Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha maji safi na salama katika Kata za Kikolo, Utiri, Mbangamao, Kilimani na Mateka?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Vile vile naomba niishukuru Serikali kwa kutekeleza miradi ya Lusaka, Mradi wa Mpepai na mradi wa Lifakara. Mwaka 2020 Serikali ilianza kutekeleza mradi katika Kata ya Myangayanga na Kata ya Ruahita, miradi hiyo miwili hadi sasa bado haijatekelezwa. Kwa hiyo nataka nijue, je, Serikali ina mpango gani wa kutekeleza miradi katika hizo kata mbili? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jonas Mbunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hizi kata alizozitaja ziko kwenye mpango wa utekelezaji na kwa Mbinga Mjini tunatarajia hadi kufika 2023 Disemba, labda vitabaki kama vijiji viwili tu ambavyo vitakuwa bado havijapata maji. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, kwa namna ambavyo tunashirikiana nampongeza sana na nimhakikishie maji Mbinga yanakwenda kupatikana.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha maji safi na salama katika Kata za Kikolo, Utiri, Mbangamao, Kilimani na Mateka?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri. Je, ni lini Serikali itafikisha huduma ya majisafi na salama katika Wilaya za pembezoni katika Mkoa wa Mtwara?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara imejipanga kutumia Mto Ruvuma kuona maeneo yote ya pembezoni yanaenda kupata maji na Wizara tunaendelea kutafuta fedha, naamini ndani ya mwaka ujao wa fedha maeneo mengi ya pembezoni mwa Mtwara yataenda kupata maji.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha maji safi na salama katika Kata za Kikolo, Utiri, Mbangamao, Kilimani na Mateka?

Supplementary Question 3

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Changamoto ya maji Wilaya ya Chunya ni kubwa sana. Sasa naomba nimuulize swali Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Mradi wa Maji wa Kiwira umekuwa unatajwa muda mrefu na mpaka sasa utekelezaji wake haujaanza na mradi huu utafaidisha Wilaya ya Chunya pamoja na Mbeya Mjini. e, ni lini sasa Serikali itatoa fedha mradi huu uanze kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka, Mbunge kutoka Chunya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba kumpongeza Mbunge Kasaka kwa kazi nzuri aliyoifanya Chunya, miradi ambayo ilikuwa kichefuchefu toka mwaka 2012, Mradi wa Matwiga sasa hivi upo kwenye hatua nzuri na tayari tumeshampata mkandarasi anakuja kule kwa ajili ya usambazaji wa vijiji vinne vya awali na huu Mradi wa Kiwira wiki ijayo tunakwenda kusaini mkataba ili mradi uanze utekelezaji. Hivyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana na kwa kazi nzuri anayoifanya Wanachunya wanakwenda kufaidika. (Makofi)

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha maji safi na salama katika Kata za Kikolo, Utiri, Mbangamao, Kilimani na Mateka?

Supplementary Question 4

NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nimekuwa nikiuliza mara kwa mara Mradi wa Maji wa Igando Kijombe ndani ya Wilaya ya Wanging’mbe. Mradi huu sasa hivi ni muda wa miaka mitatu imepita, bajeti yake ya kwanza ni bilioni 12, lakini hadi sasa ni bilioni nne tu ambazo zimekwenda kwenye mradi hule, muda umekuwa mrefu na mradi huu ni muhimu kwa wananchi wa Wilaya Wanging’mbe. Je, ni lini mradi huu utaenda kukamilika ili uweze kuleta tija kwa wananchi wa Wanging’ombe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amekuwa akitoa ushirikiano sana katika mradi huu, lakini napenda kumwarifu Mheshimiwa Mbunge huu mradi tayari tumeutembelea hivi karibuni na nimpongeze kwa ushirikiano na Mheshimiwa Dkt. Dugange ameweza kufuatilia. Vile vile niseme tu kwamba tayari mkandarasi anaendelea na kazi na kwa sababu mradi huu ulikuwa ni mkubwa tunafikia phase za mwisho, maeneo ambayo tayari yalikamilika wananchi wameanza kupata huduma ya maji. Hivyo napenda kumtoa hofu Mbunge, mradi huu unakwenda kukamilika ndani ya sera ya kumtua ndoo mama kichwani, tumshukuru Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuisimamia vizuri. (Makofi)