Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID I. RAMADHANI aliuliza: - Barabara ya kutoka Singida kupitia Mji Mdogo wa Ilongero – Mtinko hadi Hydom ni muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Singida, Manyara na Simiyu. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Ilongero – Mtinko hadi Hydom kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID I. RAMADHANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri yenye natumaini ya Serikali lakini naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Mheshimiwa Waziri anatuambia kwamba mkataba umeshasainiwa tangu Oktoba, 2021 ambapo utachukua mwaka mzima mpaka 2022 mwishoni. Kwa nini sasa upembuzi yakinifu uchukue muda mrefu hivyo kwa kilomita 93 tu wakati tayari fedha zipo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Kwa kuwa hadi sasa sijaona chochote kinachoendelea katika barabara hii, Waziri yuko tayari kuongozana nami hadi site kwenda kuona na kusimamia utekelezaji wa kazi hii uanze ipasavyo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhan, Mbunge wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kilomita 93.3 ni kilomita nyingi na tunachofanya siyo tu upembuzi yakinifu ni upembezi yakinifu na usanifu wa kina ambao ndiyo utatoa sasa gharama ya hii barabara itahitaji kiasi gani. Kwa hiyo, baada ya hilo nadhani pengine kwa bajeti itakayofata ndiyo sasa tutakuwa tumepata gharama ili kuanza kuingiza kwenye mpango kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge ambao barabara hii inawahusu, mara baada ya kikao hiki cha Bunge nitatembelea Mkoa wa Singida kwani natambua barabara hii inaunganisha Singida, Manyara hadi Simiyu.

Kwa hiyo, nimejipanga kutembelea hii barabara, Mheshimiwa Mbunge awe tayari kwamba tutaongozana kuangalia hii barabara. Ahsante. (Makofi)

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. ABEID I. RAMADHANI aliuliza: - Barabara ya kutoka Singida kupitia Mji Mdogo wa Ilongero – Mtinko hadi Hydom ni muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Singida, Manyara na Simiyu. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Ilongero – Mtinko hadi Hydom kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kupitia bajeti ya mwaka huu wa fedha (2021/2022), Serikali imepamga kujenga barabara kwa kiwango cha lami Morogoro - Njombe Boda walau kwa kuanza na kilomita 50. Swali langu: Je, ni lini Serikali itatangaza zabuni walau ujenzi huu uanze kwa kilomita 50 hizi? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godwin Kunambi, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge nataka nikuhakikishie kwamba barabara zote ambazo zimetengewa fedha tayari ziko kwenye michakato ya manunuzi. Kwa hiyo, mara tu hizo hatua zitakapokamilika, nikuhakikishie kwamba zitatangazwa kwa ajili ya kuanza ujenzi. Ahsante.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. ABEID I. RAMADHANI aliuliza: - Barabara ya kutoka Singida kupitia Mji Mdogo wa Ilongero – Mtinko hadi Hydom ni muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Singida, Manyara na Simiyu. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Ilongero – Mtinko hadi Hydom kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nilitaka kuuliza swali la nyongeza kwa Wizara ya Ujenzi kwamba katika kazi zilizotangazwa na zilizoanza kufanyika sasa hivi na TANROAD kule Kigoma, nyingi zimekwama kwa sababu GN hazijatolewa. Je, mna mpango gani wa kufanya mawasiliano na Wizara ya Fedha kuhakikisha GN hizo zinatoka kabla mvua nyingi hazijaanza kunyesha katika maeneo hayo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inafanya mawasiliano na Wizara ya Fedha na tunapoongea hivi nina hakika muda siyo mrefu GN zitakuwa zimetoka ili tuweze kuanza kutekeleza hiyo miradi haraka kabla ya mvua haijakolea. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, labda kama kuna barabara ambayo ni specific ama kuna shida, hiyo haitatoka GN mpaka wajiridhishe kwamba kila kitu kimekaa sawa. Ila kwa barabara nyingine nina hakika siyo muda mrefu zabuni zote zitatangazwa baada ya kutoka hiyo GN. Ahsante.