Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza agizo la Rais wa Awamu ya Tatu la kuitambua Kizengi kuwa Tarafa?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nataka niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na miongozo yote ambayo ameitoa hapa swali langu lilikuwa ni ahadi ya Viongozi Wakuu, hayati Dkt. Benjamini Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu ambaye alikuja katika jimbo la Igalula, Kata ya Igalula mwaka 2002 na akatangaza Tarafa ya Kizenji ambapo ilikuwa na Kata Kizengi, Tula na Loya. Tulisimama kufuata miongozo hii kwa sababu Rais alikuwa kashatamka. Sasa, je kama Serikali wana utaratibu gani wa kufuatilia kauli za Rais na kuzifanyia kazi ili tusiweze kuleta mikanganyiko ya kuwa tunaomba mara mbili mbili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Jimbo la Igalula pamoja na mambo mengine ni kubwa sana na jiografia yake ni kubwa sana. Je, ni nini mkakati wa Serikali kutoa utaratibu wa kuanzisha na kutoa maagizo ya kuanzisha maeneo ya utawala mengine, maombi mapya ili tuweze kuleta hasa maombi ya halmashauri?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MITAA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa David Protas Venant, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba halmashauri ya Igalula kwa maana ya Jimbo la Igalula linahitaji kupata Tarafa ya Kizenga, lakini pamoja na maelezo ya Mheshimiwa Mbunge kwamba ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, Serikali inatekeleza ahadi za viongozi wa kitaifa kwa utaratibu na kwa wakati, lakini kuna miongozo ambayo ni muhimu iweze kufuatwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo Serikali inaitambua na tutaifanyia kazi, lakini watendaji wameelekezwa kufuata mwongozo kwa maana kuanzishwa vikao ngazi ya vijiji, kata, wilaya na mkoa ili sasa wawasilishe maombi hayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kadri ya mwongozo na maamuzi yaweze kufanyika. Kwa hiyo, naomba kumhakikishia Mheshimiwa kwamba wakiwasilisha mambo hayo mamlaka husika itafanya tathmini na kufanya maamuzi kama tunaweza kuanzisha tarafa hiyo au viginevyo na taarifa rasmi zitapelekwa katika wilaya hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili; utaratibu huu wa kuanzisha maeneo mapya ya utawala kama nilivyotangulia kujibu kwenye swali la msingi, unaongozwa kwa miongozo ambayo ipo rasmi. Kwa hiyo kama kuna uhitaji wowote wa kuanzisha halmashauri mpya ni lazima tufuate miongozo ile. Kwa hivyo nimpe rai Mheshimiwa Mbunge na viongozi wa halmashauri husika wakafanye utaratibu wa vikao hivyo na kuleta maombi yao level ya Wizara. Ahsante.