Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuchimba malambo kwa ajili ya maji ya mifugo katika maeneo ya wafugaji mkoani Manyara?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, Nakushukuru sana na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja dogo la nyongeza. Vifo vingi vya mifugo hutokea kipindi cha kiangazi au ukame kutokana na upungufu mkubwa wa maji na malisho ya mifugo hususan mwaka jana mwezi Septemba mpaka Januari mwaka huu vifo vingi vilitokea hasa katika Wilaya ya Kiteto ambapo zaidi ya mifugo 1,874 ilikufa na Simanjiro zaidi ya mifugo 62,500 ilikufa, mabaki Bonde la Magara mifugo ilikufa lakini mifugo ilizidi kudhoofu katika Wilaya ya Mbulu na Hanang.

Je, Serikali sasa haioni umuhimu wa kuwekeza miundombinu wa uhakika ikiwepo wa uchimbaji wa visima virefu, mabwawa na malambo katika maeneo haya kukabiliana na vifo vya mifugo, lakini vile vile, kumnusuru mfugaji asibaki katika dimbwi la umasikini. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA UVUVI NA MIFUGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yustina, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampa hongera Mheshimiwa Mbunge Yustina kwa ufuatiliaji huu wa jambo hili zito lililowapata wafugaji. Mbili, pia atakubaliana nami kwamba Serikali ilitoa pole kwa wafugaji wote wa Mkoa huu wa Manyara ambao ameutaja hapa.

Katika jibu letu la msingi tumeeleza ya kwamba tutafanya mazingatio katika bajeti ya mwaka huu wa 2022/ 2023 ambapo tutachimba visima virefu na vile vile tutajenga mabwawa na kwa msisitizo maeneo haya aliyoyataja yote tutazingatia ili kusudi pasiendelee kuwepo kwa marejeo ya mambo yaliyotokea katika mwaka huu ambapo palikuwa na kiangazi kirefu.

Name

Christopher Olonyokie Ole-Sendeka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuchimba malambo kwa ajili ya maji ya mifugo katika maeneo ya wafugaji mkoani Manyara?

Supplementary Question 2

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya nyongeza. Kwa kuwa janga la mwaka huu na mwisho wa mwaka jana inalika nguvu za ziada za Serikali katika kutenga fedha za kutosha kuchimba mabwawa katika maeneo ya nyanda kame. Je, Serikali itaweka bayana idadi ya mabwawa yatakayoweza kujengwa ili kunusuru hali iliyotokea juzi isirejee kabla ya bajeti ya mwaka 2022/2023 kuanza?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba jambo hili la idadi hasa liwe ni jambo la utendaji kazi. Kwa hivyo, sisi tutawasiliana halmashauri yake tupate namba halisi ili tuweze kulifanyia kazi.