Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri kweli ya Serikali, lakini je, barabara hii ambayo imengojewa kwa muda mrefu sana na Serikali inaendelea kutafuta fedha. Je, wananchi wa Jimbo langu wasubiri mpaka lini ili barabara hii ianze kujengwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kipande kile cha Mambari – Bukumbi, Shitaga na Ishihimulwa, je, ni lini Serikali itaweka katika bajeti fedha za kufanyia usanifu wa ujenzi wa barabara hii? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge aone jitihada za Serikali, ni mwaka jana tu 2020, tumekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa maana, ya maandalizi ya kuanza kujenga kwa kiwango cha lami kilomita hizo 56. Hata hivyo, barabara iliyobaki tumekiri kwamba bado haijafanyiwa upembuzi na Serikali inatafuta fedha.

Kwa hiyo, Mheshimiwa avute subira, Serikali ina mpango na ndio maana tayari tumeshaanza hatua na fedha itakapopatikana tutaanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Kipande kilichobaki hadi Muhulidede kitafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nataka kujua wananchi wa Kokoto, Mzinga mpaka Kongowe ambao walithaminiwa zaidi ya miaka minne sasa, je, ni lini sasa Serikali itawalipa fidia zao ili ujenzi wa barabara hiyo uanze? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kokoto, Zinga, Kongowe ni kweli inasubiri fidia zifanyike ili barabara ianze ujenzi. Naomba nimhakikishie taratibu zinaendelea na Serikali, ili tukishapata tathmini na kupata fidia kamili tutaanza kuwalipa na utaratibu wa ujenzi wa barabara hii utaanza. Kwa sababu, hatuwezi kuanza ujenzi kabla ya fidia. Ahsante.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami kuunganisha barabara ya Mnivata – Tandahimba – Newala – Masasi kwa kuwa tulishaona kwenye vyombo vya habari upatikanaji wa fedha umekamilika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Agnes kwamba barabara ya Mnivata – Tandahimba- Newala hadi Masasi yenye urefu wa kilomita 210; kilomita 50 Mtwara hadi Mnivata imekamilika na tayari barabara hii ipo kwenye taratibu za manunuzi ambapo itafadhiliwa na Benki ya African Development kwa ajili ya ujenzi wa barabara yote. Ahsante. (Makofi)

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri: Je, ni lini Serikali itamalizia barabara ya Bonyokwa – Kimara ambayo tangu mwaka 2021 ilikuwa kwenye bajeti ambayo ni kilomita 3.5? Ni lini itawekwa lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoisema ya Bonyokwa ipo kwenye mpango wa TANROADS wa kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, Serikali bado inaendelea kutafuta fedha kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Segerea kwamba hii barabara ni muhimu sana ambayo inaunganisha Segerea na Kimara; na tutaijenga kwa kiwango cha lami mara fedha itakapopatikana. Ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Napenda kuuliza swali langu la nyongeza kwamba, barabara ya Tarime - Mugumu - Serengeti ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Mkoa wa Mara na Tanzania ukizingatia watalii wanaotokea Kenya kuingia Mkoa wa Mara: -

Je, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami ukizingatia wananchi ambao walikuwa wanaishi kandokando ya barabara hii kwa upande wa Tarime wamebomolewa nyumba zao na waliokuwa wanafanya biashara kuondolewa ili kupisha ujenzi wa barabara hii? Je, ni lini ujenzi utaanza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Tarime hadi Mugumu - Serengeti tayari imeshakamilisha usanifu wa kina na Serikali iko kwenye kutafuta fedha kuijenga; lakini ilionekana ni busara kujenga kwanza daraja ambalo lilikuwa linasumbua sana ambalo tumelikamilisha. Baada ya hapo fedha ikishapatikana tutaanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita nane kati ya kilomita 42 inayoanzia Kibosho Shaini – Kwa Rafael hadi International School?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Partrick Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ametaka kujua ni lini Serikali itakamilisha kipande cha kilomita Nane cha barabara yake ya kutoka Kibosho Shaini - Kwa Rafael hadi International School. Barabara hii ina urefu wa kilomita Nane. Serikali ilishaanza na ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha na ikipatikana, kipande hiki cha kilomita nane zilizobaki itakijenga kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, barabara inayotoka Singida kwenda Sepuka kupita Ndago mpaka Kizaga yenye urefu wa kilomita 95 iliahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapunduzi toka mwaka 2015 na Rais Hayati Dkt John Joseph Pombe Magufuli alipokuja kwenye kampeni kwenye Jimbo langu aliahidi kujengwa kwa barabara hiyo kwa kiwango cha lami: -

Je, ni lini Serikali ya Chama cha Mapinduzi itakwenda kutekeleza ahadi hii ikiwa ni moja ya kumbukumbu ya kuenzi ahadi za Hayati Dkt. John Joseph Pombe Magufuli? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kingu, Mbunge wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ya kutoka Sepuka hadi Ndago, kama alivyosema ni ahadi ya Kiongozi wa Kitaifa; na moja ya vipaumbele vya Serikali ni kuhakikisha kwamba tunatimiza ahadi zote za Mheshimiwa Rais. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii itajengwa. Namwaomba Mheshimiwa Mbunge mara baada ya hapa kwa sababu pengine ni kipindi cha bajeti, basi tunaweza tukaonana ili tuone namna ambavyo tunaweza tukaingiza kwenye bajeti zinazoendelea kupangwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itakamilisha upanuzi wa barabara ya Moshi – Arusha kipande kinachoanzia Tengeru - Moshi mpaka Holili?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tarimo, Mbunge wa Moshi kama ifuatavyo: -

Mhesimiwa Mwenyekiti, huu ni mwendelezo wa barabara ambayo ipo kwenye mpango. Tayari tumeshaanza huko Arusha na tunategemea kwa sababu ni barabara muhimu kutoka Arusha kwenda Holili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ipo kwenye mpango na tunaendelea. Ninaamini katika bajeti inayokuja barabara hii itapata mwendelezo wa kuijenga hatua kwa hatua kadri fedha inavyopatikana. Ahsante. (Makofi)