Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, mpango wa kuzipandisha hadhi Sekondari za Ngweli, Ngoma A, Tamabu, Nyamatongo, Sima, Nyampande na Katunguru kuwa za Kidato cha Tano na Sita Wilayani Sengerema umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Sengerema tunazo shule 31 za Sekondari na katika hizo shule 31 Sekondari mbili ndiyo zina kidato cha Tano na Sita, Sengerema Sekondari na Nyampurukano Sekondari na zimeelemewa wanafunzi na kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja aliona ile hali ya Sengerema kwa watoto walivyowengi na wananchi wa Sengerema wanamshukuru Mwenyezi Mungu wanaendelea kufanya kazi ya ziada kwa ajili ya kuwashughulikia akinamama kupata watoto wengi kuijaza dunia.

Mheshimiwa Spika, sasa hili jambo la Sengerema kutokukosa Sekondari hizi za Kidato cha Tano, Sengerema wanafunzi wanakosa nafasi na Mheshimiwa Naibu Waziri aliona na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI alikuja kule na akaona hiyo hali. Lini sasa hili jambo litafanyika kwa haraka kwa ajili ya huyo Mdhibiti Ubora kwenda kukagua hizi shule kwa sababu zimekaguliwa mwaka huu na mwaka kesho tunategemea wanafunzi watakuwa ni wengi nini msaada wa wizara katika jambo hili, la kwanza.

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili ni kwamba Sengerema Sekondari imeelemewa na bahati nzuri Mheshimiwa Waziri alikuja pale na akatoa ahadi ya kutupa vitanda kutokana na watoto alivyoona wanalala katika mazingira magumu na Nyampurukano Sekondari pia imeelemewa ni nini msaada wa Serikali katika jambo hili ili waweze kutusaidia kwa haraka sasa katika kuzisajili shule hizi.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Tabasamu Mbunge wa Jimbo la Sengerema niweze kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ameeleza kwamba katika halmashauri yake ya Sengerema kuna Sekondari karibu 31 na katika hilo eneo kuna shule mbili tu za kidato cha tano sita na anataka kwamba tuwaagize watu wa Udhibiti Ubora kwamba waende wakakague hizi shule tuone kama zinakidhi vigezo.

Mheshimiwa Spika, na ni nitumie fursa hii najua kwamba kazi nzuri ambayo anaifanya Mheshimiwa Mbunge na bahati nzuri nilifika pale na niliona jitihada yake kubwa kujenga shule 15 kwa mpigo. Niwaagize tu Halmashauri ya Sengerema kwamba waende sasa hivi huko walipo kuanzia wiki ijao wakague na watuletee taarifa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kama maeneo haya yanakidhi vigezo ya kuanzishwa kidato cha tano na cha sita na kwa sababu tunaile programu yetu ya kuzipanua shule 100 kwa ajili ya kuziongezea madarasa na miundombinu ili kuzifanya kuwa kidato cha tano na cha sita. Kwa hiyo, tutazingatia katika ule mpango ili tuone tunaweza tutaongeza shule ngapi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili kwamba Mheshimiwa Waziri alifika kule na aliahidi nimwambie tu kabisa kwamba najua alifika shule eneo la Sengerema na aliahidi kutoa baadhi ya vitanda kuhakikisha kwamba tunaongeza idadi ya wanafunzi ama waweze kupata malazi bora. Kwa hiyo, ahadi ile ipo pale pale na itatekelezeka kama ambavyo Mheshimiwa Waziri alikuwa ameahidi na nikuhakikishie tu kwamba shule zote ambazo zitakidhi vigezo basi tutaziingiza katika mpango. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, mpango wa kuzipandisha hadhi Sekondari za Ngweli, Ngoma A, Tamabu, Nyamatongo, Sima, Nyampande na Katunguru kuwa za Kidato cha Tano na Sita Wilayani Sengerema umefikia wapi?

Supplementary Question 2

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto la Jimbo la Sengerema ni sawa sawa na Jimbo la Igalula.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Igalula hatuna shule ya kidato cha tano na sita, lakini baada ya kutambua hayo wadau na wanachi tumeweza kujikongoja na tumepata mabweni na miundombinu salama ya kuweza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita.

Je, lini Serikali itaitambua shule ya Sekondari ya Tula ili iweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita ili kupunguza uhaba wa shule katika nchi hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Venant Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi kwamba katika maeneo yale ambayo yanahitajika kuanzishwa kidato cha tano na cha sita ni lazima halmashauri husika kupitia Ofisi za Elimu pamoja na watu wa Udhibiti Ubora wanakwenda katika eneo husika wanakagua ile shule, wanatuletea hayo mapendekezo tunaona kama ina meet vile vigezo.

Kwa hiyo, kama inafikisha vile vigezo basi sisi tutakuwa tayari kuongeza fedha na baadhi ya miundombinu ili kuhakikisha tunaisajili na kupokea. Kwa hiyo, na yeye Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tutawaagiza watu katika halmashauri yake watatuletea hiyo taarifa na baada ya hiyo taarifa maana yake tutaleta majibu ya msingi kama inakidhi kupandishwa au itasubiri katika mwaka mwingine wa fedha. Ahsante sana.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, mpango wa kuzipandisha hadhi Sekondari za Ngweli, Ngoma A, Tamabu, Nyamatongo, Sima, Nyampande na Katunguru kuwa za Kidato cha Tano na Sita Wilayani Sengerema umefikia wapi?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, shule ya Sekondari Farukwa ilipandishwa hadhi na ikawa ya kidato cha tano na sita lakini baadaye wakasitisha na sababu walizofanya wasitishe tumezimaliza tayari ni lini sasa wataturudishia shule yetu ya kidato cha tano na sita. Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Monni Mbunge wa Chemba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, anasema kwamba Shule ya Farukwa ambayo ipo katika Jimbo la Chemba wameshamaliza zile changamoto kwa hiyo wanataka kujua ni lini sasa Serikali itairudisha ile shule ili sasa ianze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita. Kwa hiyo, niseme tu kwamba tutawatuma wataalam kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI watakuja kukagua kujiridhisha kama hizo vile vigezo vyote mmeshamaliza na kama itakuwa imekamilika basi nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mwaka unaokuja hiyo shule itafunguliwa na wanafunzi wataenda kusoma hapo. Ahsante sana.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, mpango wa kuzipandisha hadhi Sekondari za Ngweli, Ngoma A, Tamabu, Nyamatongo, Sima, Nyampande na Katunguru kuwa za Kidato cha Tano na Sita Wilayani Sengerema umefikia wapi?

Supplementary Question 4

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante Jimbo la Makete linakata 23, kata tatu hatuna shule za Sekondari na katika vipaumbele ambavyo nilivileta kwenye wizara ni Kata ya Mlondwe ndiyo ianze kujengwa shule ya Makete Boys na tuliahidiwa kupewa milioni mia 600, lakini hadi sasa milioni 600 hatujazipata.

Je, ni lini milioni 600 zitafika ili tuanze ujenzi wa Makete boys na baadaye tufuate shule Kigala na baadaye tufuate shule ya sekondari Bulongwa? Naomba majibu ya Serikali.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA
SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri Silinde kwa majibu mazuri sana kwa maswali yaliyotangulia nimesimama kuhusu swali lililoulizwa na Mheshimiwa Sanga ni lini shilingi milion 600 zitatoka kwa ajili ya kujenga sekondari katika Kata ambazo hazina sekondari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumekamilisha orodha ya sekondari 214 za kila Jimbo ambazo zitapata shilingi milioni 600, lakini Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema atatupa shilingi milioni 470 kilichonikwamisha hatujatoa mkeka Waheshimiwa Wabunge wanabadilisha mara kwa mara. Kwa hiyo, hapa simu yangu imekufa nilikuwa nitoe taarifa na ndiyo maana nimesimama kutoa taarifa kwa Waheshimiwa Wabunge kujiridhisha na kile kipaumbele ulichoweka cha Kata yako nitatuma ujumbe kwenye group la Wabunge kusema umpigie mtu gani, uangalie je, hiyo kata yako iliyowekwa ndiyo kata ya kipaumbele. Lakini Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yuko tayari tumekwama sisi kwa sababu Wabunge wanabadilisha badilisha.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ile shule ya Mkoa mmoja na waomba sana Waheshimiwa Wabunge tuliomba mchakato uanze kwenye RCC. Kwa hiyo, tumeandikiwa barua na Makatibu Tawala wa Mikoa, wakisema kwamba shule ile moja. Kwa hiyo, kutakuwa na 214 za kila Jimbo, halafu tutanza na moja ya kila mkoa, naomba sana Wabunge mapendekezo yametoka kwa Makatibu Tawala wa Mikoa. Kwa hiyo, tunaomba sana tumeona kuna watu wanabadilisha toa wilaya hii peleka hii sisi tumezingatia ushauri wa Makatibu Tawala wa Mikoa.

Mheshimiwa Spika, by tarehe 15 Mheshimiwa Sanga mkitupa confirmation, hela Mheshimiwa Dkt. Mwigulu yupo tayari zitakuwa zimeshaenda kwenye halmashauri zenu. (Makofi)