Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bwawa la Zombo linatumika kikamilifu kwa ufugaji wa samaki na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali ambayo yanatoa tumaini kwa vijana wa Jimbo la mikumi. Swali langu la kwanza; kwa kuwa Serikali itaangalia uwekezaji unaofaa katika bwawa hilo, je, mpango huo unahusisha pia uzalishaji wa vyakula vya samaki katika viwanda vidogo na vya kati katika eneo la Jimbo la Mikumi ili kukuza ufugaji wa samaki?

Mheshimiwa Spika, la pili, karibu na Zombo kuna reli ya mwendokasi ambako kuna mashimo makubwa ambayo walikuwa wanachimba kokoto wakati wa ujenzi huo. Mashimo haya makubwa yana potential ya kubadilishwa kuwa mabwawa kwa ajili ya ufugaji wa samaki lakini pia kwa ajili ya mifugo. Je, Serikali itakubaliana nami kwamba wakati umefika wa kuyatengeneza mabwawa haya ili kutatua tatizo letu? Nashukuru.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Denis Lazaro Londo, Mbunge wa Jimbo la Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, umuhimu na uhitaji wa vyakula vya mifugo nchini hususan samaki ni mkubwa sana na kwa kadri tunavyoendelea kuhamasisha ufugaji wa samaki umuhimu umezidi kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Londo, kwamba tunahitaji uwekezaji zaidi. Katika Mkakati tulio nao ndani ya Serikali ni kuvutia uwekezaji wa uzalishaji wa chakula cha samaki.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa mabwawa ama mashimo yaliyotokana na ujenzi wa reli ya SGR, nakubaliana naye na ni wazo jema sana.

Mheshimiwa Spika, sisi katika Wizara tumeanza mazungumzo na wenzetu wa reli ili kuhakikisha kwamba mabwaya yale tunayaongezea thamani kwa kuyatengenezea miundombinu ili yaweze kutumika kwa ajili ya shughuli za ufugaji pamoja na shughuli za ufugaji wa samaki. Ahsante sana.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bwawa la Zombo linatumika kikamilifu kwa ufugaji wa samaki na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali inatambua ufugaji wa samaki kwenye mabwawa kule ukanda wa Ziwa Victoria na maeneo yote yanayozunguka na hasa maeneo ya kandokando kwenye miji mikubwa, zoezi la ufugaji wa samaki kwenye vizimba linaendelea kukua kwa kasi na tunaamini linaweza likatoa ajira nyingi sana kwa vijana.

Je, ni upi sasa mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba vijana wengi zaidi wanaingizwa katika shughuli hizi na kupewa fedha ili waweze kuwekeza kwenye ufugaji wa vizimba?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mkakati wetu ndani ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ni kwamba tumeweka hela kiasi cha shilingi milioni 154. Pesa hizi ni kwa ajili ya kwenda kufanya mpango wa matumizi bora, kwa lugha nyepesi, katika eneo la Ziwa Victoria, Mkoa wa Mwanza na Mkoa wa Kagera. Tunakwenda kufanya demarcation na pesa hii tumeipeleka katika Taasisi yetu ya Utafiti ya TAFIRI kwa lengo la kutuandalia maeneo mahsusi ambayo vijana watakwenda kuyatumia kwa ajili ya ufugaji wa vizimba.

Mheshimiwa Spika, kama haitoshi, vijana hawa tutawaweka katika ushirika ambao utawasaidia kuweza kupata mikopo na kuweza kujifanyia shughuli zao.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bwawa la Zombo linatumika kikamilifu kwa ufugaji wa samaki na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali Wilaya ya Bunda inaishi karibu sana na Ziwa Victoria na Jimbo la Bunda ni kilometa 45 kutoka Ziwa Victoria. Sasa kwa sababu kuna pressure kubwa ya uvuvi wa samaki na kwa sababu sasa tunataka kupunguza hiyo pressure ya wavuvi wa samaki.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuweka mikakati ya kuweka vizimba katika Jimbo la Bunda na hasa pale kwenye mabwawa ya kuchimbwa kwa ajili ya kufuga samaki?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni mkakati endelevu tulionao wa kuhakikisha kwamba tunakwenda kwenye eneo hili la ufugaji wa samaki na hasa upande wa Ziwa Victoria ambako kuna ufugaji wa kutumia vizimba na hivyo Jimbo la Bunda nalo litafikiwa.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bwawa la Zombo linatumika kikamilifu kwa ufugaji wa samaki na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana?

Supplementary Question 4

MHE. JAFARY W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa shughuli hii ya ufugaji wa samaki inafanyika pia katika Jimbo la Rorya, kwa maana ya wilaya nzima, hasa ukizingatia kwamba umbali wa kutoka ziwa kuelekea kwenye maeneo ya wananchi haizidi hata mita tano. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia vijana wa maeneo yale ambao wanaishi karibu na ziwa ili kufanya na kuanzisha ufugaji huu wa samaki?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeeleza, kwamba ufugaji wa samaki, hasa kwenye vizimba, upande wa Ziwa Victoria ndicho kipaumbele chetu cha kule tunakolekea ili kupunguza pressure ya uvuvi ule wa asili. Ili kuweza kufanikiwa katika lengo hili tunahamasisha uundaji wa vikundi, hasa vikundi vya Ushirika, hivyo namwomba Mheshimiwa Chege na Waheshimiwa Wabunge wengine wote wa eneo hili waweze kuwahamasisha vijana wale wajiunge katika vikundi ili tuweze kupata mikopo kupitia Benki yetu ya Kilimo na hatimaye kuweza kuifanya shughuli hii ambayo itawaingizia kipato na kukuza pato la Taifa letu.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bwawa la Zombo linatumika kikamilifu kwa ufugaji wa samaki na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana?

Supplementary Question 5

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kilimo na Chakula (FAO) limetangaza mpango maalum wa ufugaji wa samaki katika maneo mbalimbali duniani ikiwemo Ziwa Tanganyika. Je, Serikali yetu imechukua hatua gani za haraka za kushirikiana na shirika hili katika kufanikisha mpango huo?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. FAO ni wadau wetu wakubwa na tunashirikiana nao kama Serikali. Hata hivyo, kwa jambo hili mahsusi alilolisema Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda ninaomba nimkaribishe kula swali mahsusi ili tuweze kulifanyia kazi. Ahsante.