Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kutatua mgogoro wa bomoabomoa wa nyumba za wananchi zilizokuwa pembezoni mwa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kibamba ulioanza mwaka 2017?

Supplementary Question 1

MHE ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini ukweli mwenye dhamana ya kutafsiri sheria ni Mahakama na kumekuwepo na kesi ya ardhi chini ya Jaji Bongoyo ya mwaka 2005 ikahukumiwa mwaka 2013. Kesi ya Prochesta Lyimo na wenzake 72 dhidi ya AG na Wizara ya Ujenzi. Katika dhamana hiyo wadai walihalalishwa kwamba eneo ni la kwao na kama Serikali inalihitaji inatakiwa illipe fidia. Swali langu la kwanza, je, ni lini Serikali itatekeleza hukumu hii ya Mahakama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, Sheria ya Barabara ya mwaka 1932, Kanuni ya Mwaka 1955 na marekebisho Na. 13 mwaka 2009 inakinzana sana na Sheria nyingine za Mipangomiji na Sheria ya Vijiji ya mwaka 1999 ambayo ilifuta mikataba mingine na sheria nyingine zote zilizotangulia kwa kuweza kuwamilikisha watu ardhi ikiwa ilienda sambamba na zoezi la Operesheni Vijiji ya Mwaka 1974 na 1975 iliyoleta watu pembezoni mwa barabara kubwa na kuwapa miundombinu ya maji na elimu na kadhalika. Je, ni ipi kauli ya Serikali katika mchangamano huu au mchanganyiko wa sheria hizi ya barabara ya mwaka 1932 na hizi nyingine za ardhi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kiamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge wa Kibamba, kwanza nimshukuru na kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akilifuatilia suala hili kila wakati ili kuhakikisha tu wananchi wake hawa wanapata hicho ambacho anawapigania. Naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan inaongozwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria iliyopo. Moja ya wajibu wa Serikali ni kulinda wananchi pamoja na mali zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi aliyoisema ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ipo kwa Wakili Mkuu wa Serikali ambae yupo chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hatua waliyochukua wananchi hawa kupeleka suala hili kwenye vyombo vya kisheria, naomba nimhakikishie kwamba sheria itakapotamka mara ya mwisho nadhani haki itatolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kuhusu sheria kukinzana naomba tu nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara tunatumia Sheria yetu ya Barabara, lakini suala la kukinzana kwa sheria nadhani Serikali imelichukua na itaenda kuangalia sheria mbalimbali zinavyokinzana ili ziweze kusomeka na kueleweka kwa pamoja. Ahsante. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kutatua mgogoro wa bomoabomoa wa nyumba za wananchi zilizokuwa pembezoni mwa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kibamba ulioanza mwaka 2017?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mgogoro wa muda mrefu sana kati ya wananchi wa Kata ya KIA kwa maana ya vijiji saba na Kata ya Rundugai na kule Arumeru dhidi ya Uwanja wa Ndege wa KIA. Mgogoro huu Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba ataumaliza, lakini humu ndani nimekuwa nikiahidiwa na Serikali kila mara kwamba tutaenda kuumaliza. Hivi ninavyozungumza Mheshimiwa Diwani wa Kata ya KIA muda si mrefu amenipigia simu akiniambia kwamba wameanza kuweka alama ya X nyumba za watu bila kushirikisha wananchi na viongozi wa wananchi. Naomba majibu ya Serikali yaliyo thabiti, je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro huu? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saasisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na mgogoro kati ya wananchi na Serikali kwenye uwanja wa KIA. Mbunge amekuwa akilifuatilia mara kwa mara, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ameshaunda timu ambayo imekwenda kufanya tathmini na kufanya utafiti na mara watakapoleta taarifa tunategemea kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha Mheshimiwa Mbunge atapewa hiyo taarifa na tuna uhakika baadaye tutakwenda kwenye eneo la tukio lenyewe na yeye pamoja na wananchi ili suala hili liweze kufika mwisho. Ahsante. (Makofi)

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kutatua mgogoro wa bomoabomoa wa nyumba za wananchi zilizokuwa pembezoni mwa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kibamba ulioanza mwaka 2017?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata za Nanganga, Nangoo, Ndanda, Mwenda, Chikundi, Chigugu, Chikukwe, Chikunja pamoja na Lukuledi ambazo zinapitiwa na barabara kuu inayokwenda Nachingwea kutokea Masasi au barabara kuu inayotoka Mingoyo kulekea Mbamba Bay na Songea. Kwa muda mrefu sasa zaidi ya miaka Kumi hadi Ishirini nyumba za watu pamoja na mali zao zimewekewa alama za X. Ziko alama za X za kijani lakini pia zipo alama za X nyekundu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa wameshindwa kufanya shughuli zao zozote kwa sababu hawaelewi tafsiri ya alama hizi. Nataka kauli ya Serikali itueleweshe ni nini maana ya kuweka alama (X) nyekundu au alama (X) ya kijani kwenye maeneo hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecil Mwambe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, alama hizi zinaonesha kwamba wananchi wamejenga kwenye hifadhi ya barabara ama barabara itapita kwenye maeneo hayo. Wapo ambao barabara imewafuata kijani na wale ambao watatakiwa kufidiwa walikuwepo barabara wamewekewa alama ya (X) lakini ni kwamba hawa wote wataondolewa kwa utaratibu na kwa mujibu wa sheria. Ahsante. (Makofi)

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali imefikia hatua gani katika kutatua mgogoro wa bomoabomoa wa nyumba za wananchi zilizokuwa pembezoni mwa Barabara ya Morogoro kutoka Kimara hadi Kibamba ulioanza mwaka 2017?

Supplementary Question 4

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Kata ya Kipawa ambao walipisha Airport terminal three tangu mwaka 1997 na sehemu hiyo mpaka sasa hivi shughuli za maendeleo zimesimama. Je, ni lini Serikali itawalipa hawa wananchi fidia? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi aliowasema wa Kipawa Airport ambao walipisha ujenzi wa uwanja wa ndege, suala hili nimwombe Mheshimiwa Mbunge aweze kutuletea maelezo sahihi kwa sababu ambao walilipwa na hawa ambao hawakulipwa ili tuweze kujua ni wapi ambao hasa anawasimamia ili tuweze kuwa na majibu sahihi kwa upande wa Serikali. Ahsante.