Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Wodi za Wagonjwa wenye matatizo ya Ubongo na Akili katika Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kwa sasa wagonjwa wote wa akili katika Hospitali za Temeke, Mwananyamala na Amana, wanapelekwa katika Hospitali ya Muhimbili, lakini jengo hilo la wagonjwa wa akili la Hospitali ya Muhimbili halijafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu kiasi kwamba, mwananchi wa kawaida kuingia kwenye ile wodi unaogopa. Sasa napenda niiulize Serikali.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati jengo la wagonjwa wa akili katika Hospitali ya Muhimbili, ili Madaktari wetu waweze kufanya kazi zao katika mazingira mazuri na wagonjwa waishi katika mazingira mazuri? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha kwamba, kuanzia mwaka 2020 kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa akili duniani na hasa vijana kuanzia miaka 15 mpaka miaka 35 na hiyo inatokana na matatizo na changamoto mbalimbali za kimaisha. Haya yameanza kujitokeza katika nchi yetu ya Tanzania, watu wameanza kuuana ovyo na matendo ambayo sio ya kibinadamu yanatendeka sana, tunapata hizo taarifa. Je, Serikali haioni haja sasa ya kujenga hospitali maalum ya wagonjwa wa akili badala ya kuwa Mirembe, Dodoma peke yake? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mbunge kwa ufuatiliaji mzuri sana anaoufanya kwa kufuatilia masuala ya afya ya watu wanaoishi kwenye Mkoa wa Dar-es-Salaam, tunampongeza sana Mheshimiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama Mheshimiwa Mbunge anavyosema kwamba, kweli jengo lile liko chakavu pale Muhimbili, lakini kwa mwaka huu tu, hii miezi miwili iliyopita, hospitali ya Muhimbili Rais wetu amepeleka bilioni 16 pale, lakini ilitengwa zaidi zaidi ya milioni 400 kwa ajili ya kukarabati jengo lile, lakini kwa sababu ya matatizo ya corona na kulikuwa na umuhimu wa kuhakikisha baadhi ya expenses zilizoongezeka wangebeba wananchi wenyewe ingeleta shida, fedha zile zilielekezwa upande huu, lakini ameshatoa maelekezo Waziri wa Afya juzi alivyotembelea Muhimbili na sasa hiyo kazi inaenda kuanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, samahani. Swali lake la pili amezungumzia kwamba, kuna matatizo ya akili yameongezeka duniani, lakini vilevile hapa nchini kwetu Tanzania. Ni kweli, yameongezeka, suala sio kuongeza idadi ya hospitali, lakini ni kuangalia visababishi ambavyo vinasababisha watu kupata matatizo hayo viweze kutatuliwa. Vilevile sio tu kujenga hospitali maalum kwa ajili ya hiyo, lakini ni ku-integrate hizi huduma kwenye huduma nyingine mpaka kushuka chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais wetu ameshaelekeza kwamba, hospitali zote zianze na nilianza na Kigoma kama uliangalia kwenye vyombo vya habari, kulikuwa na wataalam wa afya ya akili na wale wataalam wa afya ya akili tukaanza kuelekeza kwamba, waanze sasa kutengewa bajeti na zile ofisi zao zipewe bajeti ya kutosha ili waweze kufanya kazi zao na kushuka chini mpaka kwenye vituo vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata unapoona CT-Scan zimesambazwa kwenye hospitali zote za mkoa, wakati mwingine wagonjwa wa akili wamekuwa wakitibiwa kwa kuangalia dalili zao tu, lakini sasa tunataka kwenda kuwaangalia kabisa, kwa sababu wanaweza wote kuonesha dalili zinazofanana, lakini visababishi vikawa tofauti. Kwa hiyo, sasa tunaenda kwenye level ya kupiga CT scan za ubongo ili kila mmoja aweze kutibiwa kwa namna ambavyo ana tatizo lake. Ahsante sana.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Wodi za Wagonjwa wenye matatizo ya Ubongo na Akili katika Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala?

Supplementary Question 2

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo la afya ya akili hata katika Mkoa wetu wa Iringa limekuwa kubwa sana na changamoto kubwa kabisa ya tatizo hili ni kwamba, bei ya dawa iko juu sana, sana. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba, dawa zinakuwa na bei ndogo au kuondoa kabisa, ili waweze kupatiwa bure kama yalivyo magonjwa mengine?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba nijibu swali lake la nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kwanza dawa za wagonjwa wa akili zinatolewa bure na tayari Serikali imeshapeleka kwenye maeneo yote watu wa kufanya hivyo. Kama kuna mahali wanawauzia kwa Mkoa wa Iringa, nitalifanyia kazi ili kuona namna ya kufanya. Nalipokea ili tuweze kulifanyia kazi. Wote tutaona kwamba Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan ameshaunda Wizara ya Maendeleo ya Jamii, mojawapo ya kazi ni kuhakikisha, ile Wizara itakaposimama kwenye eneo lake tutapunguza sana mambo yanayosababisha yanayoongezea idadi ya watu wenye matatizo ya akili kwenye jamii.

Kwa hiyo, kikweli nachukua wazo la Mheshimiwa la dawa, lakini tutaenda kulifuatilia zaidi na kwenda Iringa kuimarisha zaidi hicho kitengo ambacho umekizungumzia hasa kwenye eneo la dawa.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Wodi za Wagonjwa wenye matatizo ya Ubongo na Akili katika Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nikiri kabisa kwamba, Wizara ya Afya kwa kweli, kwa upande wetu Jimbo la Hai wanatutendea haki, lakini naomba niulize swali. Hospitali yetu ya Wilaya ya Hai ni chakavu sana na watumishi wanapata tabu kweli kutoa huduma pale. Walk ways zimekuwa chakavu, hatuna jengo la mama na mtoto, hatuna jengo la pharmacy, kiufupi hospitali hii ni chakavu na Naibu Waziri anaifahamu vizuri. Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika hospitali yetu ya Wilaya ya Hai?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Hai kwa jinsi ambavyo anapambana na matatizo ya watu wa Hai. Kwenye hospitali hiyo ya Hai Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan amepeleka milioni 220, amepeleka 300, akapeleka tena milioni 90 kwa ajili ya kujenga nyumba ya watumishi, hata hivyo, nakubaliana na yeye kwamba, kwa kweli hospitali hiyo ni chakavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipita mimi na yeye na kikubwa tuliongea na DMO pale kwamba, sasa waanze kuweka kwenye mchakato wa bajeti ya mwaka huu ili itakapofika fedha zimepatikana basi liweze kutekelezeka kulingana na taratibu za fedha.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Wodi za Wagonjwa wenye matatizo ya Ubongo na Akili katika Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kama ilivyoelezwa hapo awali kwamba, kumekuwa na ongezeko la matatizo ya akili na tunafahamu ongezeko la matatizo ya akili ni pamoja na kukosekana kwa watu wa ushauri na unasihi. Je, ni nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha inaongeza Maafisa Ustawi wa Jamii mpaka ngazi ya kata? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge alivyosema. Tunachukua hilo wazo, lakini katika sehemu nyingi kuna Maafisa Ustawi wa Jamii, bahati mbaya tu tukienda kwenye wilaya zetu wamepewa kufanya kazi nyingine, unakuta wengine ni Watendaji wa Vijiji au wengine wanafanya shughuli nyingine ambazo sio za ustawi wa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kikubwa kwanza tutaenda kusimamia waliopo kwanza wafanye kazi ambayo walitakiwa kuifanya na wawezeshwe kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa sababu tumefika kwenye level ya mkoa kupeleka wataalam hawa wanaoshughulikia masuala ya akili, basi tutashusha kwenye wilaya ikiwezekana kwenye vituo vya afya jinsi bajeti itakavyoruhusu. Ahsante sana.