Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusimamia kikamilifu Sera ya Afya ili akinamama wajawazito na watoto wasitozwe gharama katika vituo vya afya?

Supplementary Question 1

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu ya Serikali yaliyotolewa hapa, bado kuna tatizo kubwa, hasa kwenye vituo vyetu vya afya, huduma hii imekuwa ngumu sana kwani akinamama wanapokwenda kujifungua wameendelea kutozwa hela na watoto chini ya miaka mitano wanapokwenda pia kupata huduma wameendelea kutozwa fedha. Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini ni nini hasa kinakwamisha huduma hii au sera hii isitekelezwe?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika vituo vyetu vya afya kumekuwa na upungufu mkubwa sana wa dawa na vifaa tiba. Je, Serikali ina mkakati gani sasa kuhakikisha kwamba vifaa tiba na dawa zinapatikana katika vituo vyetu vya afya ili watoto wetu na akinamama wanapokwenda kujifungua waweze kupata huduma hiyo? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Spika, nilijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Regina Ndege kwamba kwa kweli tumeshafanya uchunguzi wa kutosha na kujua kwamba tatizo hilo lipo, ndiyo maana straight forward tumetaka kuwaelekeza wanaohusika kufanya kazi yao. Hata kwenye presentation ya semina iliyofanywa jana kwa Wabunge wote na Wizara ya Afya tulionesha kwamba exemption ile ya akinamama na watoto inachukua asilimia 0.1 mpaka 10.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo maeneo ambayo ni 0.1 ni maeneo yale ambayo kwa kweli unakuta akinamama walitakiwa kupewa hiyo huduma bure na hawapewi; tutakwenda kuboresha kwa nguvu kuhakikisha kwamba huduma inapatikana. Ndiyo maana tumeleta vilevile kwenu ili tushirikiane kwa pamoja ili kuweza kutatua tatizo hilo.

La pili, kwenye eneo la dawa; kwenye eneo hili, Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan alishatoa bilioni 16 na najua Kamati inakwenda siku ya Jumapili, kimejengwa kiwanda kule Njombe ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha vidonge vyote vya kutosha nchi nzima kwa siku mbili tu na kimeshafika asilimia 98 kukamilika.

Mheshimiwa Spika, tayari Rais wetu, mama Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi ya bilioni 185 kwa ajili ya kununua dawa. Tukijumlisha na uelewa ambao jana tulipeana Wabunge wa kusimamia upotevu wa dawa, wanaweza kuona tuna items zaidi ya 400 za dawa, lakini tumechunguza tu items 20 ndani ya mwaka mmoja kuna upotevu wa bilioni 83. Maana yake tukishirikiana kwa pamoja sisi na viongozi tuliotaja hapa huko mbele tutaweza kufika hatua nzuri na dawa zikapatikana kwenye maeneo yetu. Ahsante sana.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusimamia kikamilifu Sera ya Afya ili akinamama wajawazito na watoto wasitozwe gharama katika vituo vya afya?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nami niulize swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, wewe ni shahidi; hii sera ni ya muda mrefu na haitekelezeki. Wabunge mnajua kwenye majimbo yetu, akinamama wajawazito, wazee na watoto chini ya miaka mitano hakuna matibabu bure. Sasa Mheshimiwa Waziri anasema atatoa miongozo, kama hakuna kitu cha kumbana mambo ni yaleyale.

Je, kwa nini kusiwe na sheria kwamba ni lazima akinamama wajawazito, watoto chini ya miaka mitano na wazee wapate matibabu bure ili wazee wasiweke tiba ya kisaikolojia tena, wakienda hospitali wapate matibabu bure? Sera imekuwepo haitekelezeki, leteni sheria kama mna dhamira njema.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge na ndiyo maana umekuwa mkali sana kwenye suala zima la bima ya afya kwa wote. Nataka kukuhakikishia tukienda kutekeleza agizo lako la suala la bima ya afya kwa wote, haya mambo yatakuwa ni historia. Kwa wakati huu miongozo iliyopo tutaendelea kuifuatilia na kusisitiza, lakini Mheshimiwa Ester Bulaya aendelee kushirikiana na sisi ili tuweze kufanya hilo litekelezeke. Ahsante sana. (Makofi)