya historia kila siku tunaisikia ipo tokea hatujazaliwa hadi leo; na kwa kuwa wanawake na watoto wanapata shida sana na vifo vingi vinasababishwa na umbali wa kutoka Hospitali ya Musoma hadi Mwanza, je, Serikali inaonaje sasa kwa sababu imeshaitengea bajeti Hospitali ya Kwangwa kumalizia suala hilo au kuipa kipaumbele Hospitali ya Kwangwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali imepokea suala zima la Hospitali ya Kwangwa. Maelekezo yetu ni kuhakikisha Hospitali za Wilaya na Mikoa zinafanya vizuri na zile ambazo zina changamoto kama vile miundombinu haijakamilika, changamoto za kibajeti zilizojitokeza katika kipindi cha nyuma kwamba bajeti zimetengwa lakini hazikufika, tunaenda kusisitiza suala zima la ukusanyaji wa mapato, huduma ya afya tumesema ni jambo la msingi ili kila mwananchi apate huduma bora ya afya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Marwa, Serikali imejipanga na katika kipindi hiki tutaangalia bajeti inasemaje katika hospitali hii. Lengo letu ni kuipa nguvu wananchi wa eneo hilo wapate huduma kwa manufaa ya Serikali yao.