Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha bei ya mbolea inashuka hadi kufikia kiwango cha Wakulima kumudu kuinunua ili kuiepusha nchi yetu kukumbwa na janga la njaa?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MAONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Sasa naomba niulize swali la nyongeza, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, mpaka sasa hivi Serikali bado haijawa na majibu sahihi kwa wakati sahihi yanayohusiana na suala la mbolea, ambayo kimsimgi imepanda bei katika maeneo yote ya nchi yetu ya Tanzania, hususan Mkoa wa Ruvuma: Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka ruzuku kwenye mbolea ili wananchi waweze kupata mbolea kwa bei nafuu?

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, Mkoa wa Ruvuma ndiyo benki ya chakula nchini Tanzania; na bila shaka yoyote Mkoa wa Ruvuma umeongoza takribani miaka minne mfululizo kwa uzalishaji wa mazao ya nafaka: Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kiwanda cha uzalishaji wa mbolea katika nyanda za juu Kusini, hususan Mkoa wa Ruvuma ikiwa ni pamoja na kuweka benki ya kilimo katika Mkoa wa Ruvuma? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline Msongozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza hakuna njia ya mkato kwenye sekta ya kilimo zaidi ya ku-design modal ya kutoa ruzuku. Nataka nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba, ilikuwa ni vigumu kwa mwaka huu kutengeneza mfumo wa ruzuku kwenye bei ya mbolea kwa sababu, historia inaonesha mifumo ya awali iliharibu na mifumo ile ilisababisha fedha nyingi za umma kupotea na wakulima hawaku-benefit na mfumo wa ruzuku uliokuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilihakikishie Bunge lako Tukufu, maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kwamba, Wizara ya Kilimo tutengeneze mechanism ambayo itatuletea mfumo sahihi wa ruzuku kwa pembejeo. Tutaleta mfumo wa stabilization fund na katika bajeti ya mwaka kesho mtaiona na tutaiwekea mkakati ili ruzuku iweze kwenda moja kwa moja kuwafaidisha wakulima. Hiyo ndiyo njia pekee itakayoweza kuwalinda wakulima wetu wadogo na huo ndiyo mwelekeo wa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tungetoa ruzuku leo, tusingekuwa na framework ambayo ingeweza kumfaidisha mkulima, bali kwenda kupoteza fedha za umma na hiyo isingekuwa haki kwa nchi. Kwa hiyo, kuanzia mwaka ujao wa fedha 2022/2023 tunaleta mfumo wa Stabilization Fund itakayotumika kwenye pembejeo na pale ambapo mazao ya wakulima yanaanguka kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu, ili kuwalinda wakulima wetu wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kujenga kiwanda; uwekezaji wa kiwanda unaangalia variables nyingi sana, siyo tu kwa sababu eneo fulani linazalisha mazao mengi, upatikanaji wa rasilimali kwa maana ya raw materials na zipo sababu nyingine. Siwezi kutoa ahadi ndani ya Bunge lako kwamba Serikali itaenda kujenga kiwanda katika Mkoa wa Ruvuma, lakini kama atatokea mwekezaji anataka kujenga kiwanda Mkoa wa Ruvuma, sisi kama Serikali tutamsaidia na kum-support ili aweze kujenga. Tunachokifanya, tunamsaidia mwekezaji wa intracom aliyeko hapa Dodoma ili aweze kuzalisha mbolea kutokana na ikolojia ya nchi yetu na yasitokee makosa yaliyotokea huko nyuma kwenye kiwanda cha Minjingu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo ambayo tunayafanya na tunawapa support. Kwa hiyo, kuna kiwanda hiki cha hapa Dodoma; na vilevile tumewasaidia Minjingu kwa ajili ya kupata fedha waweze ku-expand kiwanda chao cha Minjingu ili kiweze kufikia zaidi ya tani 100,000 tuweze kukidhi mahitaji ya nchi. (Makofi)