Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kuendeleza Mradi wa Maji wa Lukululu ili kumaliza tatizo la maji katika vijiji 14 vya Jimbo la Vwawa?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru sana kwa majibu ya Serikali. Naomba nitumie nafasi hii kuishukuru sana Serikali kwa kutenga shilingi bilioni
1.3 kwa ajili ya mradi huu ambao ni wa muda mrefu. Naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika awamu ya kwanza inahusu vijiji vitano; na kwa kuwa maji haya yanatoka katika Kijiji cha Lukululu ambao ndio wanalinda hata vyanzo vya maji, lakini hawapo katika awamu ya kwanza; na kwa kuwa maji yanapotoka Kijiji cha Lukululu yanakuja Mlangali yanakwenda Shaji na Mahenje, lakini Kijiji cha Shaji ambacho kiko katikati hakiko katika mpango huu wa kwanza: -

Je, atakuwa tayari kubadilisha huu mpango ili hivi vijiji viwili, cha Lukululu ambako maji yanatoka na kile cha Shaji viwepo katika awamu ya kwanza? Hilo ni swali la kwanza.

Swali la pili: Kwa kuwa Mbewe umeitaja na imeandikwa kwenye maeneo mawili; kwenye mpango awamu ya kwanza na awamu ya pili; sasa kuna kijiji ambacho kimesahaulika kilitakiwa kiingie katika vile vijiji kumi vya awamu ya pili, ambacho ni Ihoa: -

Je, Serikali itakuwa tayari sasa kukiingiza hicho kijiji ili nacho kiwemo katika orodha ya vijiji vitakavyopata maji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hasunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa Vijiji hivi vya Lukululu na Shaji sifa yake tu namna ambavyo ipo inafaa kuingia kwenye awamu ya kwanza, hivyo hatutakariri namna ambavyo tuliweka. Kwanza, Sera ya Maji inatutaka kijiji kile ambacho chanzo kipo kiwe mnufaika namba moja, hivyo tutazingatia hilo kama Wizara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na maji kufika Ihoa, hii nayo nimeipokea. Kwa kuwa nia njema, dhamira safi ya Mheshimiwa Rais ni kuona kwamba maeneo yote yanafikiwa na huduma ya maji safi na salama, tutafikisha maji Ihoa pia. (Makofi)