Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kwa kutengeneza miundombinu ya kupeleka maji kwa Wakazi waishio sehemu za miinuko?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa majibu yaliyotolewa, lakini watu wa Kyerwa hawana majikwa asilimia 56 kama Serikali inayoeleza. Changamoto ya upatikanaji wa maji ni kubwa zaidi, naweza kusema ni asilimia kama 25. Kwa hiyo, naomba Serikali ifanye mkakati wa maksudi wa kuwasaidia watu wa Kyerwa wapare maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, ametaja Mradi wa Runyinya, Chanya, Kimuli, Rwanyango, Nyamiaga na Nyakatera ambapo ukiweza kusainiwa na kuanza utapunguza kwa kiwango kikubwa upatikanaji wa maji. Nataka kujua ni lini sasa mkataba utasainiwa kwa sababu imekuwa ni kila siku mkataba unakaribia kusainiwa. Nataka nijue ni lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wananchi wa Kata za Nyakatuntu, Kimuli, Kamuli, Bugara na maeneo mengine wana changamoto kubwa ya maji na wameahidiwa watakuwa kwenye mradi wa vijiji 57 ambapo iwapo utatekelezwa ungepunguza changamoto ya maji. Haujaanza na hatujui unaanza lini. Nataka nijue ni lini huo mradi utaanza na kukamilika ili kuondoa adha kubwa ya maji kwa wananchi wa Jimbo la Kyerwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda kumpongeza Mheshimiwa Anatropia kwa maswali yake mazuri na ninamwona ana ushirikiano wa karibu sana na Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge mwenye Jimbo, ambaye ameendelea kufuatilia miradi hii yote. Mheshimiwa Innocent Bilakwate ni juzi ametoka Ofisini kuhakikisha anaweka sawa miradi hii ambayo inaenda kufanyika katika Jimbo la Kyerwa. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tuna mradi wa Kamuli ambao kijiografia upo juu. Tunatarajia mradi huu kwenda kutekelezwa hivi karibuni na utekelezaji wa mradi huu utasaidia kusambaza maji katika vijiji vingi vya Jimbo la Kyerwa. Hivyo, napenda kukutoa hofu Mheshimiwa Mbunge, miradi hii itasainiwa kwa taratibu za Wizara zilizopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, percentage za usambazaji maji katika Jimbo la Kyerwa ni asilimia za kitaalam, siyo za kufikirika kuangalia tu kwa macho na ukasema ni asilimia 20. Ni asilimia zilizotajwa na watalaam, zimefanyiwa kazi na tuna uhakika na kazi tunayoifanya. Nasi Wizara ya Maji siyo wababaishaji, lengo letu kubwa ni kuhakikisha tunamtua ndoo mama kichwani kama ambavyo Mheshimiwa Rais wetu anatutaka. (Makofi)

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kwa kutengeneza miundombinu ya kupeleka maji kwa Wakazi waishio sehemu za miinuko?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Changamoto iliyopo kwenye Jimbo la Kyerwa inafanana kabisa na changamoto zilizopo Wilaya ya Chemba. Changamoto kubwa ni miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru sana Serikali kwa kupitia Wizara ya Maji, nami ni shabiki mkubwa wa Mheshimiwa Waziri Jumaa Aweso. Yale maneno ambayo Ndugu yangu Mheshimiwa Jerry Silaa alisema, nami nayathibitisha kwamba anapaswa kupewa zile Ph.D ambazo zinatolewa, tena apewe Tanzania. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu sasa. Pamoja na kuwa tumepata visima vitano na vimechimbwa zaidi ya miaka miwili, vingine mmoja, lakini bado havifanyi kazi kwa sababu miundombinu yake haipo tayari: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua, ni lini sasa Serikali kupitia Wizara ya Maji itaweka miundombinu ili watu wale nao waanze kupata maji? Ahsante sana.(Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, kwa kweli nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge wa Chemba kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya kwa muda mfupi katika Jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, ni kweli tulishafika Chemba, hali ya Chemba ilikuwa siyo nzuri. Maelekezo ya kwanza ambayo tumeyafanya ni katika kuhakikisha kwamba tunachimba visima vya dharura ili wananchi wa Chemba waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Nataka nimhakikishie katika mfuko wa mwezi huu tutatoa fedha ya uanzaji wa miradi ile ili wananchi wa Chemba waweze kupata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumaliza kabisa tatizo la Maji Chemba, siyo maeneo yote ambayo utachimba ukapata huduma ya maji. Eneo la Chemba limetupa experience baadhi ya maeneo yamekuwa na ukame. Tunakwenda kuchimba bwawa kubwa katika kuhakikisha wananchi wa Chemba wanaendelea kunufaika na maji. Tunaona mvua zinazonyesha maji yanapotea tu. Mkakati wa Wizara na mageuzi ya Wizara ni kuhakikisha tunachimba mabwawa makubwa ili kuvuna maji na wananchi wa Chemba waendelee kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kwa kutengeneza miundombinu ya kupeleka maji kwa Wakazi waishio sehemu za miinuko?

Supplementary Question 3

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Nianze kwanza kwa kutoa pongeza nyingi sana kwa Serikali kwa namna ilivyoshughulikia matatizo ya wananchi wa Jimbo la Buchosa. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa juhudi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upo mradi wa Lumea, Nyakariro, Karebezo hadi Nyehunge wa shilingi bilioni 1.6. Mradi huu ni kichefuchefu, ulijengwa chini ya kiwango, mabomba yanapasuka, maji yanamwagika chini na wananchi hawapati maji: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini atatembelea mradi huu ili kuweza kuwa na utaratibu wa kufanya maboresho na wananchi waweze kupata maji?

Pili, ni lini Serikali itapeleka watalaam kuchunguza na kugundua watu waliohusika na ubadhirifu kwenye mradi huu ili waweze kuchukuliwa hatua kuepusha kuharibu sifa ya Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa ujumla. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eric Shigongo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la kwenda kutembelea Mheshimiwa Mbunge mantahofu, mara baada ya Mkutano huu tutakwenda kutembelea na kujionea na kuona kwamba kazi zinaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Watalaam kwenda kuchunguza, Mheshimiwa Waziri ameshatengeneza task force ya kufuatilia miradi yote kichefuchefu na kuona kwamba inafanyiwa kazi na inakamilika na huduma ya maji inapatikana bombani na tunamtua ndoo mwanamke kichwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, napenda kusema kwamba, ile task force naamini wamesikia na ninasisitiza maagizo ya Mheshimiwa Waziri mara wasikiapo maagizo haya waweze kwenda mara moja ili kuchunguza na miradi ile iweze kukamilika na lengo la kutoa maji na kumtua mama ndoo kichwani liweze kutimilika. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia maji wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kwa kutengeneza miundombinu ya kupeleka maji kwa Wakazi waishio sehemu za miinuko?

Supplementary Question 4

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nakushukuru kwa kuniruhusu niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la Jimbo la Kyerwa la maji, linafanana sana na tatizo la Jimbo la Kawe; na kwa kuwa ndugu Waziri wa Maji, Mheshimiwa Jumaa Aweso alikuwa na mradi unaotokea Ruvu Chini mahali ambapo amejenga matenki Mabwepande, Bunju A, Tegeta, Salasala na maeneo mengine ya Jimbo la Kawe; na mradi huu ulitegemewa mwisho wa mwaka Desemba uwe umeshakamilika ili watu wapate maji, lakini mpaka leo Madale, Nakasangwe, Kisauke, Mabwepande, Tegeta hazina maji: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa mradi huu utakamilika ili wananchi wangu wa Jimbo la Kawe wapate maji? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, kwa kweli nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu Mheshimiwa Askofu Josephat Gwajima kwa kazi kubwa anayoifanya katika Jimbo la Kawe. Kwa kweli maeneo ya Mabwepande yamekuwa na changamoto kubwa sana na tunaona kazi kubwa inayofanywa na DAWASA. Naomba baada ya saa 7.00 tukutane, tufanye mawasiliano na Mkurugenzi wa DAWASA ili tuweze kutia nguvu kwa pamoja na mradi ule uweze kukamilika na wananchi wa Mabwepande waendelee kupata huduma ya maji. Ahsante sana. (Makofi)